Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

A3

Namna Biblia Ilitufikia

Mutungaji na Mwanzilishi wa Biblia ndiye pia Mulinzi wake. Yeye ndiye alifanya maneno haya yaandikwe:

“Neno la Mungu wetu linadumu milele.”Isaya 40:8.

Maneno hayo ni ya kweli, hata kama hakuna maandishi ya kwanza ya Biblia ya Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu * ao ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yenye kupatikana mupaka leo. Basi, namna gani tunaweza kuwa hakika kama mambo yenye kuwa katika Biblia yenye tuko nayo leo ndiyo yalikuwa kabisa katika maandishi ya kwanza yenye yaliongozwa na roho ya Mungu?

WAANDIKAJI WA KOPI WANALINDA NENO LA MUNGU

Kuhusu Maandiko ya Kiebrania, iliwezekana kwa sababu ya desturi ya zamani yenye iliwekwa na Mungu, mwenye alisema kama habari ilipaswa kuandikwa kwenye kopi mbalimbali. * Kwa mufano, Yehova aliagiza kwamba wafalme wa Israeli wajifanyie kopi zao wenyewe za Sheria yenye kuandikwa. (Kumbukumbu la Torati 17:18) Zaidi ya hayo, Mungu alipatia Walawi daraka la kulinda Sheria na kuifundisha watu. (Kumbukumbu la Torati 31:26; Nehemia 8:7) Kisha Wayahudi kupelekwa katika uhamisho kule Babiloni, kikundi cha waandikaji, ao waandishi (Wasoferi), kilitokea. (Ezra 7:6, maelezo ya chini) Kisha, waandishi hao waliandika kopi nyingi za vile vitabu 39 vya Maandiko ya Kiebrania.

Kwa mamia ya miaka, waandishi waliandika kopi za vitabu hivyo kwa uangalifu. Katika kipindi cha Enzi za Kati, kikundi cha waandishi Wayahudi wenye kujulikana kuwa Wamasora waliendeleza desturi hiyo. Maandishi ya zamani zaidi ya Kimasora yenye kuenea ni Kodeksi ya Leningrad, ni ya tangu miaka ya 1008/1009 K.K.Y. Hata hivyo, katikati ya karne ya 20 (1901-​2000), maandishi 220 hivi ya Biblia ao vipande vya maandishi vilivumbuliwa kati ya Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi. Maandishi hayo ya Biblia yalikuwa ya zamani kwa zaidi ya miaka elfu moja hivi kuliko Kodeksi ya Leningrad. Kulinganisha Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi na Kodeksi ya Leningrad kunahakikisha jambo hili la maana: Hata kama Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi viko na tofauti fulani za maneno, hakuna hata moja ya tofauti hizo yenye inabadilisha ujumbe wenyewe.

Namna gani kuhusu vile vitabu makumbi mbili na saba (27) vya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo? Vitabu hivyo viliandikwa kwanza na mitume fulani wa Yesu Kristo na wanafunzi wengine kidogo wa kwanza. Kwa kufuata desturi ya waandishi Wayahudi, Wakristo wa zamani waliandika kopi za vitabu hivyo. (Wakolosai 4:16) Hata kama Mutawala Muroma Diokletiani na wengine walijaribu kuharibu maandishi yote ya kwanza ya Kikristo, maelfu ya vipande na maandishi ya zamani vimelindwa mupaka siku zetu.

Maandishi ya Kikristo yalitafsiriwa pia katika luga zingine. Tafsiri za kwanza za Biblia zinatia ndani tafsiri za luga za zamani kama vile Kiarmenia, Kikopti, Kietiopia, Kijeorjia, Kilatini, na Kisiria.

KUCHAGUA MAANDISHI YA KIEBRANIA NA YA KIGIRIKI ILI KUTAFSIRI

Kopi zote za maandishi ya zamani ya Biblia hazina maneno yaleyale. Basi, namna gani tunaweza kujua mambo yenye yalikuwa katika maandishi ya kwanza?

