Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 5

Biblia Iko na Ujumbe Gani?

“Nitatia uadui kati yako na ule mwanamuke na kati ya uzao wako na uzao wake. Ataponda kichwa chako, na wewe utamupiga kwenye kisigino.”

Mwanzo 3:15

“Kupitia uzao wako mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka kwa sababu umesikiliza sauti yangu.”

Mwanzo 22:18

“Ufalme wako ukuje. Mapenzi yako yafanyike duniani kama mbinguni.”

Matayo 6:10

“Kwa upande wake, Mungu mwenye anatoa amani atamuponda Shetani chini ya miguu yenu hivi karibuni.”

Waroma 16:20

“Wakati vitu vyote vitakuwa vimewekwa chini ya mamlaka yake, halafu Mwana mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Ule mwenye aliweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, ili Mungu akuwe vitu vyote kwa kila mutu.”

1 Wakorinto 15:28

“Sasa ahadi zilitolewa kwa Abrahamu na kwa uzao wake . . . , ambaye ni Kristo. Zaidi ya hayo, kama ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa Abrahamu.”

Wagalatia 3:16, 29

“Ufalme wa ulimwengu umekuwa Ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, na atatawala akiwa mufalme milele na milele.”

Ufunuo 11:15

“Basi ule nyoka mukubwa akatupwa chini, ule nyoka wa zamani, mwenye kuitwa Ibilisi na Shetani, mwenye anapotosha dunia yote yenye kuikaliwa na watu; akatupwa chini katika dunia, na malaika wake wakatupwa chini pamoja naye.”

Ufunuo 12:9

“Akamukamata ule nyoka mukubwa, ule nyoka wa ­zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na akamufunga kwa miaka elfu moja (1000).”

Ufunuo 20:2