Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Kujifunza Katika Neno la Mungu

NAMNA YA KUPATA MAANDIKO KATIKA BIBLIA

Biblia ni mukusanyo wa vitabu vidogo-vidogo makumi sita na sita (66). Inagawanywa katika sehemu mbili: Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu (“Agano la Kale”) na Maandiko ya Kigiriki (“Agano Jipya”). Kila kitabu cha Biblia kinagawanywa katika sura na mistari. Wakati maandiko yanatajwa, namba ya kwanza kisha jina la kitabu inaonyesha sura, na namba yenye kufuata ao namba zenye kufuata zinaonyesha mustari ao mistari. Kwa mufano, Mwanzo 1:1 maana yake Mwanzo sura ya 1, mustari wa 1.