Mezali 12:1-28

  • Mwenye anachukia karipio hana akili (1)

  • “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga” (18)

  • Kuendeleza amani kunaleta furaha (20)

  • Midomo yenye kusema uongo inamuchukiza Yehova (22)

  • Mahangaiko yanalemea moyo (25)

12  Mwenye anapenda nizamu anapenda ujuzi,+Lakini mwenye anachukia karipio hana akili.*+   Mutu mwema anakubaliwa na Yehova,Lakini Yeye anamuhukumu mutu mwenye kufanya mipango ya uovu.+   Hakuna mutu mwenye anakuwa na usalama kwa kutenda uovu,+Lakini wenye haki hawatangolewa hata kidogo.   Bibi mwenye uwezo ni taji kwa bwana yake,+Lakini bibi mwenye kutenda mambo ya haya ni kama kuoza katika mifupa ya bwana yake.+   Mawazo ya wenye haki ni ya haki,Lakini muongozo wa waovu ni udanganyifu.   Maneno ya waovu yanavizia ili kuua,*+Lakini kinywa cha watu wanyoofu kinawaokoa.+   Wakati waovu wanapinduliwa, hawako tena,Lakini nyumba ya wenye haki itaendelea kusimama.+   Mutu anasifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+Lakini mutu mwenye kuwa na moyo wenye kupotoka atatendewa kwa zarau.+   Afazali usiheshimiwe sana lakini ukuwe na mutumishiKuliko kujitukuza mwenyewe na ukose chakula.*+ 10  Mwenye haki anatunza wanyama wake wa kufugwa,*+Lakini hata rehema ya waovu ni yenye ukali. 11  Mwenye analima shamba lake atakuwa na chakula kingi,+Lakini mwenye kufuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote hana akili ya muzuri.* 12  Mutu muovu anatamani kitu chenye kilikamatwa na watu wengine waovu,Lakini muzizi wa wenye haki unazaa matunda. 13  Mutu muovu ananaswa na mazungumuzo yake ya zambi,+Lakini mwenye haki anaponyoka katika taabu. 14  Mutu anashiba mema kutokana na matunda ya maneno yake,*+Na kazi ya mikono yake itamupatia zawabu. 15  Njia ya mupumbavu iko sawa mbele ya macho yake mwenyewe,+Lakini mwenye hekima anakubali shauri.+ 16  Mupumbavu anaonyesha pale pale* kwamba ameuzika,+Lakini mutu mwerevu anapuuza* matusi. 17  Mwenye anatoa ushuhuda kwa uaminifu atasema kweli,*Lakini shahidi wa uongo anasema mambo ya udanganyifu. 18  Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga,Lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.+ 19  Midomo yenye kusema kweli itadumu milele,+Lakini ulimi wenye kusema uongo utadumu wakati kidogo tu.+ 20  Udanganyifu uko katika moyo wa wale wenye kufanya mipango mibaya,Lakini wale wenye kuendeleza* amani wako na furaha.+ 21  Hakuna mambo yenye kuumiza yenye yatamupata mwenye haki,+Lakini waovu watapatwa na misiba mingi.+ 22  Midomo yenye kusema uongo ni chukizo kwa Yehova,+Lakini wale wenye kutenda kwa uaminifu wanamufurahisha. 23  Mutu mwerevu anaficha mambo yenye anajua,Lakini moyo wa mupumbavu unasema-sema mambo ya upumbavu.+ 24  Mukono wa wenye bidii utatawala,+Lakini mikono yenye uvivu itafanyishwa kazi ya kulazimishwa.+ 25  Mahangaiko katika moyo wa mutu yanalemea moyo,*+Lakini neno la muzuri linauchangamusha.+ 26  Mwenye haki anatafuta malisho yake,Lakini njia ya waovu inawapoteza. 27  Wavivu hawafuatilie mawindo,+Lakini bidii ni hazina yenye samani ya mutu. 28  Njia ya haki inaongoza kwenye uzima;+Hakuna kifo katika njia hiyo.

Maelezo ya Chini

Ao “hana ufahamu.”
Tnn., “yanavizia ili kumwanga damu.”
Tnn., “mukate.”
Ao “nafsi ya munyama wake wa kufugwa.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “kinywa chake.”
Ao “siku ileile.”
Tnn., “anafunika.”
Tnn., “mambo yenye haki.”
Tnn., “Lakini washauri wa.”
Ao “yanamufanya ashuke moyo.”