Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 A2

Mambo ya Maana ya Tafsiri Hii Yenye Ilirekebishwa

Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilitolewa katika Kiingereza katika mwaka wa 1950, na Biblia​​Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yenye kuenea ilichapishwa katika mwaka wa 1961. Tangu wakati huo, makumi ya mamilioni ya wasomaji katika luga zaidi ya mia moja (100) wamepata faida kutokana na tafsiri hii yenye haina makosa lakini pia yenye kuwa mwepesi kusoma ya Biblia yenye imetafsiriwa kutokana na luga za kwanza.

Hata hivyo, katika miaka makumi tano (50) yenye imepita, luga zimebadilika. Halmashauri ya sasa ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mupya ilitambua uhitaji wa kufanya jambo fulani kwa ajili ya mabadiliko hayo ili kugusa moyo wa musomaji wa leo. Kwa sababu hiyo, mabadiliko mengi yamefanywa katika mutindo wa kuandika na maneno katika tafsiri hii yenye imerekebishwa, ili kutimiza mambo haya:

  • Kutumia luga ya sasa, na yenye kueleweka. Kwa mufano, neno “ustahimilivu,” pengine linaweza kueleweka kimakosa kumaanisha “kuteseka kwa wakati murefu.” Hata hivyo, wazo lenye kufichwa hapa ni kujizuia kwa kutaka, na linaonyeshwa muzuri zaidi kwa kutumia neno “uvumilivu.” (Wagalatia 5:22) Kuliko kutumia maneno “fazili zenye upendo,” wazo limetolewa kwa njia yenye kuwa wazi zaidi kwa kutumia maneno “upendo mushikamanifu.” Hilo linatoa maana ya neno la Biblia lenye mara nyingi linatumiwa pamoja na neno “uaminifu.” (Zaburi 36:5; 89:1) Maneno “siku za miaka ya maisha” yamebadilishwa kuwa “miaka.” (Mwanzo 25:7; 47:8, 9; 2 Samweli 19:34) Katika tafsiri hii yenye ilirekebishwa, maneno “mwenendo mupotovu” yamebadilishwa kuwa “mwenendo mupotovu wa bila haya” na maneno “karamu za kupindukia” yamebadilishwa kuwa “karamu za kupitisha mipaka.” (Wagalatia 5:19-​21) Maneno “wakati usio na kipimo” yamebadilishwa na maneno kama vile “milele,” “-a kudumu,” “-a milele,” ao “zamani sana,” ili kuleta maana ya kweli katika kila habari.​—Mwanzo 3:22; Kutoka 31:16; Zaburi 133:3; Muhubiri 1:4; Mika 5:2.

    Neno “mbegu” katika Kiebrania cha zamani na Kigiriki cha zamani lilitumiwa ili kuzungumuzia mbegu ya mumea na pia uzao wa mwanadamu, ao wazao, ao mbegu za uzazi. Kwa sababu haiko jambo la kawaida katika Swahili (Congo) kutumia neno “mbegu” ili kuzungumuzia wanadamu, neno hilo lilibadilishwa na maneno yenye yanaleta maana yenye inakusudiwa kulingana na habari yenye kuzungumuziwa. (Mwanzo 1:11; 22:17; 48:4; Matayo 22:24; Yohana 8:37) Katika habari nyingi, neno “uzao” ndilo linatumiwa sasa wakati wa kuzungumuzia ahadi ya Edeni, yenye kupatikana kwenye Mwanzo 3:15.

    Kitenzi (verbe) cha Kiingereza “impale” (kuchoma ao kuingiza mutu muti) kilitumiwa katika matoleo ya zamani ya Kiingereza ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ili kuzungumuzia namna Yesu aliuawa. Hata kama neno hilo linaweza kutumiwa kuhusu namna Yesu alipigiliwa misumari kwenye muti wa mateso, mara nyingi linatumiwa ili kuonyesha njia ya zamani ya kuua mutu kwa kuingiza muti wenye kuchongwa ndani ya mwili wa mutu na kumuacha aninginie kwenye muti huo. Kwa kuwa Yesu hakuchomwa ao kuingizwa muti wa mateso, tafsiri ya Kiingereza yenye ilirekebishwa inatumia maneno kama vile “kuuawa kwenye muti” na “kupigiliwa misumari kwenye muti” ili kuzungumuzia namna Yesu aliwekwa kwenye muti wa mateso.​—Matayo 20:19; 27:31, 35.

