Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 2

Namna gani Unaweza Kujifunza Juu ya Mungu?

“Kitabu hiki cha Sheria kisitoke katika kinywa chako, na unapaswa kukisoma kwa sauti ya chini muchana na usiku, ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yenye kuandikwa ndani; ukifanya vile, njia yako itakuwa na matokeo ya muzuri na utatenda kwa hekima.”

Yoshua 1:8

“Wakaendelea kusoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu, katika Sheria ya Mungu wa kweli, wakaifasiria waziwazi na kueleza maana yake; kwa hiyo wakasaidia watu kuelewa mambo yenye yalikuwa yanasomwa.”

Nehemia 8:8

“Mwenye furaha ni mutu mwenye hatembee kulingana na shauri la waovu . . . , lakini anapendezwa na sheria ya Yehova, na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini muchana na usiku. . . . Kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.”

Zaburi 1:1-3

“Filipo akakimbia pembeni-pembeni na akamusikia iko anasoma kwa sauti kubwa nabii Isaya, akamuuliza: ‘Je, kweli unajua mambo yenye unasoma?’ Akajibu: ‘Kwa kweli, ninaweza kujua namna gani kama mutu fulani haniongoze?’”

Matendo 8:30, 31

“Sifa zake zenye hazionekane zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaonekana kupitia vitu vyenye vilifanywa, ndiyo, nguvu zake za milele na Uungu, na hivyo hawana sababu ya kujitetea.”

Waroma 1:20

“Fikiri sana juu ya mambo hayo; zama katika mambo hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote.”

1 Timoteo 4:15

“Tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo ya muzuri, bila kuacha kukutana pamoja.”

Waebrania 10:24, 25

“Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila lawama, na atapewa hiyo.”

Yakobo 1:5