Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 10

Biblia Inaahidi Nini Kuhusu Wakati Wenye Kuja?

“Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”

Zaburi 37:29

“Dunia inadumu milele.”

Muhubiri 1:4

“Atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapanguza machozi kwenye nyuso zote.”

Isaya 25:8

“Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatafunguliwa. Wakati huo kilema wa miguu ataruka-ruka kama paa, na ulimi wa bubu utapiga vigelegele vya shangwe. Kwa maana maji yatabubujika katika jangwa, na mito midogo katika jangwa tambarare.”

Isaya 35:5, 6

“Atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita kabisa.”

Ufunuo 21:4

“Watajenga nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani, wala hawatapanda ili wengine wakule. Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za muti, na wachaguliwa wangu watafurahia kwa ukamili kazi ya mikono yao.”

Isaya 65:21, 22