Mezali 17:1-28

  • Usilipe ubaya kwa wema (13)

  • Ondoka mbele ugomvi uanze (14)

  • Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote (17)

  • “Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri” (22)

  • Mutu mwenye utambuzi anazuia maneno yake (27)

17  Afazali kipande chenye kukauka cha mukate mahali kwenye kuko amani*+Kuliko nyumba yenye kujaa karamu* pamoja na ugomvi.+   Mutumishi mwenye ufahamu atatawala juu ya mwana mwenye anatenda kwa haya;Atapokea uriti kama mumoja wa ndugu za mwana huyo.   Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+Lakini Yehova ndiye anachunguza mioyo.+   Mutu muovu anasikiliza maneno yenye kuumiza,Na mutu mudanganyifu anasikiliza ulimi wenye uovu.+   Mutu yeyote mwenye kuchekelea maskini anatukana Mutengenezaji wake,+Na kila mutu mwenye anafurahia musiba wa mwingine hatakosa kupewa azabu.+   Wajukuu ni taji kwa wenye wamezeeka,Na baba* ni utukufu wa wana* wao.   Maneno manyoofu* hayamufae mupumbavu.+Namna gani maneno ya uongo kwa mutawala!*+   Zawadi ni kama jiwe lenye samani kwa mwenye kuwa nayo;*+Kila mahali kwenye anageukia, linamuletea mafanikio.+   Kila mutu mwenye anasamehe* kosa anatafuta upendo,+Lakini ule mwenye anaendelea kuongea juu ya jambo anatenganisha marafiki wa karibu.+ 10  Kemeo linamugusa moyo zaidi mutu mwenye uelewaji+Kuliko kumupiga mujinga mara mia moja (100).+ 11  Mutu mubaya anatafuta uasi tu,Lakini mujumbe mwenye hana huruma atatumwa ili kumupatia azabu.+ 12  Ni muzuri zaidi kukutana na dubu mwenye amepoteza vitoto vyakeKuliko kukutana na mujinga katika upumbavu wake.+ 13  Kama mutu analipa ubaya kwa wema,Ubaya hautaondoka katika nyumba yake.+ 14  Kuanzisha vita ni kama kufungua mulango mukubwa wa mafuriko;*Mbele ugomvi uanze, ondoka.+ 15  Mutu yeyote mwenye kumuhesabia muovu kuwa hana kosa na mutu yeyote mwenye kumuhukumu mwenye haki kuwa na kosa+—Wote wawili ni chukizo kwa Yehova. 16  Kuko faida gani kwa mujinga kuwa na uwezo wa kupata hekimaWakati hana moyo wa kuipata?*+ 17  Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote+Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+ 18  Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anapana mukono na kukubaliKulipia mwingine mukopo mbele ya jirani yake.+ 19  Mutu mwenye anapenda ugomvi anapenda kosa.+ Kila mutu mwenye anainua mahali pake pa kuingilia anaalika taabu.+ 20  Mutu mwenye kupotoka katika moyo hatapata mafanikio,*+Na ule mwenye kusema maneno ya udanganyifu ataanguka katika uharibifu. 21  Baba mwenye anazaa mutoto mwenye hana akili atakuwa na huzuni;Na baba ya mutoto mwenye hana akili hana furaha.+ 22  Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri,*+Lakini roho yenye kupondwa inamaliza mutu nguvu.*+ 23  Mutu muovu atakamata rushwa* kwa uficho*Ili apotoshe njia ya haki.+ 24  Hekima iko kabisa mbele ya mutu mwenye utambuzi,Lakini macho ya mujinga yanaenda huku na huku mupaka kwenye miisho ya dunia.+ 25  Mwana mujinga analetea baba yake huzuniNa kuletea ule mwenye alimuzaa maumivu ya moyo.*+ 26  Haiko muzuri kumupatia mwenye haki azabu,*Na kupiga viboko watu wenye kuheshimiwa ni kinyume na mambo yenye kuwa sawa. 27  Mutu mwenye ujuzi anazuia maneno yake,+Na mutu mwenye utambuzi atabakia mutulivu.*+ 28  Hata mupumbavu mwenye anabakia kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,Na ule mwenye anafunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.

Maelezo ya Chini

Tnn., “zabihu.”
Ao “utulivu.”
Ao “wazazi.”
Ao “watoto.”
Ao “mutu mwenye cheo.”
Ao “ya muzuri.”
Ao “ni jiwe lenye kufanya mwenye kuwa nalo akubaliwe.”
Tnn., “mwenye anafunika.”
Ao “kufungua ukuta wa maji.” Tnn., “kuachilia maji.”
Ao “Wakati hana akili ya muzuri?”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “mema.”
Ao “inakausha kabisa mifupa.”
Ao “unasaidia mutu kupona.”
Ao “kata-midomo.”
Tnn., “rushwa kutoka katika kifua.”
Tnn., “uchungu.”
Ao “kulipisha mwenye haki amande.”
Tnn., “atabakia na roho yenye kutulia.”