Hali hiyo inaweza kulinganishwa na ya mwalimu mwenye anaomba kila mumoja wa wanafunzi wake mia moja (100) aandike kopi moja ya sura ya kitabu fulani. Hata kama baadaye ile sura yenye kuwa na maandishi ya kwanza inapotea, kulinganisha zile kopi mia moja kutaonyesha tu maandishi ya kwanza. Hata kama kila mwanafunzi anaweza kufanya makosa fulani, ni vigumu sana kuwazia kwamba wanafunzi wote wamefanya kabisa makosa yaleyale. Vilevile, wakati watu wenye elimu nyingi wanalinganisha maelfu ya vipande na kopi za vitabu vya Biblia vya zamani vyenye wamepata, wanaweza kutambua makosa ya waandikaji wa kopi hizo na kujua maandishi ya kwanza.

“Inaweza kusemwa kwa uhakika kwamba hakuna maandishi mengine ya zamani yenye yaliandikwa bila makosa kama maandishi hayo”

Namna gani tunaweza kuwa hakika kwamba mawazo yenye kuwa katika maandishi ya kwanza ya Biblia yametufikia bila makosa? Wakati mutu mwenye elimu nyingi William H. Green alitoa maelezo juu ya Maandiko ya Kiebrania, alisema hivi: “Inaweza kusemwa kwa uhakika kwamba hakuna maandishi mengine ya zamani yenye yaliandikwa bila makosa kama maandishi hayo.” Kuhusu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ao yenye kuitwa Agano Jipya, mutu mwenye elimu nyingi ya Biblia F. F. Bruce aliandika hivi: “Uhakika wa maandishi yetu ya Agano Jipya ni mwingi zaidi kuliko uhakika wa maandishi ya waandikaji wengi wa zamani, na hakuna mutu mwenye anaweza kujaribu kupinga maandishi hayo.” Alisema tena hivi: “Kama Agano Jipya lingekuwa mukusanyo wa maandishi yenye hayako ya kidini, kwa ujumla, ukweli wake ungekubaliwa bila mashaka yoyote.”

Sura ya 40 ya kitabu cha Isaya katika Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi (vya mwaka wa 125 mupaka 100 M.K.Y.)

Wakati yanalinganishwa na maandishi ya Kiebrania ya karibu miaka elfu moja baadaye, tofauti za kidogo-kidogo tu ndizo zilipatikana, zaidi sana katika namna maneno yanaandikwa

Sura ya 40 ya kitabu cha Isaya katika Kodeksi ya Aleppo, maandishi ya maana sana ya Kiebrania ya Wamasora ya karibu mwaka wa 930 K.K.Y

Maandishi ya Kiebrania: Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Maandiko ya Kiebrania (1953-​1960 ya Kiingereza) ilitegemea Biblia Hebraica, ya Rudolf Kittel. Tangu wakati huo, matoleo yenye yalirekebishwa ya maandishi ya Kiebrania, ni kusema, Biblia Hebraica Stuttgartensia na Biblia Hebraica Quinta, yametia ndani utafiti wa hivi karibuni wenye ulitegemea Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi na maandishi mengine ya zamani. Maandishi hayo ya watu wenye elimu nyingi yalichukua maandishi ya Kodeksi ya Leningrad katika habari kubwa pamoja na maelezo ya chini yenye kuwa na maneno ya kulinganisha kutoka katika maandishi mengine, kutia ndani pantateki ya Kisamaria, Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi, Septante ya Kigiriki, Targumi za Kiaramu, Vulgate ya Kilatini, na Peshitta ya Kisiria. Biblia zote mbili, ni kusema, Biblia Hebraica Stuttgartensia na Biblia Hebraica Quinta zilichunguzwa wakati wa kutayarisha Biblia hii yenye ilirekebishwa ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

