Zaburi 119:1-176

  • Kulithamini neno la Mungu lenye thamani

    • ‘Vijana wanaweza kuisafishaje njia yao?’ (9)

    • “Ninavipenda sana vikumbusho vyako” (24)

    • “Neno lako ni tumaini langu” (74, 81, 114)

    • “Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!” (97)

    • “Ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote” (99)

    • “Neno lako ni taa ya mguu wangu” (105)

    • ‘Kiini cha neno lako ni kweli’ (160)

    • Wanaoipenda sheria ya Mungu wana amani (165)

א [Aleph] 119  Wenye furaha ni wale wasio na lawama* katika njia yao,Wanaotembea katika sheria ya Yehova.+   Wenye furaha ni wale wanaoshika vikumbusho vyake,+Wanaomtafuta kwa moyo wao wote.+   Hawatendi uovu wowote;Wanatembea katika njia zake.+   UmeamuruKwamba maagizo yako yafuatwe kwa uangalifu.+   Laiti ningeweza kubaki imara*+Ili niyashike masharti yako!   Ndipo sitaaibishwa+Ninapokazia uangalifu amri zako zote.   Nitakusifu kwa moyo mnyoofuNinapojifunza hukumu zako za uadilifu.   Nitayashika masharti yako. Kamwe usiniache kabisa. ב [Beth]   Kijana anaweza kuisafishaje njia yake? Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+ 10  Ninakutafuta kwa moyo wangu wote. Usiache nikengeuke kutoka katika amri zako.+ 11  Ninaweka neno lako moyoni mwangu kama hazina+Ili nisikutendee dhambi.+ 12  Na usifiwe, Ee Yehova;Nifundishe masharti yako. 13  Kwa midomo yangu ninatangazaHukumu zote ulizonena. 14  Ninashangilia kwa sababu ya vikumbusho vyako+Kuliko vitu vingine vyote vyenye thamani.+ 15  Nitatafakari* maagizo yako+Na kuzikazia macho njia zako.+ 16  Ninazipenda sana sheria zako. Sitalisahau neno lako.+ ג [Gimel] 17  Nitendee kwa fadhili mimi mtumishi wako,Ili niishi na kulishika neno lako.+ 18  Yafumbue macho yangu ili nione waziMambo yanayostaajabisha katika sheria yako. 19  Mimi ni mgeni tu nchini.+ Usinifiche amri zako. 20  Ninapondeka* kwa kutamani sanaHukumu zako nyakati zote. 21  Unawakemea wenye kimbelembele,Watu waliolaaniwa wanaokengeuka kutoka katika amri zako.+ 22  Niondolee* dhihaka na dharau,Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako. 23  Hata wakuu wanapoketi pamoja na kusema mambo mabaya kunihusu,Mimi mtumishi wako ninatafakari* masharti yako. 24  Ninavipenda sana vikumbusho vyako;+Navyo ni washauri wangu.+ ד [Daleth] 25  Ninalala kifudifudi mavumbini.+ Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+ 26  Nilikwambia kuhusu njia zangu, nawe ukanijibu;Nifundishe masharti yako.+ 27  Nifanye nielewe maana* ya maagizo yako,Ili niweze kutafakari* kazi zako zinazostaajabisha.+ 28  Nimekosa usingizi kwa sababu ya huzuni. Nitie nguvu kulingana na neno lako. 29  Niondolee njia ya udanganyifu,+Na unionyeshe kibali kwa kunipa sheria yako. 30  Nimechagua njia ya uaminifu.+ Ninatambua kwamba hukumu zako zinafaa. 31  Ninashikamana na vikumbusho vyako.+ Ee Yehova, usiache nikatishwe tamaa.*+ 32  Nitaifuata kwa bidii* njia ya amri zakoKwa sababu wewe huufanya moyo wangu uwe na nafasi kwa ajili yake.* ה [He] 33  Nifundishe, Ee Yehova,+ njia ya masharti yako,Nami nitaifuata mpaka mwisho.+ 34  Nipe uelewaji,Ili niweze kushika sheria yakoNa kuitii kwa moyo wangu wote. 35  Niongoze* katika njia ya amri zako,+Kwa maana ninapendezwa nayo. 36  Uelekeze moyo wangu kwenye vikumbusho vyako,Wala si kwa tamaa ya* kichoyo.+ 37  Yageuzie mbali macho yangu yasitazame mambo yasiyofaa;+Nihifadhi hai katika njia yako. 38  Nitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako,*Ili uogopwe.* 39  Niondolee aibu ninayoogopa sana,Kwa maana hukumu zako ni njema.+ 40  Tazama jinsi ninavyoyatamani sana maagizo yako! Nihifadhi hai katika uadilifu wako. ו [Waw] 41  Acha nijionee upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova,+Wokovu wako kulingana na ahadi yako;*+ 42  Kisha nitamjibu yule anayenidhihaki,Kwa maana ninalitumaini neno lako. 43  Usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,Kwa maana nimetumaini* hukumu yako. 44  Nitaishika sheria yako daima,Milele na milele.