Kulingana na Yohana 8:12-59

  • Baba anatoa ushahidi juu ya Yesu (12-30)

    • Yesu ni “mwangaza wa ulimwengu” (12)

  • Watoto wa Abrahamu (31-41)

    • “Kweli itawaweka ninyi huru” (32)

  • Watoto wa Ibilisi (42-47)

  • Yesu na Abrahamu (48-59)

8  12  Kisha Yesu akawaambia tena, akisema: “Mimi ndiye mwangaza wa ulimwengu.+ Kila mutu mwenye ananifuata hatatembea hata kidogo katika giza, lakini atakuwa na mwangaza+ wa uzima.” 13  Basi Wafarisayo wakamuambia: “Wewe unatoa ushahidi juu yako mwenyewe; ushahidi wako hauko wa kweli.” 14  Yesu akawajibu: “Hata kama ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, ushahidi wangu ni wa kweli, kwa sababu ninajua kwenye nilitoka na kwenye ninaenda.+ Lakini ninyi hamujue kwenye nilitoka na kwenye ninaenda. 15  Ninyi munahukumu kulingana na mwili;*+ mimi simuhukumu mutu yeyote hata kidogo. 16  Na bado hata kama ninahukumu, hukumu yangu ni ya kweli, kwa sababu siko peke yangu, lakini Baba mwenye alinituma iko* pamoja na mimi.+ 17  Pia, imeandikwa katika Sheria yenu wenyewe, ‘Ushahidi wa watu wawili ni wa kweli.’+ 18  Mimi ninatoa ushahidi juu yangu mwenyewe, na Baba mwenye alinituma anatoa ushahidi juu yangu.”+ 19  Kisha wakamuuliza: “Baba yako iko* wapi?” Yesu akajibu: “Ninyi hamunijue na hamumujue Baba yangu.+ Kama mungenijua, mungemujua Baba yangu pia.”+ 20  Alisema maneno hayo katika chumba cha hazina+ wakati alikuwa anafundisha katika hekalu. Lakini hakuna mwenye alimukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika.+ 21  Kwa hiyo, akawaambia tena: “Ninaenda, na ninyi mutanitafuta, na bado mutakufa katika zambi yenu.+ Kwenye ninaenda hamuwezi kuja.”+ 22  Basi Wayahudi wakaanza kusema: “Je, atajiua? Kwa sababu anasema, ‘Kwenye ninaenda, hamuwezi kuja.’” 23  Akaendelea kuwaambia: “Ninyi munatoka katika makao ya chini; mimi ninatoka katika makao ya juu.+ Ninyi munatoka katika ulimwengu huu; mimi sitoke katika ulimwengu huu. 24  Ndiyo sababu niliwaambia ninyi: Mutakufa katika zambi zenu. Kwa maana kama hamuamini kwamba mimi ndiye, mutakufa katika zambi zenu.” 25  Basi wakaanza kumuuliza: “Wewe ni nani?” Yesu akawajibu: “Sababu gani hata ninasema na ninyi? 26  Niko na mambo mengi ya kusema juu yenu na kutoa hukumu juu ya mambo hayo. Kwa hakika, Ule mwenye alinituma ni wa kweli, na mambo yenye nilisikia kutoka kwake ninayasema katika ulimwengu.”+ 27  Hawakuelewa kwamba alikuwa anawaambia juu ya Baba. 28  Kisha Yesu akasema: “Wakati mutakuwa mumeinua Mwana wa binadamu,+ ndipo mutajua kwamba mimi ndiye,+ na kwamba sifanye jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe;+ lakini kama vile Baba alinifundisha, ni vile ninasema mambo haya. 29  Na Ule mwenye alinituma iko* pamoja na mimi; hakuniacha peke yangu, kwa sababu sikuzote ninafanya mambo yenye kumupendeza.”+ 30  Wakati alikuwa anasema mambo hayo, wengi wakamuamini. 31  Kisha Yesu akaendelea kuambia Wayahudi wenye walikuwa wamemuamini: “Kama munakaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu, 32  na mutajua kweli,+ na kweli itawaweka ninyi huru.”+ 33  Wakamujibu: “Sisi ni uzao wa Abrahamu na hatujakuwa watumwa wa mutu yeyote hata siku moja. Namna gani unasema, ‘Mutakuwa huru’?” 34  Yesu akawajibu: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye anazoea kutenda zambi ni mutumwa wa zam­bi.