Mezali 10:1-32

  • Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake (1)

  • Mikono yenye bidii inaleta utajiri (4)

  • Kusema maneno mengi kunaleta makosa (19)

  • Baraka ya Yehova inamufanya mutu kuwa tajiri (22)

  • Kumuogopa Yehova kunarefusha maisha (27)

10  Mezali za Sulemani.+ Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+Lakini mwana mupumbavu ni huzuni kwa mama yake.   Mali zenye zilipatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,Lakini haki ndiyo inaokoa katika kifo.+   Yehova hataacha mwenye haki akae* na njaa,+Lakini ataima waovu mambo yenye wanatamani sana.   Mikono yenye uvivu italeta umaskini,+Lakini mikono yenye bidii inaleta utajiri.+   Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto,Lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.+   Baraka ziko juu ya kichwa cha mwenye haki,+Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.   Kumbukumbu la* mwenye haki litabarikiwa,+Lakini jina la muovu litaoza.+   Mutu mwenye moyo wa hekima atakubali mafundisho,*+Lakini mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+   Mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu atatembea kwa usalama,+Lakini mwenye kupotosha njia zake atajulikana.+ 10  Mwenye kufinya jicho lake kwa udanganyifu anatokeza huzuni,+Na ule mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+ 11  Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima,+Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.+ 12  Chuki ndiyo inachochea ugomvi,Lakini upendo unafunika makosa yote.+ 13  Hekima inapatikana kwenye midomo ya mutu mwenye utambuzi,+Lakini fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa mutu mwenye hana akili ya muzuri.*+ 14  Watu wenye hekima wanaweka ujuzi kama hazina,+Lakini kinywa cha mupumbavu kinaalika uharibifu.+ 15  Mali ya* tajiri ni muji wake wenye ngome. Uharibifu wa maskini ni umaskini wao.+ 16  Kazi ya mwenye haki inaongoza kwenye uzima;Lakini mazao ya muovu yanaongoza kwenye zambi.+ 17  Mwenye kutii nizamu ni njia yenye inapeleka kwenye uzima,*Lakini mwenye anapuuza karipio anapoteza wengine. 18  Mwenye kuficha chuki yake anasema uongo,+Na mwenye kueneza habari zenye kuumiza* ni mujinga. 19  Wakati maneno ni mengi, kosa haliwezi kuepukwa,+Lakini mutu yeyote mwenye anazuia midomo yake anatenda kwa busara.+ 20  Ulimi wa mwenye haki uko kama feza ya muzuri kabisa,+Lakini moyo wa muovu uko na mafaa kidogo. 21  Midomo ya mwenye haki inakulisha* wengi,+Lakini wapumbavu wanakufa kwa sababu ya kukosa akili.+ 22  Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri,+Naye haongeze maumivu* yoyote pamoja nayo. 23  Kujiingiza katika mwenendo wa haya ni kama muchezo kwa mujinga,Lakini hekima ni ya mutu mwenye utambuzi.+ 24  Kile muovu anaogopa kitamufikia;Lakini tamaa ya mwenye haki itatimizwa.+ 25  Wakati zoruba itapita, muovu hatakuwa tena,+Lakini mwenye haki ni musingi milele.+ 26  Kama siki* kwenye meno na moshi katika macho,Ni vile mutu muvivu iko* kwa ule mwenye kumutuma.* 27  Kumuogopa Yehova kunarefusha maisha,+Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+ 28  Tumaini* la wenye haki linaleta shangwe,+Lakini tumaini la waovu litapotea.+ 29  Njia ya Yehova ni ngome kwa mutu mwenye hana lawama,+Lakini ni uharibifu kwa watenda maovu.+ 30  Mwenye haki hataangushwa hata siku moja,+Lakini waovu hawatakaa tena katika dunia.+ 31  Kinywa cha mwenye haki kinatokeza* hekima,Lakini ulimi wenye kupotoka utakatwa. 32  Midomo ya mwenye haki inajua mambo yenye kupendeza,Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi ya mwenye haki ikae.”
Ao “Sifa ya.”
Tnn., “amri.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “Kitu cha maana cha.”
Ao pengine, “iko kwenye njia yenye inapeleka kwenye uzima.”
Ao “habari zenye haziko hakika.”
Ao “inaongoza.”
Ao “huzuni; magumu.”
Ao “vinaigre.”
Ao “eko.”
Ao “bwana wake wa kazi.”
Ao “Tarajio.”
Ao “kinazaa tunda la.”