Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 19

Vitabu Mbalimbali vya Biblia Vinazungumuzia Nini?

MAANDIKO YA KIEBRANIA (“AGANO LA KALE”)

PANTATEKI (VITABU 5):

Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu, Kumbukumbu la Torati

Vitabu hivyo vinazungumuzia habari kuanzia uumbaji mupaka kuundwa kwa taifa la zamani la Israeli

VITABU VYA HISTORIA (VITABU 12):

Yoshua, Waamuzi, Rutu

Vitabu hivyo vinazungumuzia kuingia kwa taifa la Israeli katika Inchi ya Ahadi na mambo yenye yalitokea kisha wakati huo

1 na 2 Samweli, 1 na 2 Wafalme, 1 na 2 Mambo ya Nyakati

Vitabu hivyo vinazungumuzia historia ya taifa la Israeli mupaka uharibifu wa Yerusalemu

Ezra, Nehemia, Esta

Vitabu hivyo vinazungumuzia historia ya Wayahudi kisha kurudia kutoka katika Uhamisho kule Babiloni

VITABU VYA MASHAIRI (VITABU 5):

Yobu, Zaburi, Mezali, Muhubiri, Wimbo wa Sulemani

Vitabu hivyo ni mukusanyo wa nyimbo na semi mbalimbali za hekima

VITABU VYA UNABII (VITABU 17):

Isaya, Yeremia, Maombolezo, Ezekieli, Danieli, Hosea, Yoeli, Amosi, Obadia, Yona, Mika, Nahumu, Habakuki, Sefania, Hagai, Zekaria, Malaki

Vitabu hivyo viko na unabii mbalimbali, ao mambo yenye yalitabiriwa, kuhusu watu wa Mungu

MAANDIKO YA KIGIRIKI YA KIKRISTO (“AGANO JIPYA”)

INJILI INE (VITABU 4):

Matayo, Marko, Luka, Yohana

Vitabu hivyo vinazungumuzia maisha ya Yesu na utumishi wake

MATENDO YA MITUME (KITABU 1):

Kitabu hicho kinazungumuzia mwanzo wa kutaniko la Kikristo na kazi ya umisionere

BARUA (VITABU 21):

Waroma, 1 na 2 Wakorinto, Wagalatia, Waefeso,

Wafilipi, Wakolosai, 1 na 2 Watesalonike

Vitabu hivyo ni barua kwa makutaniko mbalimbali ya Kikristo

1 na 2 Timoteo, Tito, Filemoni

Vitabu hivyo ni barua kwa Wakristo mumoja-mumoja

Waebrania, Yakobo, 1 na 2 Petro,

1, 2, na 3 Yohana, Yuda

Vitabu hivyo ni barua zenye zilitumwa kwa Wakristo kwa ujumla

UFUNUO (KITABU 1):

Kitabu hicho kiko na maono yenye kufuatana ya unabii yenye mutume Yohana alipewa