Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 6

Biblia Ilitabiri Nini Juu ya Masiya?

UNABII

“Wewe, Ee Betlehemu Efrata, . . . mwenye atatawala katika Israeli kwa ajili yangu atatokea kwako.”

Mika 5:2

UTIMIZO

“Kisha Yesu kuzaliwa katika Betlehemu ya ­Yudea katika siku za mufalme Herode, angalia! watu wenye elimu ya ­nyota kutoka Mashariki walikuja Yerusalemu.”

Matayo 2:1

UNABII

“Wanagawana nguo zangu kati yao wenyewe, na ­wanapigia nguo zangu kura.”

Zaburi 22:18

UTIMIZO

“Sasa, kisha maaskari kumupigilia Yesu misumari kwenye muti, wakakamata nguo zake za inje na kuzigawanya katika sehemu ine (4) . . . Lakini nguo hiyo ya ­ndani haikukuwa na mushono, ilikuwa imesukwa kuanzia juu mupaka chini. Basi wakaambiana: ‘Tusiipasue, lakini tuipigie kura ili kuamua itakuwa ya nani.’”

Yohana 19:23, 24

UNABII

“Analinda mifupa yake yote; hakuna mumoja kati ya mifupa yake wenye umevunjwa.”

Zaburi 34:20

UTIMIZO

“Wakati walikuja kwa Yesu, waliona kwamba alikuwa amekwisha kufa, kwa hiyo hawakuvunja miguu yake.”

Yohana 19:33

UNABII

“Alitobolewa kwa silaha kwa ajili ya ukosaji wetu.”

Isaya 53:5

UTIMIZO

“Mumoja wa maaskari akamuingiza mukuki kwenye ubavu, na mara moja damu na maji vikatoka.”

Yohana 19:34

UNABII

“Wakalipa malipo yangu, vipande makumi tatu (30) vya feza.”

Zekaria 11:12, 13

UTIMIZO

“Kisha mumoja wa wale Kumi na Mbili (12), ule mwenye aliitwa Yuda Iskariote, akaenda kwa wakubwa wa makuhani na kusema: ‘Mutanipatia nini ili nimusaliti kwenu?’ Wakasikilizana kumupatia vipande makumi tatu (30) vya feza.”

Matayo 26:14, 15; 27:5