Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

A1

Kanuni za Kutafsiri Biblia

Biblia iliandikwa kwanza katika luga za zamani, ni kusema, Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Leo inapatikana ikiwa nzima ao ikiwa sehemu katika luga karibu elfu tatu (3000). Watu wengi wenye wanasoma Biblia hawaelewe luga za kwanza na kwa hiyo wako na lazima ya tafsiri. Ni kanuni gani zenye zinapaswa kuongoza namna Biblia inatafsiriwa, na namna gani kanuni hizo zimefuatwa ili kutafsiri Biblia​Tafsiri ya Ulimwengu Mupya?

Watu fulani wanaweza kusema kama tafsiri yenye kuwa sawasawa kabisa, ya neno kwa neno, ya mutindo wa mustari kwa mustari inaweza kusaidia musomaji asome ujumbe wenye unakaribiana zaidi na mambo yenye yalisemwa katika luga za kwanza. Lakini, haiko vile kila wakati. Ona sababu fulani:

  • Hakuna luga mbili zenye kufanana kabisa katika sarufi, maneno, na mupangilio wa maneno katika musemwa. Profesa mumoja wa Kiebrania, S. R. Driver, aliandika kwamba luga “zinatofautiana hapana katika sarufi na maneno tu, lakini pia . . . katika namna mawazo yanaunganishwa ili kuunda musemwa.” Luga zenye kuwa tofauti zinaomba pia njia yenye kuwa tofauti kabisa ya kupanga mawazo. Profesa Driver anaongeza hivi: “Kwa hiyo, mipangilio ya musemwa katika luga mbalimbali haiko sawasawa.”

  • Hakuna luga yoyote ya sasa yenye iko kabisa-kabisa na maneno na sarufi kama za Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki cha Biblia; kwa hiyo tafsiri ya neno kwa neno ya Biblia haiwezi kuwa wazi ao wakati fulani inaweza hata kuleta maana yenye haiko ya kweli.

  • Maana ya neno ao usemi fulani inaweza kubadilika kwa kutegemea habari yenye kuzungumuziwa.

Mutafsiri anaweza kuwa na uwezo wa kutafsiri neno kwa neno luga ya kwanza katika maandiko fulani, lakini hilo linapaswa kufanywa kwa uangalifu sana.

Ona mifano fulani juu ya namna tafsiri ya neno kwa neno inaweza kueleweka mubaya:

  • Maandiko yanatumia maneno “kulala usingizi” ili kuzungumuzia usingizi wa kawaida na pia usingizi wa kifo. (Matayo 28:13; Matendo 7:60) Wakati maneno hayo yanatumiwa katika habari zenye kuzungumuzia kifo, watafsiri wa Biblia wanaweza kutumia maneno kama vile “kulala usingizi katika kifo,” yenye yanasaidia musomaji wa leo asielewe maneno hayo mubaya.​—1 Wakorinto 7:39; 1 Watesalonike 4:13; 2 Petro 3:4.

  • Mutume Paulo alitumia maneno yenye kupatikana katika Waefeso 4:14 yenye yanaweza kutafsiriwa neno kwa neno “katika kucheza dadu (jeu de dés) ya watu.” Maneno hayo ya mufano ya zamani yanaonyesha zoea la kudanganya wengine katika muchezo wa dadu. Katika luga nyingi, tafsiri ya neno kwa neno ya maneno hayo haina maana kabisa. Kutafsiri maneno hayo kuwa “udanganyifu wa watu” ni njia yenye kuwa wazi zaidi ya kutafsiri maana.

  • Kwenye Waroma 12:11, kunatumiwa maneno ya Kigiriki yenye neno kwa neno maana yake ni “kwa kutokota kwa roho.” Maneno hayo hayalete maana katika Swahili (Congo), kwa hiyo katika tafsiri hii yametafsiriwa “muwake roho.”

