Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

ULIZO LA 16

Namna Gani Unaweza Kupiganisha Mahangaiko?

“Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.”

Zaburi 55:22

“Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio, lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.”

Mezali 21:5

“Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe. Usihangaike, kwa maana niko Mungu wako. Nitakutia nguvu, ndiyo, nitakusaidia, nitakushika kwelikweli kwa mukono wangu wa kuume wa haki.”

Isaya 41:10

“Ni nani kati yenu mwenye kwa kuhangaika anaweza kuongeza kipimo cha mukono mumoja kwenye urefu wa uzima wake?”

Matayo 6:27

“Basi, musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku iko na matatizo yake yenye yanaeneana na siku hiyo.”

Matayo 6:34

“Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”

Wafilipi 1:10

“Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu pamoja na kutoa shukrani, maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.”

Wafilipi 4:6, 7