+ 45  Nami nitatembeatembea mahali salama,*+Kwa maana ninayatafuta maagizo yako. 46  Nitaongea kuhusu vikumbusho vyako mbele ya wafalme,Nami sitaaibika.+ 47  Ninazipenda sana amri zako,Naam, ninazipenda.+ 48  Nitainua mikono yangu kuelekea amri zako, ambazo ninazipenda,+Nami nitayatafakari* masharti yako.+ ז [Zayin] 49  Likumbuke neno lako ulilomwambia* mtumishi wako,Ambalo kupitia hilo unanipa tumaini.* 50  Hilo ndilo faraja yangu katika mateso yangu,+Kwa maana neno lako limenihifadhi hai. 51  Wenye kimbelembele wananidhihaki sana,Lakini sikengeuki kutoka kwenye sheria yako.+ 52  Ninazikumbuka hukumu zako za tangu zamani,+ Ee Yehova,Nazo zinanifariji.+ 53  Nimeshikwa na hasira kali kwa sababu ya waovu,Wanaoiacha sheria yako.+ 54  Masharti yako ni nyimbo kwanguPopote ninapoishi.* 55  Wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, Ee Yehova,+Ili niweze kuishika sheria yako. 56  Nimezoea kufanya hivyoKwa sababu nimeyatii maagizo yako. ח [Heth] 57  Yehova ni fungu langu;+Nimeahidi kuyashika maneno yako.+ 58  Ninakusihi* kwa moyo wangu wote;+Nionyeshe kibali+ kulingana na ahadi yako.* 59  Nimezichunguza njia zangu,Ili niirudishe miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+ 60  Ninafanya haraka wala sikawiiKuzishika amri zako.+ 61  Kamba za waovu zinanizunguka,Lakini siisahau sheria yako.+ 62  Katikati ya usiku ninaamka ili kukushukuru+Kwa sababu ya hukumu zako za uadilifu. 63  Mimi ni rafiki ya wote wanaokuogopa weweNa ya wale wanaoyatii maagizo yako.+ 64  Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, umeijaza dunia;+Nifundishe masharti yako. ט [Teth] 65  Umenitendea mema mimi mtumishi wako,Ee Yehova, kulingana na neno lako. 66  Nifundishe busara na ujuzi,+Kwa maana nimezitumaini amri zako. 67  Kabla ya kuteswa, nilikuwa nikikengeuka,*Lakini sasa ninalishika neno lako.+ 68  Wewe ni mwema+ na kazi zako ni njema. Nifundishe masharti yako.+ 69  Wenye kimbelembele hunipaka uwongo,Lakini ninayatii maagizo yako kwa moyo wangu wote. 70  Moyo wao umekufa ganzi,*+Lakini ninaipenda sana sheria yako.+ 71  Ni vema kwamba nimeteswa,+Ili nijifunze masharti yako. 72  Sheria uliyotangaza ni njema kwangu,+Kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha.+ י [Yod] 73  Mikono yako iliniumba na kunifinyanga. Nipe uelewaji,Ili nijifunze amri zako.+ 74  Wale wanaokuogopa huniona na kushangilia,Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+ 75  Ninajua, Ee Yehova, kwamba hukumu zako ni za uadilifu+Na kwamba umenitesa kwa uaminifu wako.+ 76  Tafadhali, upendo wako mshikamanifu+ na unifariji,Kulingana na ahadi yako uliyonipa* mimi mtumishi wako. 77  Nionyeshe rehema ili niendelee kuishi,+Kwa maana ninaipenda sana sheria yako.+ 78  Wenye kimbelembele na waaibishwe,Kwa maana wananikosea bila sababu.* Lakini nitayatafakari* maagizo yako.+ 79  Acha wale wanaokuogopa warudi kwangu,Wale wanaojua vikumbusho vyako. 80  Moyo wangu na uwe bila lawama katika kufuata masharti yako,+Ili nisiaibishwe.+ כ [Kaph] 81  Ninautamani sana wokovu wako,+Kwa maana neno lako ni tumaini langu.* 82  Macho yangu yanatamani sana neno lako+Huku nikisema: “Utanifariji lini?”+ 83  Kwa maana mimi ni kama kiriba cha ngozi kilichokaushwa na moshi,Lakini siyasahau masharti yako.+ 84  Mimi mtumishi wako nisubiri kwa siku ngapi? Ni lini utakapowahukumu wale wanaonitesa?+ 85  Wenye kimbelembele wananichimbia mashimo,Wale wanaoasi sheria yako. 86  Amri zako zote zinategemeka. Watu wananitesa bila sababu; nisaidie!+ 87  Karibu waniangamize kutoka duniani,Lakini sikuyaacha maagizo yako. 88  Nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu,Ili nishike vikumbusho ulivyosema. ל [Lamed] 89  Milele, Ee Yehova,Neno lako litadumu mbinguni.