  • Kufanya maneno ya Biblia yakuwe wazi zaidi. Maneno fulani yenye yalitumiwa katika matoleo ya zamani ya Kiswahili ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yalihitaji mara nyingi kufasiriwa ili yaeleweke muzuri. Kwa mufano, neno la Kiebrania “Sheoli” na neno la Kigiriki “Hadesi” yanatumiwa katika Biblia ili kuzungumuzia kaburi la wanadamu wote. Maneno hayo hayajulikane na watu wengi, na neno “Hadesi” liko na maana mbili kutokana na matumizi yake katika hadisi za kuwazia-wazia za Wagiriki. Kwa hiyo, maneno hayo mbili yalibadilishwa na kile chenye waandikaji wa Biblia walimaanisha, ni kusema, “Kaburi.” Sasa maneno “Sheoli” na “Hadesi” yanatiwa katika maelezo ya chini.​—Zaburi 16:10; Matendo 2:27.

    Katika matoleo ya zamani, neno la Kiebrania neʹphesh na neno la Kigiriki psy·kheʹ yalitafsiriwa kila mahali “nafsi.” Kwa kuwa watu wengi wanaelewa mubaya maana ya neno “nafsi,” kufanya vile kulisaidia musomaji kuona namna waandikaji wa Biblia wenye waliongozwa na roho ya Mungu walitumia maneno hayo ya luga za kwanza. Kwa kutegemea habari yenye kuzungumuziwa, maneno hayo yanaweza kumaanisha (1) mutu, (2) uzima wa mutu, (3) viumbe vyenye uzima, (4) tamaa ya mutu na hamu yake ya kula ao, katika habari fulani, (5) hata watu wenye wamekufa. Hata hivyo, kwa kuwa matumizi kama hayo ya neno “nafsi” hayako ya kawaida katika Swahili (Congo), uamuzi ulichukuliwa ili kutafsiri maneno hayo ya luga za kwanza kulingana na maana yake ya kweli, mara nyingi kwa kuyawekea maelezo ya chini yenye kusema “Ao ‘nafsi.’” (Angalia, kwa mufano, Mwanzo 1:20; 2:7; Mambo ya Walawi 19:28; Zaburi 3:2; Mezali 16:26; Matayo 6:25.) Lakini, katika mashairi (poèmes) fulani ao katika habari fulani zenye kujulikana muzuri, neno “nafsi” liliachwa katika habari kubwa, pamoja na maelezo ya chini yenye kupeleka mutu kwenye Maana ya Maneno ao yenye kuonyesha njia ingine yenye neno hilo linaweza kutafsiriwa.​—Kumbukumbu la Torati 6:5; Zaburi 131:2; Mezali 2:10; Matayo 22:37.

    Vilevile, neno “figo” lilibakia wakati linamaanisha kiungo cha mwili. Hata hivyo, wakati linatumiwa kwa njia ya mufano katika maandiko kama vile Zaburi 7:9 na 26:2 na Ufunuo 2:23, wazo la kweli la “hisia za ndani kabisa” ao “mawazo ya ndani kabisa” linatolewa katika habari kubwa, na wazo la neno kwa neno linatolewa katika maelezo ya chini.

