Mezali 25:1-28

  • Kuweka siri (9)

  • Maneno yenye kuchaguliwa muzuri (11)

  • Kuheshimia wakati wa wengine wa kuwa peke yao (17)

  • Kukusanya makaa juu ya kichwa cha adui (21, 22)

  • Habari ya muzuri ni kama maji ya baridi (25)

25  Hizi pia ni mezali za Sulemani,+ zenye watu wa Hezekia+ mufalme wa Yuda waliandika:*   Ni utukufu wa Mungu kuweka jambo likiwa siri,+Na utukufu wa wafalme ni kuchunguza jambo kwa undani.   Kama vile mbingu ziko juu na kama vile dunia iko na urefu kuenda chini,Vilevile moyo wa wafalme hauchunguzike.   Ondoa takataka kwenye feza,Nayo itatoka ikiwa imesafishwa kabisa.+   Ondoa muovu mbele ya mufalme,Na kiti chake cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika haki.+   Usijipatie heshima mbele ya mufalme,+Na usikae kati ya watu wa maana,+   Kwa maana ni muzuri zaidi yeye akuambie, “Kuja hapa juu,” Kuliko akupatishe haya mbele ya mutu mwenye cheo.+   Usipeleke haraka-haraka mashitaka kwenye tribinali,Kwa maana utafanya nini kisha kama jirani yako anakupatisha haya?+   Utetee shida yako pamoja na jirani yako,+Lakini usifunue mambo yenye uliambiwa kwa siri,*+ 10  Ili mwenye kukusikiliza asikupatishe hayaNa ili usieneze habari ya mubaya* yenye haiwezi kukusanywa tena. 11  Kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa*Ni vile pia neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa.+ 12  Kama hereni la sikio la zahabu na pambo la zahabu safiNi vile pia mukaripiaji mwenye hekima kwa sikio lenye kusikia.+ 13  Kama baridi ya teluji* siku ya mavunoNi vile pia mujumbe muaminifu kwa wale wenye walimutumaKwa maana mujumbe huyo anaburudisha bwana wake.*+ 14  Kama mawingu na upepo wenye haulete mvuaNi vile pia mutu mwenye anajisifu kuhusu zawadi yenye haijatolewa hata kidogo.*+ 15  Kwa uvumilivu kamanda anashawishiwa,Na ulimi laini* unaweza kuvunja mufupa.+ 16  Ukipata asali, kula tu yenye unahitaji,Kwa maana ukikula nyingi sana, unaweza kuitapika.+ 17  Muguu wako usifike mara nyingi katika nyumba ya jirani yako,Ili asikuchoke na kukuchukia. 18  Kama gongo* ya vita na upanga na mushale wenye kuwa na makaliNi vile pia mutu mwenye anatoa ushahidi wa uongo juu ya jirani yake.+ 19  Kama jino lenye kuvunjika ao muguu wenye kuyumba-yumbaNi vile pia kutumainia mutu mwenye hategemeke* nyakati za taabu. 20  Kama mutu mwenye anatosha nguo siku ya baridiNa kama siki* yenye kumwangwa kwenye chumvi ya asiliNi vile pia mutu mwenye kuimbia moyo wenye huzuni nyimbo.+ 21  Kama adui yako* iko* na njaa, umupatie mukate akule;Kama iko* na kiu, umupatie maji akunywe,+ 22  Kwa maana utakuwa unakusanya makaa yenye kuwaka juu ya kichwa chake,*+Na Yehova atakupatia zawabu. 23  Upepo wa kaskazini unaleta mvua kubwa,Na ulimi wenye kupiga porojo unaleta uso wenye kasirani.+ 24  Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumbaKuliko kuishi katika nyumba moja na bibi mugomvi.*+ 25  Kama maji ya baridi juu ya nafsi* yenye kuchokaNi vile pia habari ya muzuri yenye inatoka katika inchi ya mbali.+ 26  Kama chemchemi yenye matope na kisima chenye kuharibikaNi vile pia mwenye haki ambaye anakubali kufuata* muovu. 27  Haiko muzuri kula asali nyingi sana,+Wala haiko utukufu kujitafutia utukufu wako mwenyewe.+ 28  Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukutaNi vile pia mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake.*+

Maelezo ya Chini

Ao “walifanya kopi na kukusanya.”
Ao “siri za wengine.”
Ao “habari ya mubaya yenye haiko hakika.”
Ao “vikalio vya feza.”
Ao “neige.”
Ao “nafsi ya bwana wake.”
Tnn., “anajisifu kuhusu zawadi ya uongo.”
Ao “wenye upole.”
Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
Ao pengine, “mudanganyifu.”
Ao “vinaigre.”
Tnn., “mwenye anakuchukia.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ni kusema, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.
Ao “musumbufu.”
Ao “mwenye anakubaliana na.” Tnn., “mwenye anayumba-yumba mbele ya.”
Ao “mwenye anashindwa kuzuia roho yake.”