+ 90  Uaminifu wako umekuwepo kwa vizazi vyote.+ Umeiimarisha kabisa dunia, ili idumu.+ 91  Kwa sababu ya hukumu zako zinadumu* mpaka leo,Kwa maana zote ni watumishi wako. 92  Kama singeipenda sana sheria yako,Ningekuwa nimeangamia katika mateso yangu.+ 93  Sitayasahau kamwe maagizo yako,Kwa sababu kupitia hayo umenihifadhi hai.+ 94  Mimi ni wako; niokoe,+Kwa sababu nimeyatafuta maagizo yako.+ 95  Waovu wanasubiri kuniangamiza,Lakini ninavikazia sana fikira vikumbusho vyako. 96  Nimeona mwisho wa ukamilifu wote,Lakini amri yako haina mpaka.* מ [Mem] 97  Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!+ Ninaitafakari* mchana kutwa.+ 98  Amri yako hunifanya niwe na hekima kuliko maadui wangu,+Kwa sababu ninayo milele. 99  Nina ufahamu mwingi kuliko walimu wangu wote,+Kwa sababu ninavitafakari* vikumbusho vyako. 100  Ninatenda kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,Kwa sababu ninayatii maagizo yako. 101  Ninakataa kutembea kwenye njia yoyote ya uovu,+Ili nishike neno lako. 102  Sigeuki kando kutoka katika hukumu zako,Kwa maana umenifundisha. 103  Jinsi maneno yako yalivyo matamu kwenye kaakaa langu,Kuliko asali kinywani mwangu!+ 104  Kwa sababu ya maagizo yako ninatenda kwa uelewaji.+ Ndiyo sababu ninaichukia kila njia ya uwongo.+ נ [Nun] 105  Neno lako ni taa ya mguu wangu,Na nuru ya njia yangu.+ 106  Nimeweka kiapo, nami nitakitimiza,Kwamba nitazishika hukumu zako za uadilifu. 107  Nimeteseka sana.+ Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na neno lako.+ 108  Tafadhali yafurahie matoleo yangu ya hiari ya kukusifu,*+ Ee Yehova,Na unifundishe hukumu zako.+ 109  Uhai wangu umo hatarini daima,*Lakini sijaisahau sheria yako.+ 110  Waovu wamenitegea mtego,Lakini sijakengeuka kutoka katika maagizo yako.+ 111  Ninavichukua vikumbusho vyako kuwa mali yangu ya kudumu,*Kwa maana hivyo ni shangwe ya moyo wangu.+ 112  Nimeazimia* kuyatii masharti yakoNyakati zote, mpaka mwisho. ס [Samekh] 113  Ninawachukia watu wenye moyo nusunusu,*+Lakini ninaipenda sheria yako.+ 114  Wewe ni mahali pangu pa kujificha na ngao yangu,+Kwa maana neno lako ni tumaini langu.*+ 115  Kaeni mbali nami, enyi waovu,+Ili nizishike amri za Mungu wangu. 116  Nitegemeze kama ulivyoahidi,*+Ili niendelee kuishi;Usiache tumaini langu libadilike na kunikatisha tamaa.*+ 117  Nitegemeze ili niokolewe;+Kisha nitayakazia uangalifu daima masharti yako.+ 118  Unawakataa wote wanaokengeuka kutoka katika masharti yako,+Kwa maana ni waongo na wadanganyifu. 119  Unawatupilia mbali waovu wote walio duniani kana kwamba ni takataka.*+ Ndiyo sababu ninavipenda vikumbusho vyako. 120  Mwili wangu unatetemeka kwa sababu ya kukuhofu;Ninaogopa hukumu zako. ע [Ayin] 121  Nimetenda yaliyo ya haki na uadilifu. Usiniache mikononi mwa wale wanaonikandamiza! 122  Nihakikishie hali njema mimi mtumishi wako;Wenye kimbelembele wasinikandamize. 123  Macho yangu yamechoka nikiungojea wokovu wako+Na ahadi yako ya* uadilifu.+ 124  Nitendee mimi mtumishi wako kwa upendo mshikamanifu,+Na unifundishe masharti yako.+ 125  Mimi ni mtumishi wako; nipe uelewaji,+Ili nijue vikumbusho vyako. 126  Wakati umefika wa Yehova kutenda,+Kwa maana wameivunja sheria yako. 127  Ndiyo sababu ninazipenda amri zakoKuliko dhahabu, hata dhahabu bora.*+ 128  Kwa hiyo, ninayaona mafundisho* yote yanayotoka kwako kuwa yanafaa;+Ninaichukia kila njia ya uwongo.+ פ [Pe] 129  Vikumbusho vyako ni vizuri sana. Ndiyo sababu ninavishika. 130  Kufunuliwa kwa maneno yako huleta nuru,+Na humpa uelewaji mtu asiye na uzoefu.+ 131  Ninakifumbua wazi kinywa changu na kutweta,*Kwa sababu ninazitamani sana amri zako.+ 132  Nigeukie na kunionyesha kibali,+Kama unavyowatendea* wale wanaolipenda jina lako.