Hamia kwenye habari

Nifanye Nini Ikiwa Ninapenda Kutazama Ponografia

Nifanye Nini Ikiwa Ninapenda Kutazama Ponografia

Unachoweza kufanya

 Elewa ponografia ni nini hasa. Ponografia ni kushushia heshima kitu ambacho Mungu aliumba kiheshimike. Kuelewa hilo kuhusu ponografia kutakusaidia ‘uchukie yaliyo mabaya.’—Zaburi 97:10.

 Fikiria madhara. Ponografia huwashushia heshima wahusika. Pia inamdhalilisha mwenye kuitazama. Biblia inasema hivi kwa sababu nzuri: “Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha.”—Methali 22:3.

 Azimia. Mwanamume mwaminifu aliyeitwa Ayubu alisema hivi: “Nimefanya agano na macho yangu yasimtazame msichana kwa kumtamani.” (Ayubu 31:1, Neno—Biblia Takatifu) Wewe pia unaweza ‘kufanya maagano’ yafuatayo:

  •  Sitatumia Intaneti nikiwa peke yangu.

  •  Nitafunga tovuti yoyote inayotokea ghafula na kuonyesha mambo machafu.

  •  Nitazungumza na rafiki mkomavu endapo nitatumbukia tena katika tatizo hili.

Kadiri unavyozidi kutazama ponografia ndivyo inavyokuwa vigumu kuiepuka

 Mwombe Mungu akusaidie. Mtunga-zaburi alimsihi Yehova Mungu hivi: “Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa.” (Zaburi 119:37, Neno—Biblia Takatifu) Mungu anataka ufaulu, na ukimwomba akusaidie, anaweza kukupa nguvu za kufanya yaliyo mema!—Wafilipi 4:13.

 Zungumza na mtu. Kuchagua mtu unayeweza kumweleza mambo ya siri ni hatua muhimu inayoweza kukusaidia kuvunja mazoea hayo.—Methali 17:17.

 Kumbuka hili: Kila wakati unapoepuka ponografia, unakuwa umepiga hatua kubwa sana. Mwambie Yehova Mungu kuhusu ushindi huo, na umshukuru kwa nguvu alizokupa. Unapoepuka ponografia, unafanya moyo wake ushangilie!—Methali 27:11.