    Neno la Swahili (Congo) “moyo” kama vile linatafsiriwa kutoka katika Kiebrania na Kigiriki, liko na maana ya kweli-kweli na maana ya mufano, kwa hiyo lilibakia mara nyingi katika mistari ya Biblia. Lakini, katika habari za kidogo kwenye maana haikukuwa wazi, lilitafsiriwa kwa njia yenye kuwa wazi zaidi. Kwa mufano, katika kitabu cha Mezali, maneno “kupungukiwa moyoni” sasa yametafsiriwa ‘kutokuwa na akili ya muzuri’ ao “kukosa akili ya muzuri” na wazo la neno kwa neno linatolewa katika maelezo ya chini. Maneno mengine, kwa mufano, “unono,” “mwili,” na “pembe,” yalishugulikiwa kwa njia hiyo pia kulingana na habari yenye kuzungumuziwa. (Mwanzo 45:18; Muhubiri 5:6; Yobu 16:15) Maneno fulani kati ya hayo yanaelezwa katika sehemu “Maana ya Maneno ya Biblia.”

  • Kuifanya ikuwe mwepesi zaidi kusoma. Katika matoleo ya zamani ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Kiswahili, maneno ya kusaidia yalitumiwa ili kuonyesha kama kitenzi (verbe) cha Kiebrania kinaonyesha tendo lenye kuendelea ao tendo lenye limekamilika. Kwa mufano, tendo lenye kuendelea lenye kuonyeshwa mara nyingi na vitenzi vyenye vinaonyesha kama tendo linaendelea lilionyeshwa na maneno kama vile “akaendelea” na maneno mengine ya namna hiyo. Mukazo wenye kuonyeshwa mara nyingi na kitenzi cha tendo lenye limekamilika katika Kiebrania ulionyeshwa kwa kuongeza maneno kama vile “hakika,” “lazima,” “kwa kweli,” na maneno mengine ya namna hiyo. Matokeo ni kwamba, maneno hayo yalitumiwa mara maelfu katika habari. Katika tafsiri hii yenye ilirekebishwa, maneno ya kusaidia yalibakia katika habari fulani kwa kutumia maneno kama vile “kuendelea,” na “kuzoea” wakati kulikuwa sababu kabisa ya kueleza kuwa tendo ni la kuendelea. (Mwanzo 3:9; 34:1; Mezali 2:4) Lakini, maneno hayo ya kusaidia yaliondolewa ili usomaji ukuwe mwepesi zaidi wakati maneno ya kusaidia hayakukuwa ya lazima sana ili kutoa maana ya luga ya kwanza.

  • Kutafsiri wazo la kweli la maneno yenye kuzungumuzia jinsia. Nomino za Kiebrania na za Kigiriki zinaonyesha jinsia ya kiume ao jinsia ya kike, na katika Kigiriki, kuko pia jinsia yenye haiko ya kiume wala ya kike. Hata hivyo, wakati fulani, kuonyesha jinsia ya neno la luga ya kwanza kunaweza kuficha maana ya kweli. Katika Kiebrania na Kigiriki, nomino zenye kuwa katika uwingi kwa ujumla ni za jinsia ya kiume, hapana tu wakati zinataja wanaume peke yao lakini pia wakati zinataja wanaume na wanamuke. Kwa mufano, hata kama maneno “wana wa Israeli” yanaweza kumaanisha wana kumi na mbili (12) wa Yakobo, mara nyingi yanamaanisha taifa lote la Israeli, wanaume na wanamuke. (Mwanzo 46:5; Kutoka 35:29) Kwa hiyo, katika tafsiri yenye ilirekebishwa, mara nyingi maneno hayo yalitafsiriwa “Waisraeli” ili kuonyesha kwamba yanazungumuzia taifa lote. Vilevile, maneno “mvulana asiye na baba” yalitafsiriwa “mutoto mwenye hana baba” ao “yatima” ili kuonyesha kwamba yanaweza kuzungumuzia mutoto mwanaume ao mwanamuke. Kwa upande mwingine, kwa kuwa Biblia inatumia jinsia ya kiume ili kuzungumuzia Mungu na Mwana wake, na pia malaika mbalimbali na pepo wachafu, hakuna sababu ya kutumia maneno yenye hayaonyeshe jinsia kama vile inafanywa katika tafsiri fulani za sasa.

