Kulingana na Yohana 17:1-26

  • Sala ya mwisho ya Yesu pamoja na mitume wake (1-26)

    • Kufikia kumujua Mungu kunaongoza kwenye uzima wa milele (3)

    • Wakristo hawako sehemu ya ulimwengu (14-16)

    • “Neno lako ni kweli” (17)

    • ‘Nimejulisha jina lako’ (26)

17  Yesu alisema mambo haya, na akainua macho yake kuelekea mbinguni, na kusema: “Baba, saa imekuja. Tukuza mwana wako ili mwana wako akutukuze,+  kwa kuwa ulimupatia mamlaka juu ya miili yote,*+ ili apatie uzima wa milele+ wale wote wenye umemupatia.+  Uzima wa milele ndio huu,+ wafikie kukujua* wewe Mungu wa pekee wa kweli,+ na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.+  Nimekutukuza katika dunia,+ kwa kuwa nimemaliza kazi yenye ulinipatia nifanye.+  Basi sasa, Baba, unitukuze pembeni yako kwa utukufu wenye nilikuwa nao pembeni yako mbele ya ulimwengu kuwa.+  “Nimejulisha jina lako kwa watu wenye ulinipatia kutoka katika ulimwengu.+ Walikuwa wako, na ukanipatia, na wameshika* neno lako.  Sasa wamejua kwamba mambo yote yenye ulinipatia yametoka kwako;  kwa sababu nimewapatia maneno yenye ulinipatia,+ na wameyakubali na wamejua kabisa kwamba nilikuja nikiwa mwakilishi wako,+ na wameamini kwamba ulinituma.+  Ninaomba kwa ajili yao; siombe kwa ajili ya ulimwengu, lakini ninaomba kwa ajili ya wale wenye wewe ulinipatia, kwa sababu ni wako; 10  na vitu vyangu vyote ni vyako na vyako ni vyangu,+ na nimetukuzwa kati yao. 11  “Mimi siko tena katika ulimwengu, lakini wao wako katika ulimwengu,+ na ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde+ kwa sababu ya jina lako lenye umenipatia, ili wakuwe kitu kimoja* kama vile sisi tuko kitu kimoja.*+ 12  Wakati nilikuwa pamoja nao nilikuwa ninawalinda+ kwa sababu ya jina lako, lenye umenipatia; na nimewalinda, na hakuna hata mumoja wao mwenye aliharibiwa+ isipokuwa ule mwana wa uharibifu,+ ili andiko litimizwe.+ 13  Lakini sasa ninakuja kwako, na ninasema mambo haya katika ulimwengu ili furaha yangu ikuwe kamili ndani yao.+ 14  Nimewapatia neno lako, lakini ulimwengu umewachukia, kwa sababu hawako sehemu ya ulimwengu,+ kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu. 15  “Siombe kwamba uwatoshe katika ulimwengu, lakini ninaomba kwamba uwalinde kwa sababu ya ule muovu.+ 16  Wao hawako sehemu ya ulimwengu,+ kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.+ 17  Uwatakase* kwa njia ya ile kweli;+ neno lako ni kweli.+ 18  Kama vile ulinituma katika ulimwengu, mimi pia nimewatuma katika ulimwengu.+ 19  Na ninajitakasa kwa ajili yao, ili wao pia watakaswe kwa njia ya ile kweli. 20  “Siombe kwa ajili ya hawa tu, lakini ninaomba pia kwa ajili ya wale wenye wananiamini kupitia neno lao, 21  ili wote wakuwe kitu kimoja,+ kama vile wewe, Baba, uko katika umoja na mimi na mimi niko katika umoja na wewe,+ wao pia wakuwe katika umoja na sisi, ili ulimwengu uamini kwamba wewe ulinituma. 22  Nimewapatia utukufu wenye ulinipatia, ili wakuwe kitu kimoja kama vile sisi tuko kitu kimoja.+ 23  Mimi katika umoja nao na wewe katika umoja na mimi, ili wakamilishwe katika umoja,* ili ulimwengu ujue kwamba ulinituma na kwamba uliwapenda kama vile ulinipenda mimi. 24  Baba, ninataka wale wenye umenipatia wakuwe pamoja na mimi kwenye niko,+ ili waone utukufu wangu wenye umenipatia, kwa sababu ulinipenda mbele ya kuwekwa kwa musingi wa ulimwengu.+ 25  Baba mwenye haki, kwa kweli, ulimwengu haujakujua wewe,+ lakini mimi ninakujua,+ na hawa wamejua kwamba ­ulinituma. 26  Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha,+ ili upendo wenye ulinipenda ukuwe ndani yao na mimi nikuwe katika umoja nao.”+

Maelezo ya Chini

Ao “wanadamu; watu.”
Ao “waendelee kupata ujuzi juu yako.”
Ao “wametii.”
Ao “katika umoja.”
Ao “katika umoja.”
Ao “Uwaweke pembeni; Uwafanye kuwa watakatifu.”
Ao “waunganishwe kikamili.”