Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 17

Namna gani Biblia Inaweza Kusaidia Familia Yako?

BWANA/BABA

“Kwa njia ileile, bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe. Mwanaume mwenye anamupenda bibi yake anajipenda yeye mwenyewe, kwa maana hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake; lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo . . . Kila mumoja wenu anapaswa kumupenda bibi yake kama vile anajipenda mwenyewe.”

Waefeso 5:28, 29, 33

“Ninyi baba, musikuwe munakasirisha watoto wenu, lakini muendelee kuwalea katika nizamu na maonyo ya Yehova.”

Waefeso 6:4

BIBI

“Bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.”

Waefeso 5:33

“Ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu, kwa kuwa inafaa katika Bwana.”

Wakolosai 3:18

WATOTO

“Watoto, mutii wazazi wenu katika umoja na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la haki. ‘Heshimia baba yako na mama yako,’ hiyo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi: ‘Ili mambo yakuendee muzuri na ukae wakati murefu katika dunia.’”

Waefeso 6:1-3

“Ninyi watoto, mutii wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo linamupendeza Bwana.”

Wakolosai 3:20