  • MATAYO 5:3

    Neno kwa neno katika Swahili (Congo): “maskini wa roho”

    Wazo: “wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho”

    Katika Mahubiri yake ya Mulimani yenye kujulikana sana, Yesu alitumia maneno yenye mara nyingi yanatafsiriwa “Heri walio maskini wa roho.” (Matayo 5:3, Union Version) Lakini katika luga nyingi tafsiri ya neno kwa neno ya maneno hayo haieleweke. Katika luga fulani, tafsiri ya sawasawa kabisa ya neno kwa neno inaweza hata kufanya mutu afikiri kwamba “maskini wa roho” ni watu wenye wanakosa usawaziko wa kiakili ao wenye wanakosa nguvu na azimio. Hata hivyo, katika andiko hili Yesu alikuwa anafundisha watu kama furaha yao ilitegemea kutambua kama wako na lazima ya muongozo wa Mungu lakini haikutegemea kutimiza mahitaji yao ya kimwili. (Luka 6:20) Kwa hiyo, tafsiri kama vile “wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho” ao “wale wenye wanajua kama wako na lazima ya Mungu” zinaonyesha maana ya kweli kabisa ya maneno hayo ya luga ya kwanza.​—Matayo 5:3.

  • Katika habari nyingi, neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “wivu” linalingana na maana yenye kujulikana ya neno la Swahili (Congo), ni kusema, kusikia kasirani juu ya wenye unaonekana kuwa ukosefu wa uaminifu wa rafiki wa karibu ao kusikilia wengine wivu kwa sababu ya mali yao. (Mezali 6:34; Isaya 11:13) Hata hivyo, neno lilelile la Kiebrania linaonyesha pia sifa za muzuri. Kwa mufano, linaweza kutumiwa ili kumaanisha “bidii,” ao juhudi ya kulinda, yenye Yehova anaonyesha kwa ajili ya watumishi wake ao kumaanisha kwamba ni “mwenye kutaka watu washikamane na yeye tu.” (Kutoka 34:14; 2 Wafalme 19:31; Ezekieli 5:13; Zekaria 8:2) Neno hilo linaweza pia kutumiwa ili kumaanisha “bidii” yenye watumishi wake waaminifu wako nayo kumuelekea Mungu na ibada yake ao kumaanisha kama ‘hawavumilie ushindani wowote’ kumuelekea.​—Zaburi 69:9; 119:139; Hesabu 25:11.

  • Neno la Kiebrania yadh mara nyingi linatafsiriwa “mukono,” lakini kwa kutegemea habari yenye kuzungumuziwa, neno hilo linaweza kutafsiriwa “mamlaka,” “ukarimu,” “nguvu,” na njia zingine nyingi

    Neno la Kiebrania lenye mara nyingi linazungumuzia mukono wa mwanadamu liko na maana nyingi mbalimbali. Kwa kutegemea habari yenye kuzungumuziwa, neno hilo linaweza kutafsiriwa “mamlaka,” “ukarimu,” ao “nguvu.” (2 Samweli 8:3; 1 Wafalme 10:13; Mezali 18:21) Kwa kweli, neno hilo linatafsiriwa katika njia nyingi zenye kutofautiana ao kuachana-achana katika toleo la Swahili (Congo) la Biblia​Tafsiri ya Ulimwengu Mupya.

Kwa kufikiria mambo hayo yote, kutafsiri Biblia haiko tu kutafsiri neno la luga ya kwanza kwa kulipatia neno lilelile kila wakati linapatikana. Mutafsiri anapaswa kutumia busara ao akili ili kuchagua maneno katika luga yake yenye yanatafsiri muzuri zaidi mawazo yenye kuwa katika maandishi ya luga ya kwanza. Zaidi ya hayo, ni lazima kupanga maneno ya misemwa katika njia yenye kupatana na kanuni za sarufi za luga ya mutafsiri, na hivyo kufanya maandishi yakuwe mwepesi kusomwa.