+ 133  Ziongoze hatua zangu kwa usalama* kupitia neno lako;Jambo lolote ovu lisinitawale.+ 134  Niokoe* kutoka kwa wanadamu wanaokandamiza,Nami nitayatii maagizo yako. 135  Ufanye uso wako uniangazie* mimi mtumishi wako,+Na unifundishe masharti yako. 136  Macho yangu yanatiririkwa na machoziKwa sababu watu hawatii sheria yako.+ צ [Tsade] 137  Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+Na hukumu zako ni za haki.+ 138  Vikumbusho unavyotoa ni vya uadilifuNavyo vinategemeka kabisa. 139  Bidii yangu inanila,+Kwa sababu maadui wangu wameyasahau maneno yako. 140  Neno lako ni safi kabisa,+Nami mtumishi wako ninalipenda.+ 141  Mimi ni duni na mwenye kudharauliwa;+Hata hivyo, sijayasahau maagizo yako. 142  Uadilifu wako ni uadilifu wa milele,+Na sheria yako ni kweli.+ 143  Hata nikipatwa na taabu na shida,Nitaendelea kuzipenda sana amri zako. 144  Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa milele. Nipe uelewaji,+ ili niendelee kuishi. ק [Qoph] 145  Ninakuita kwa moyo wangu wote. Nijibu, Ee Yehova. Nitayashika masharti yako. 146  Ninakulilia wewe; niokoe! Nitashika vikumbusho vyako. 147  Nimeamka kabla ya mapambazuko* ili nililie msaada,+Kwa maana maneno yako ni tumaini langu.* 148  Macho yangu hufunguka kabla ya makesha ya usiku,Ili nitafakari* neno lako.+ 149  Isikie sauti yangu kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+ Ee Yehova, nihifadhi hai kulingana na haki yako. 150  Watu wenye mwenendo wa aibu* hunikaribia;Wako mbali sana na sheria yako. 151  Wewe uko karibu nami, Ee Yehova,+Na amri zako zote ni kweli.+ 152  Zamani za kale nilijifunza kuhusu vikumbusho vyako,Ambavyo umeviweka vidumu milele.+ ר [Resh] 153  Yatazame mateso yangu na uniokoe,+Kwa maana sijaisahau sheria yako. 154  Nitetee* na uniokoe;+Nihifadhi hai kulingana na ahadi yako.* 155  Wokovu uko mbali sana na waovu,Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+ 156  Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+ Nihifadhi hai kulingana na haki yako. 157  Wanaonitesa na pia maadui wangu ni wengi;+Lakini sijakengeuka kutoka katika vikumbusho vyako. 158  Ninawatazama wenye hila kwa chuki kali,Kwa sababu hawalishiki neno lako.+ 159  Tazama jinsi ninavyoyapenda sana maagizo yako! Ee Yehova, nihifadhi hai kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+ 160  Kiini hasa cha neno lako ni kweli,+Na hukumu zako zote za uadilifu zinadumu milele. ש [Sin] au [Shin] 161  Wakuu wananitesa+ bila sababu,Lakini moyo wangu unayahofu maneno yako.+ 162  Ninashangilia kwa sababu ya neno lako+Kama mtu anayepata nyara nyingi. 163  Nauchukia uwongo—nauchukia sana+Ninaipenda sheria yako.+ 164  Mara saba kwa siku ninakusifu weweKwa sababu ya hukumu zako za uadilifu. 165  Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi;+Hakuna chochote kinachoweza kuwakwaza.* 166  Ninayatazamia matendo yako ya wokovu, Ee Yehova,Nami ninazishika amri zako. 167  Ninavishika vikumbusho vyako,Nami navipenda sana.+ 168  Ninayatii maagizo yako na vikumbusho vyako,Kwa maana unajua mambo yote ninayotenda.+ ת [Taw] 169  Kilio changu cha kuomba msaada na kikufikie wewe, Ee Yehova.+ Nifanye nielewe, kulingana na neno lako.+ 170  Ombi langu la kutaka kibali na lifike mbele zako. Niokoe, kama ulivyoahidi.* 171  Midomo yangu na ifurikwe na sifa,+Kwa maana wewe hunifundisha masharti yako. 172  Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako,+Kwa maana amri zako zote ni za uadilifu. 173  Mkono wako na uwe tayari kunisaidia,+Kwa sababu nimechagua kutii maagizo yako.+ 174  Ninautamani sana wokovu wako, Ee Yehova,Nami ninaipenda sana sheria yako.+ 175  Acha niishi ili nikusifu;+Hukumu zako na ziwe msaada wangu. 176  Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea.+ Nitafute mimi mtumishi wako,Kwa maana sijazisahau amri zako.+