  • Mambo yenye kuonyesha uwingi wa nafsi ya pili katika toleo la Kiingereza yameondolewa. Matoleo ya zamani ya Kiingereza yalionyesha kama viwakilishi “you” (wewe ao ninyi) na “your” (yako ao yenu) na vitenzi vya nafsi ya pili vilikuwa katika umoja ao uwingi kwa kutumia herufi za mukubwa kidogo ili kuonyesha uwingi. Jambo hilo liliondolewa katika tafsiri yenye ilirekebishwa ya Kiingereza, lakini wasomaji wanaweza kuangalia tafsiri ya zamani ya Kiingereza ili kujionea jambo hilo.

    Mabadiliko yote katika habari ya Biblia yalifanywa kisha kusali, kwa uangalifu, na kwa heshima kubwa kuelekea kazi ya muzuri ya Halmashauri ya kwanza ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mupya.

Mambo mengine ya maana ya tafsiri hii yenye ilirekebishwa:

Toleo hili la Biblia liko na hesabu ya kidogo ya maelezo ya chini. Kwa ujumla maelezo ya chini yako katika aina hizi:

  • “Ao” Njia zingine zenye habari inaweza kutafsiriwa ­kutokana na Kiebrania, Kiaramu, ao Kigiriki, zenye zinaweza kuleta wazo lilelile la ujumla.​—Mwanzo 1:2, maelezo ya chini kwenye maneno “nguvu ya utendaji”; Yoshua 1:8, “sauti ya chini.”

  • “Ao pengine” Njia zingine zenye habari inaweza kutafsiriwa zenye zinaweza kutoa wazo la ujumla lenye linakubalika lakini lenye kuwa tofauti.​—Mwanzo 21:6, “atacheka pamoja na mimi”; Zekaria 14:21, “Mukanaani.”

  • “Tnn.” Tafsiri ya neno kwa neno kutokana na Kiebrania, Kiaramu, ao Kigiriki, ao maana ya musingi ya maneno ya luga ya kwanza.​—Mwanzo 30:22, “mimba”; Kutoka 32:9, “kichwa-nguvu.”

  • Maana na habari za kuongezea Maana ya majina (Mwanzo 3:17, “Adamu”; Kutoka 15:23, “Mara”); maelezo juu ya vipimo na uzito (Mwanzo 6:15, “mikono”); kitangulizi cha kiambishi (pronom) (Mwanzo 38:5, “Huyo”); habari za lazima katika Nyongeza na katika Maana ya Maneno.​—Mwanzo 37:35, “Kaburi”; Matayo 5:22, “Gehena.”

Sehemu ya mwanzo, yenye kichwa “Habari Fulani za Kujifunza Katika Neno la Mungu,” iko na habari za mafundisho ya musingi yenye kupatikana katika Biblia. Kisha kuko “Oroza ya Vitabu vya Biblia,” “Oroza ya Maneno ya Biblia,” na “Maana ya Maneno ya Biblia.” Sehemu “Maana ya Maneno” inasaidia musomaji aelewe maneno yenye yalichaguliwa kulingana na namna yanatumiwa katika Biblia. Nyongeza A iko na sehemu hizi: “Kanuni za Kutafsiri Biblia,” “ Mambo ya Maana ya Tafsiri Hii Yenye Ilirekebishwa,” “Namna Biblia Ilitufikia,” “Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kiebrania,” “Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo,” “Muchoro: Manabii na Wafalme wa Yuda na wa Israeli,” na “Matukio Makubwa ya Maisha ya Yesu Katika Dunia.” Nyongeza B iko na karte, michoro, na habari zingine za lazima kwa ajili ya wanafunzi wa Biblia wenye bidii.

Katika Biblia yenyewe, kila kitabu kinaonyesha vichwa vya habari zenye kuwa ndani ya kila sura, pamoja na mistari yenye kuhusiana na vichwa hivyo, na hilo linamupatia musomaji wazo la ujumla la kitabu chote. Kila ukurasa uko na referanse za katikati za maana zaidi kutoka katika matoleo ya zamani, zenye kuonyesha maandiko ya Biblia yenye kuhusiana na maandiko mengine.