Wakati uleule, haifae kupita mipaka wakati wa kutumia maneno tofauti ili kueleza maana ya maandishi. Mutafsiri mwenye anajipatia uhuru wa kutafsiri Biblia kwa kueleza mambo kulingana na namna yeye anaelewa wazo la ujumla anaweza kupotosha maana ya maandishi. Namna gani? Mutafsiri anaweza kuingiza kimakosa mawazo yake juu ya mambo yenye maandishi ya luga ya kwanza yanamaanisha ao anaweza kukosa kutia maelezo ya maana yenye kupatikana katika maandishi ya luga ya kwanza. Kwa hiyo, hata kama tafsiri ya Biblia ya kueleza mambo inaweza kuwa mwepesi kusoma, uhuru mwingi wa mutafsiri wakati fulani unaweza kuzuia musomaji asielewe ujumbe wa kweli wa maandishi.

Maoni ya mutafsiri kuhusu mafundisho ya Biblia yanaweza pia kumufanya abadilishe kwa vyepesi maana katika tafsiri yake. Kwa mufano, Matayo 7:13 inasema: “Barabara yenye kuongoza kwenye uharibifu ni kubwa.” Watafsiri fulani, pengine kwa sababu ya maoni yao kuhusu mafundisho ya Biblia, wametumia maneno “moto wa mateso” kuliko kutumia neno lenye kuleta maana kabisa ya neno la Kigiriki, ni kusema, “uharibifu.”

Mutafsiri wa Biblia anapaswa pia kutambua kama Biblia iliandikwa kwa kutumia luga ya kawaida, yenye ilitumiwa kila siku na watu wa kawaida, kama vile walimaji, wachungaji, na wavuvi wa samaki. (Nehemia 8:8, 12; Matendo 4:13) Kwa hiyo, tafsiri ya muzuri ya Biblia inafanya ujumbe wenye kuwa ndani ueleweke na watu wanyoofu, hata wakuwe watu wa hali gani. Maneno yenye kuwa wazi, ya kawaida, na yenye kueleweka yanapendelewa zaidi kuliko maneno yenye watu wa kawaida hawazoee kutumia.

Watafsiri wengi wa Biblia wamejipatia uhuru wenye hauna musingi wa kuondoa jina la Mungu, Yehova, katika tafsiri za sasa hata kama jina hilo linapatikana katika maandishi ya zamani ya Biblia. (Angalia Nyongeza A4.) Mahali pa jina hilo, tafsiri nyingi zinaweka jina la cheo, kama vile “Bwana,” na zingine hata zinaficha ukweli wa kwamba Mungu iko na jina. Kwa mufano, katika tafsiri fulani, sala ya Yesu yenye kupatikana kwenye Yohana 17:26 inasomeka hivi: “Nimekufanya ujulikane kwao,” na kwenye Yohana 17:6, “Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa.” Hata hivyo, tafsiri ya uaminifu ya maneno ya Yesu inasomeka hivi: “Nimewajulisha jina lako,” na “Nimejulisha jina lako kwa watu wenye ulinipatia.”

Kama vile inaonyeshwa katika utangulizi wa Biblia ya kwanza ya Kiingereza ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya: “Hatutafsiri Maandiko kwa njia ya kueleza mambo. Tangu mwanzo tumejikaza kutafsiri neno kwa neno kadiri inawezekana, mahali kwenye Kiingereza cha sasa kinaruhusu na mahali kwenye tafsiri ya neno kwa neno haifiche ao kupotosha wazo kwa njia yoyote ile.” Kwa hiyo, Halmashauri ya Kutafsiri Biblia ya Ulimwengu Mupya imejikaza kuwa na usawaziko kati ya kutumia maneno na misemwa yenye kuonyesha maana ya maandishi ya kwanza na, wakati uleule, kuepuka maneno yenye kuwa magumu kusoma ao yenye kuficha wazo la kweli. Matokeo ni kwamba, Biblia inaweza kusomwa kwa vyepesi na musomaji anaweza kuwa na uhakika kabisa kama ujumbe wa Biblia wenye uliongozwa na roho ya Mungu umetafsiriwa kwa uaminifu.​—1 Watesalonike 2:13.