Maelezo ya Chini

Au “wanaoshika utimilifu.”
Tnn., “Laiti njia zangu zingekuwa zimeimarishwa kabisa.”
Au “Nitajifunza.”
Au “Nafsi yangu inapondeka.”
Tnn., “Vingirisha mbali nami.”
Au “ninajifunza.”
Tnn., “njia.”
Au “kujifunza.”
Au “niaibishwe.”
Tnn., “Nitakimbia katika.”
Au labda, “huufanya moyo wangu uwe na ujasiri.”
Au “Nitembeze.”
Au “kwa faida za.”
Au “neno lako.”
Au labda, “Ambayo hutolewa kwa wale wanaokuogopa.”
Au “neno lako.”
Au “ninangojea.”
Au “mahali penye nafasi kubwa.”
Au “nitajifunza.”
Au “Kumbuka ahadi yako uliyompa.”
Au “Ambalo ulinifanya nisubiri.”
Au “Katika nyumba ninamoishi kama mgeni.”
Au “Ninautuliza (ninatafuta tabasamu ya) uso wako.”
Au “neno lako.”
Au “nilikuwa nikitenda dhambi bila kukusudia.”
Tnn., “hauna hisia, ni kama mafuta.”
Au “ninalingojea neno lako.”
Au “neno lako ulilonipa.”
Au labda, “kwa kusema uwongo.”
Au “nitajifunza.”
Au “ninalingojea neno lako.”
Yaani, kazi zake zote za uumbaji.
Tnn., “ni pana sana.”
Au “Ninajifunza kuihusu.”
Au “ninajifunza.”
Tnn., “matoleo ya hiari ya kinywa changu.”
Au “Nafsi yangu imo mikononi mwangu daima.”
Au “urithi wangu wa milele.”
Tnn., “Nimeuelekeza moyo wangu.”
Au “moyo uliogawanyika.”
Au “Ninalingojea neno lako.”
Au “kulingana na neno lako.”
Au “liaibishwe.”
Neno la Kiebrania linalotafsiriwa “takataka” katika mstari huu linarejelea uchafu unaotoka katika fedha au dhahabu inapoyeyushwa.
Au “neno lako la.”
Au “iliyosafishwa.”
Au “maagizo.”
Tnn., “kuhemahema.”
Tnn., “Kulingana na uamuzi wako kuwaelekea.”
Au “Zifanye hatua zangu ziwe imara.”
Tnn., “Nikomboe.”
Au “utabasamu kunielekea.”
Au “alfajiri.”
Au “Ninayangojea maneno yako.”
Au “nijifunze.”
Au “mwenendo mpotovu.”
Au “Iendeshe kesi yangu.”
Au “neno lako.”
Au “Hakuna cha kuwakwaza.”
Au “kulingana na neno lako.”