Mezali 14:1-35
14 Mwanamuke mwenye hekima kabisa anajenga nyumba yake,+Lakini mwanamuke mupumbavu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova,Lakini ule mwenye njia zake ni za udanganyifu* anamuzarau Yeye.
3 Fimbo ya kiburi iko katika kinywa cha mupumbavu,Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.
4 Kwenye hakuna ngombe, chombo cha kukulishia wanyama kiko safi,Lakini nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.
5 Shahidi muaminifu hatasema uongo,Lakini shahidi wa uongo anasema uongo kila wakati anapumua.+
6 Mutu mwenye kuchekelea wengine anatafuta hekima lakini haipate hata kidogo,Lakini ujuzi unakuja kwa urahisi kwa mutu mwenye uelewaji.+
7 Kaa mbali na mutu mupumbavu,Kwa maana hautapata ujuzi kwenye midomo yake.+
8 Kwa hekima, mutu mwerevu anaelewa njia yenye anafuata,Lakini wajinga wanadanganywa* na upumbavu wao.+
9 Wapumbavu wanachekelea hatia,*+Lakini watu wanyoofu wako tayari kufanya mapatano.*
10 Moyo unajua uchungu wake mwenyewe,*Na hakuna mutu wa inje mwenye anaweza kushiriki katika furaha yake.
11 Nyumba ya waovu itaharibiwa,+Lakini hema ya watu wanyoofu itasitawi.
12 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,+Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
13 Hata katika kicheko moyo unaweza kusikia maumivu,Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.
14 Mutu mwenye kupotoka katika moyo atavuna matokeo ya njia zake,+Lakini mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.+
15 Mujinga* anaamini kila neno,Lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.+
16 Mwenye hekima ni muangalifu na anaepuka uovu,Lakini mujinga hahangaike,* na anajiaminia sana.
17 Mutu mwenye kukasirika haraka anatenda kwa ujinga,+Lakini mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo* anachukiwa.
18 Mujinga* atariti upumbavu,Lakini werevu wanavalishwa taji la ujuzi.+
19 Watu wabaya watalazimika kuinama mbele ya watu wema,Na waovu watainama kwenye milango mikubwa ya wenye haki.
20 Maskini anachukiwa hata na majirani wake,+Lakini tajiri iko* na marafiki wengi.+
21 Mwenye anazarau jirani yake anatenda zambi,Lakini mutu yeyote mwenye anaonyesha huruma watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+
22 Je, wale wenye kufanya mipango mibaya hawatapotea njia?
Lakini wale wenye nia ya kutenda mema watapata upendo mushikamanifu na uaminifu.+
23 Kila namna ya kazi ya nguvu iko na faida,Lakini maongezi bure yanaleta umaskini.+
24 Taji la wenye hekima ni mali yao;Lakini upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.+
25 Shahidi wa kweli anaokoa uzima,*Lakini shahidi mudanganyifu anasema uongo kila wakati anapumua.
26 Kuko tumaini lenye nguvu katika kumuogopa Yehova,+Na woga huo utakuwa kimbilio la watoto wake.+
27 Kumuogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo.
28 Wingi wa watu ni utukufu wa mufalme,+Lakini mutawala mwenye hana raia ameanguka.
29 Mutu mwenye hakasirike haraka iko* na utambuzi mwingi,+Lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.+
30 Moyo mutulivu unapatia mwili uzima,*Lakini wivu unaozesha mifupa.+
31 Mwenye anapunja mutu wa hali ya chini anatukana Mutengenezaji wake,+Lakini mutu yeyote mwenye anasikilia maskini huruma anamutukuza Mungu.+
32 Uovu wa muovu utamushusha chini,Lakini mwenye haki atapata kimbilio katika uaminifu-mushikamanifu wake.+
33 Hekima inakaa kimya katika moyo wa mutu mwenye uelewaji,+Lakini inapaswa kujijulisha kati ya wajinga.
34 Haki inainua taifa,+Lakini zambi ni haya kwa taifa.
35 Mufalme anafurahia mutumishi mwenye anatenda kwa ufahamu,+Lakini kasirani yake inawaka juu ya ule mwenye kutenda kwa haya.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “zenye kupotoka.”
^ Ao pengine, “wajinga wanadanganya wengine.”
^ Ao “wanafanya muzaha wakati wanaombwa kufanya marekebisho.”
^ Ao “Lakini kuko nia njema kati ya watu wanyoofu.”
^ Ao “uchungu wa nafsi yake.”
^ Ao “Mwenye hana uzoefu.”
^ Ao “iko na kasirani kali.”
^ Ao “mutu mwenye uwezo wa kufikiri.”
^ Ao “Mwenye hana uzoefu.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “nafsi.”
^ Ao “eko.”
^ Ao “afya ya muzuri.”