Maandishi ya Kigiriki: Katika mwisho wa karne ya 19 (1801-​1900), watu wenye elimu nyingi B. F. Westcott na F.J.A. Hort walilinganisha maandishi ya Biblia na vipande vya maandishi vyenye vilikuwa wakati walikuwa wanatayarisha maandishi ya Kigiriki yenye waliona kuwa yanatafsiri muzuri zaidi mawazo ya maandishi ya kwanza. Katikati ya karne ya 20 (1901-​2000), Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mupya ilitumia maandishi hayo kuwa musingi wa tafsiri yake. Mafunjo mengine ya zamani, yenye kuwaziwa kuwa ni ya karne ya pili (101-​200) na karne ya tatu (201-​300) K.K.Y., yalitumiwa pia. Tangu wakati huo, mafunjo mengine yamepatikana. Zaidi ya hayo, maandishi kama yale ya Nestle na Aland na ya Chama cha Sosaiti za Biblia (UBS) yanaonyesha uchunguzi wa hivi karibuni wa watu wenye elimu nyingi. Mambo fulani kati ya yale yenye yalipatikana katika utafiti huo yaliingizwa katika tafsiri hii yenye ilirekebishwa.

Kwa kutegemea maandishi hayo, inaonekana wazi kama mistari fulani ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yenye kupatikana katika tafsiri za zamani, kama vile King James Version, ilikuwa tu yenye iliongezwa na waandikaji wa kopi wa baadaye na hayakukuwa hata kidogo sehemu ya Maandiko yenye yaliongozwa na roho ya Mungu. Hata hivyo, kwa sababu mugawanyo wa mistari wenye kukubaliwa katika tafsiri za Biblia ulikuwa tayari umewekwa katika karne ya 16 (1501-​1600), kuondoa mistari hiyo sasa kunatokeza sehemu zenye kuwa wazi katika namna mistari inapangwa katika Biblia nyingi. Mistari hiyo ni Matayo 17:21; 18:11; 23:14; Marko 7:16; 9:44, 46; 11:26; 15:28; Luka 17:36; 23:17; Yohana 5:4; Matendo 8:37; 15:34; 24:7; 28:29; na Waroma 16:24. Katika toleo hili lenye lilirekebishwa, mistari hiyo yenye iliondolewa iko na maelezo ya chini yenye inaonyesha kwenye mustari huo haukuwekwa.

Kuhusu umalizio murefu wa Marko 16 (mistari ya 9-​20), umalizio mufupi wa Marko 16, na maneno yenye kupatikana kwenye Yohana 7:53–​8:11, ni wazi kwamba hakuna mustari hata mumoja wa mistari hiyo wenye uliwekwa katika maandishi ya kwanza. Kwa hiyo, maandishi hayo ya uongo hayakuwekwa katika tafsiri hii yenye ilirekebishwa. *

Maneno mengine yamerekebishwa ili kuleta wazo lenye watu wenye elimu nyingi wanakubali kwa ujumla kuwa linapatana zaidi na maandishi ya kwanza. Kwa mufano, kulingana na maandishi fulani, Matayo 7:13 inasema: “Muingie kupitia mulango mwembamba kwa sababu mulango ni mukubwa na barabara yenye kuongoza kwenye uharibifu ni kubwa.” Katika matoleo ya zamani ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, maneno “mulango ni mukubwa” hayakuwekwa katika maandishi. Lakini, uchunguzi zaidi wa maandishi ya zamani ulionyesha kwamba maneno “mulango mukubwa” yalikuwa kabisa katika maandishi ya kwanza. Kwa hiyo yaliwekwa katika toleo hili. Kuko marekebisho mengi ya namna hiyo. Lakini, marekebisho hayo ni ya kidogo, na kati ya hayo hakuna hata moja lenye linabadilisha ujumbe wa musingi wa Neno la Mungu.

Maandishi ya mafunjo ya 2 Wakorinto 4:13–​5:4 ya karibu mwaka wa 200 K.K.Y.

^ fu. 5 Kuanzia hapa yataitwa tu kuwa Maandiko ya Kiebrania.

^ fu. 7 Sababu moja yenye ilifanya ikuwe lazima kufanya kopi za maandishi hayo ni kwamba maandishi ya kwanza yaliandikwa kwenye vitu vyenye vinaweza kuharibika.

^ fu. 18 Maelezo zaidi kuhusu sababu zenye zinafanya mistari hiyo ionekane kuwa ya uongo yanapatikana katika maelezo ya chini ya Les Saintes Écritures​—Traduction du monde nouveau avec notes et références, yenye ilichapishwa katika mwaka wa 1995.