Mezali 14:1-35

  • Moyo unajua uchungu wake mwenyewe (10)

  • Njia yenye inaonekana kuwa sawa inaweza kuleta kifo (12)

  • Mujinga anaamini kila neno (15)

  • Tajiri iko na marafiki wengi (20)

  • Moyo mutulivu unapatia mwili uzima (30)

14  Mwanamuke mwenye hekima kabisa anajenga nyumba yake,+Lakini mwanamuke mupumbavu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.   Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova,Lakini ule mwenye njia zake ni za udanganyifu* anamuzarau Yeye.   Fimbo ya kiburi iko katika kinywa cha mupumbavu,Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.   Kwenye hakuna ngombe, chombo cha kukulishia wanyama kiko safi,Lakini nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.   Shahidi muaminifu hatasema uongo,Lakini shahidi wa uongo anasema uongo kila wakati anapumua.+   Mutu mwenye kuchekelea wengine anatafuta hekima lakini haipate hata kidogo,Lakini ujuzi unakuja kwa urahisi kwa mutu mwenye uelewaji.+   Kaa mbali na mutu mupumbavu,Kwa maana hautapata ujuzi kwenye midomo yake.+   Kwa hekima, mutu mwerevu anaelewa njia yenye anafuata,Lakini wajinga wanadanganywa* na upumbavu wao.+   Wapumbavu wanachekelea hatia,*+Lakini watu wanyoofu wako tayari kufanya mapatano.* 10  Moyo unajua uchungu wake mwenyewe,*Na hakuna mutu wa inje mwenye anaweza kushiriki katika furaha yake. 11  Nyumba ya waovu itaharibiwa,+Lakini hema ya watu wanyoofu itasitawi. 12  Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,+Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+ 13  Hata katika kicheko moyo unaweza kusikia maumivu,Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni. 14  Mutu mwenye kupotoka katika moyo atavuna matokeo ya njia zake,+Lakini mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.+ 15  Mujinga* anaamini kila neno,Lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.+ 16  Mwenye hekima ni muangalifu na anaepuka uovu,Lakini mujinga hahangaike,* na anajiaminia sana. 17  Mutu mwenye kukasirika haraka anatenda kwa ujinga,+Lakini mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo* anachukiwa. 18  Mujinga* atariti upumbavu,Lakini werevu wanavalishwa taji la ujuzi.+ 19  Watu wabaya watalazimika kuinama mbele ya watu wema,Na waovu watainama kwenye milango mikubwa ya wenye haki. 20  Maskini anachukiwa hata na majirani wake,+Lakini tajiri iko* na marafiki wengi.+ 21  Mwenye anazarau jirani yake anatenda zambi,Lakini mutu yeyote mwenye anaonyesha huruma watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+ 22  Je, wale wenye kufanya mipango mibaya hawatapotea njia? Lakini wale wenye nia ya kutenda mema watapata upendo mushikamanifu na uaminifu.+ 23  Kila namna ya kazi ya nguvu iko na faida,Lakini maongezi bure yanaleta umaskini.+ 24  Taji la wenye hekima ni mali yao;Lakini upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.+ 25  Shahidi wa kweli anaokoa uzima,*Lakini shahidi mudanganyifu anasema uongo kila wakati anapumua. 26  Kuko tumaini lenye nguvu katika kumuogopa Yehova,+Na woga huo utakuwa kimbilio la watoto wake.+ 27  Kumuogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo. 28  Wingi wa watu ni utukufu wa mufalme,+Lakini mutawala mwenye hana raia ameanguka. 29  Mutu mwenye hakasirike haraka iko* na utambuzi mwingi,+Lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.+ 30  Moyo mutulivu unapatia mwili uzima,*Lakini wivu unaozesha mifupa.+ 31  Mwenye anapunja mutu wa hali ya chini anatukana Mutengenezaji wake,+Lakini mutu yeyote mwenye anasikilia maskini huruma anamutukuza Mungu.+ 32  Uovu wa muovu utamushusha chini,Lakini mwenye haki atapata kimbilio katika uaminifu-mushikamanifu wake.+ 33  Hekima inakaa kimya katika moyo wa mutu mwenye uelewaji,+Lakini inapaswa kujijulisha kati ya wajinga. 34  Haki inainua taifa,+Lakini zambi ni haya kwa taifa. 35  Mufalme anafurahia mutumishi mwenye anatenda kwa ufahamu,+Lakini kasirani yake inawaka juu ya ule mwenye kutenda kwa haya.+

Maelezo ya Chini

Ao “zenye kupotoka.”
Ao pengine, “wajinga wanadanganya wengine.”
Ao “wanafanya muzaha wakati wanaombwa kufanya marekebisho.”
Ao “Lakini kuko nia njema kati ya watu wanyoofu.”
Ao “uchungu wa nafsi yake.”
Ao “Mwenye hana uzoefu.”
Ao “iko na kasirani kali.”
Ao “mutu mwenye uwezo wa kufikiri.”
Ao “Mwenye hana uzoefu.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi.”
Ao “eko.”
Ao “afya ya muzuri.”