+ 35  Zaidi ya hayo, mutumwa hakae katika nyumba milele; mwana anakaa milele. 36  Kwa hiyo, kama Mwana anawaweka ninyi huru, mutakuwa huru kwelikweli. 37  Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu neno langu halifanye maendeleo katikati yenu. 38  Ninasema mambo yenye niliona wakati nilikuwa pamoja na Baba yangu,+ lakini ninyi munafanya mambo yenye mulisikia kutoka kwa baba yenu.” 39  Wakamujibu: “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia: “Ninyi mungekuwa watoto wa Abrahamu,+ mungekuwa munafanya kazi za Abrahamu. 40  Lakini sasa munatafuta kuniua, mimi mwenye nimewaambia kweli yenye nilisikia kutoka kwa Mungu.+ Abrahamu hakufanya vile. 41  Ninyi munafanya kazi za baba yenu.” Wakamuambia: “Hatukuzaliwa katika uasherati;* tuko na Baba mumoja, Mungu.” 42  Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda,+ kwa maana nilitoka kwa Mungu na niko hapa. Sikukuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, lakini Yeye ndiye alinituma.+ 43  Sababu gani hamuelewe mambo yenye ninasema? Kwa sababu hamuwezi kusikiliza neno langu. 44  Ninyi mumetoka kwa baba yenu Ibilisi, na munataka kufanya tamaa za baba yenu.+ Huyo alikuwa muuaji wakati alianza,*+ na hakusimama imara katika kweli, kwa sababu kweli haiko ndani yake. Wakati anasema uongo, anasema kulingana na muelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni muongo na baba ya uongo.+ 45  Lakini mimi, kwa sababu ninawaambia kweli, hamuniamini. 46  Ni nani katikati yenu mwenye anaweza kuhakikisha kwamba niko na zambi? Kama ninasema kweli, sababu gani hamuniamini? 47  Ule mwenye anatoka kwa Mungu anasikiliza maneno ya Mungu.+ Ndiyo sababu hamusikilize, kwa sababu hamutoke kwa Mungu.”+ 48  Wayahudi wakamuambia: “Je, hatuseme kweli wakati tunasema, ‘Wewe ni Musamaria+ na uko na pepo muchafu’?”+ 49  Yesu akajibu: “Mimi sina pepo muchafu, lakini ninamuheshimia Baba yangu, na ninyi munanivunjia heshima. 50  Lakini mimi sijitafutie utukufu;+ kuko Ule mwenye anatafuta utukufu huo na ni yeye anahukumu. 51  Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kama mutu yeyote anashika neno langu, hataona kifo hata siku moja.”+ 52  Wayahudi wakamuambia: “Sasa tunajua uko na pepo muchafu. Abrahamu alikufa, na manabii vilevile, lakini wewe unasema, ‘Kama mutu yeyote anashika neno langu, hataonja kifo hata siku moja.’ 53  Je, wewe ni mukubwa kuliko Abrahamu baba yetu, mwenye alikufa? Manabii pia walikufa. Unajiona kuwa nani?” 54  Yesu akajibu: “Kama ninajitukuza mimi mwenyewe, utukufu wangu hauko kitu. Baba yangu ndiye ananitukuza,+ ule mwenye munasema ni Mungu wenu. 55  Na bado ninyi hamujamujua,+ lakini mimi ninamujua.+ Na kama ningesema simujue, ningekuwa muongo, kama ninyi. Lakini mimi ninamujua na ninashika neno lake. 56  Baba yenu Abrahamu alifurahi sana katika tumaini la kuona siku yangu, na aliiona na kufurahi.”+ 57  Kisha Wayahudi wakamuambia: “Wewe haujakuwa hata na miaka makumi tano (50), na je, umekwisha kumuona Abrahamu?” 58  Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mbele Abrahamu azaliwe, mimi nilikuwa.”+ 59  Basi wakaokota majiwe ili wamutupie, lakini Yesu akajificha na akatoka katika hekalu.

Maelezo ya Chini

Ao “kulingana na kanuni za wanadamu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Neno la Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “tangu mwanzo.”