Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 1

Mungu Ni Nani?

“Wajue kwamba wewe, mwenye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Mwenye Kuwa Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Zaburi 83:18

“Mujue kwamba Yehova ni Mungu. Yeye ndiye alituumba, na sisi tuko mali yake.”

Zaburi 100:3

“Mimi ni Yehova. Hilo ndilo jina langu; sipatie mutu yeyote utukufu wangu, wala sipatie sanamu za kuchongwa sifa yangu.”

Isaya 42:8

“Kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa.”

Waroma 10:13

“Kwa kweli, kila nyumba inajengwa na mutu fulani, lakini ule mwenye alijenga vitu vyote ni Mungu.”

Waebrania 3:4

“Muinue macho yenu mbinguni na muone. Ni nani ameumba vitu hivi? Ni Ule mwenye kutokeza jeshi lao kwa hesabu; anaviita vyote kwa jina. Kwa sababu ya nguvu zake nyingi zenye musukumo na nguvu zake zenye kuogopesha, hakuna hata moja kati ya hizo yenye kukosekana.”

Isaya 40:26