Mezali 8:1-36

  • Hekima yenye kuzungumuziwa kama mutu inaongea (1-36)

    • ‘Mimi ni mwanzo kabisa wa kazi za Mungu’ (22)

    • ‘Nilikuwa pembeni ya Mungu nikiwa fundi wa kazi’ (30)

    • ‘Nilipenda sana wana wa binadamu’ (31)

8  Je, hekima haiite kwa sauti kubwa? Je, utambuzi haupandishe sauti yake?+   Kwenye nafasi za juu+ pembeni ya barabara,Inasimama kwenye makutano ya barabara.   Karibu na milango mikubwa yenye kupeleka kwenye muji,Kwenye miingilio ya milango,Inaendelea kulia kwa sauti kubwa:+   “Ninawaita, Enyi watu;Ninalalamikia kila mutu.*   Ninyi watu wenye hawana uzoefu, mujifunze werevu;+Ninyi wajinga, mujipatie moyo wenye uelewaji.*   Musikilize, kwa maana mambo yenye ninasema ni ya maana,Midomo yangu inasema mambo yenye kuwa sawa;   Kwa maana kinywa changu kinasema ukweli kwa sauti ya chini,Na midomo yangu inachukia sana jambo lenye uovu.   Maneno yote ya kinywa changu ni yenye haki. Kati ya maneno hayo, hakuna neno moja lenye kupengama ao lenye kupotoka.   Yote yako wazi kabisa kwa mutu mwenye utambuziNa yako sawa kwa wale wenye wamepata ujuzi. 10  Mukamate nizamu yangu pa nafasi ya feza,Na ujuzi pa nafasi ya zahabu safi sana,+ 11  Kwa maana hekima ni ya muzuri kuliko marijani;*Vitu vingine vyote vyenye kutamanika haviwezi kulinganishwa nayo. 12  Mimi, hekima, ninakaa pamoja na werevu;Nimepata ujuzi na uwezo wa kufikiri.+ 13  Kumuogopa Yehova kunamaanisha kuchukia ubaya.+ Ninachukia kujiinua na kiburi+ na njia ya uovu na maneno yenye kupotoka.+ 14  Niko na shauri la muzuri na hekima yenye kutenda;+Uelewaji+ na nguvu+ ni vyangu. 15  Kwa musaada wangu wafalme wanaendelea kutawala,Na maofisa wakubwa wanatunga sheria za haki.+ 16  Kwa musaada wangu wakubwa wanaendelea kutawala,Na watu wenye vyeo wanahukumu kwa haki. 17  Ninapenda wale wenye kunipenda,Na wale wenye kunitafuta watanipata.+ 18  Niko na utajiri na utukufu,Mali yenye kudumu* na haki. 19  Matunda yangu ni ya muzuri kuliko zahabu, hata kuliko zahabu yenye kusafishwa,Na mazao yangu ni ya muzuri kuliko feza ya muzuri kabisa.+ 20  Ninatembea katika njia ya uadilifu,*Katikati ya njia za haki; 21  Ninapatia wale wenye kunipenda uriti mwingi,Na ninajaza madepo yao. 22  Yehova aliniumba nikiwa mwanzo wa njia yake,+Mwanzo kabisa wa kazi zake za zamani sana.+ 23  Niliwekwa tangu nyakati za zamani,*+Tangu mwanzo, nyakati za zamani mbele dunia ikuwe.+ 24  Wakati hapakukuwa maji yenye kuenda chini sana,+ nilizaliwa,*Wakati hapakukuwa chemchemi zenye kujaa sana maji. 25  Mbele milima haijawekwa mahali pake,Mbele vilima vikuwe, nilizaliwa, 26  Wakati alikuwa hajaumba dunia na maeneo yake ya mashambaWala madonge ya kwanza ya udongo wa dunia. 27  Wakati alitayarisha mbingu,+ nilikuwa pale;Wakati alichora mwisho* kwenye uso wa maji,+ 28  Wakati alifanya imara* mawingu yenye kuwa juu,Wakati aliweka musingi wa chemchemi za mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana, 29  Wakati alitilia bahari sheriaKwamba maji yake yasipite agizo lake,+Wakati aliweka* misingi ya dunia, 30  Wakati huo nilikuwa pembeni yake nikiwa fundi wa kazi.+ Mimi ndiye alipenda sana+ siku kwa siku;Nilifurahi mbele yake wakati wote;+ 31  Nilifurahia dunia yake yenye kuikaliwa na watu,Na wana wa binadamu* ndio nilipenda zaidi sana. 32  Na sasa, wana wangu, munisikilize;Ndiyo, wenye furaha ni wale wenye wanashika njia zangu. 33  Musikilize nizamu+ na mukuwe na hekima,Na musiipuuze hata kidogo. 34  Mwenye furaha ni mutu mwenye ananisikilizaKwa kuja mbele ya wakati* kwenye milango yangu siku kwa siku,Kwa kungojea karibu na miimo ya milango yangu; 35  Kwa maana mwenye kunipata atapata uzima,+Na anakubaliwa na Yehova. 36  Lakini mwenye kunipuuza anajiumiza yeye mwenyewe,*Na wale wenye kunichukia wanapenda kifo.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “wana wa binadamu.”
Tnn., “muelewe moyo.”
Ao “Kanuni zenye kuritiwa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “zamani za kale.”
Ao “nilizaliwa kama vile kwa maumivu ya kuzaa.”
Tnn., “muzunguko.”
Tnn., “alifanya nguvu.”
Ao “alitunga sheria kuhusu.”
Ao “wanadamu.”
Ao “Kwa kukesha.”
Ao “anaumiza nafsi yake.”