Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

B1

Ujumbe wa Biblia

Yehova Mungu iko na haki ya kutawala. Namna yake ya kutawala ndiyo ya muzuri zaidi. Kusudi lake kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya wanadamu litatimia.

Kisha 4026 M.K.Y.

“Nyoka” anatilia mashaka haki ya Mungu ya kutawala na namna yake ya kutawala. Yehova anaahidi kutokeza “uzao,” ao “mbegu,” wenye mwishowe utamuponda nyoka, ni kusema, Shetani. (Mwanzo 3:1-5, 15, maelezo ya chini) Lakini, Yehova anaachia wanadamu wakati ili wajitawale wakiongozwa na nyoka.

1943 M.K.Y.

Yehova anamuambia Abrahamu kwamba “uzao” wenye uliahidiwa utakuwa mumoja wa wazao wake.—Mwanzo 22:18.

Kisha 1070 M.K.Y.

Yehova anamuhakikishia Mufalme Daudi na kisha mwana wake Sulemani kwamba “uzao” wenye uliahidiwa ungetokea katika kizazi chao.—2 Samweli 7:12, 16; 1 Wafalme 9:3-5; Isaya 9:6, 7.

29 K.K.Y.

Yehova anamutambulisha Yesu kuwa “uzao” wenye uliahidiwa ambao ni Muriti wa kiti cha ufalme cha Daudi.—Wagalatia 3:16; Luka 1:31-33; 3:21, 22.

33 K.K.Y.

Nyoka, ni kusema Shetani, anaumiza kwa wakati mufupi “uzao” wenye uliahidiwa kwa kumufanya Yesu auawe. Yehova anamufufua Yesu kwenye uzima mbinguni na anakubali samani ya uzima mukamilifu wa Yesu, hilo linatoa musingi wa kusamehe zambi na kupatia wazao wa Adamu uzima wa milele.—Mwanzo 3:15; Matendo 2:32-36; 1 Wakorinto 15:21, 22.

Karibu 1914 K.K.Y.

Yesu anamutupa nyoka, ni kusema, Shetani, katika dunia, ­anamuzuia katika dunia kwa wakati mufupi.—Ufunuo 12:7-9, 12.

Wakati Wenye Kuja

Yesu anamutia Shetani katika kifungo kwa miaka elfu (1000) na ­kisha anamuharibu, kwa njia hiyo anamuponda kichwa kwa njia ya mufano. Kusudi la kwanza kabisa la Yehova kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya wanadamu linatimizwa, jina lake linaondolewa lawama, na namna yake ya kutawala inatetewa.—Ufunuo 20:1-3, 10; 21:3, 4.