Kulingana na Yohana 15:1-27

  • Mufano wa muzabibu wa kweli (1-10)

  • Amri ya kuonyesha upendo kama wa Kristo (11-17)

    • ‘Hakuna upendo mukubwa kuliko huu’ (13)

  • Ulimwengu unachukia wanafunzi wa Yesu (18-27)

15  “Mimi ndiye muzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mulimaji.  Anatosha ndani yangu kila tawi lenye halizae matunda, na anasafisha kila tawi lenye linazaa matunda, ili lizae matunda zaidi.+  Ninyi mumekwisha kuwa safi kwa sababu ya neno lenye nimewaambia.+  Mukae katika umoja na mimi, na mimi nitakaa katika umoja na ninyi. Kama vile tawi likiwa peke yake haliwezi kuzaa matunda ikiwa halikae kwenye muzabibu, vilevile ninyi hamuwezi kuzaa matunda ikiwa hamukae katika umoja na mimi.+  Mimi ndiye muzabibu; na ninyi ndio matawi. Kila mutu mwenye anakaa katika umoja na mimi, na mimi katika umoja naye, huyo anazaa matunda mengi;+ kwa maana bila mimi hamuwezi kufanya jambo lolote hata kidogo.  Kama mutu yeyote hakae katika umoja na mimi, anatupwa inje kama tawi na anakauka. Na watu wanakusanya matawi hayo na kuyatupa ndani ya moto, na yanaungua.  Kama munakaa katika umoja na mimi, na maneno yangu yanakaa ndani yenu, muombe kila kitu chenye munataka na kitatendeka kwenu.+  Baba yangu anatukuzwa katika hili, kwamba muendelee kuzaa matunda mengi na kujionyesha kuwa wanafunzi wangu.+  Kama vile Baba alinipenda mimi,+ ni vile niliwapenda ninyi; mubaki katika upendo wangu. 10  Kama munashika amri zangu, mutabakia katika upendo wangu, kama vile mimi nilishika amri za Baba na ninabakia katika upendo wake. 11  “Nimewaambia ninyi mambo haya, ili furaha yangu ikuwe ndani yenu na furaha yenu ijae.+ 12  Hii ndiyo amri yangu, kwamba mupendane kama vile niliwapenda ninyi.+ 13  Hakuna mwenye iko* na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake* kwa ajili ya marafiki wake.+ 14  Ninyi ni marafiki wangu kama munafanya mambo yenye ninawaamuru.+ 15  Siwaite ninyi tena watumwa, kwa sababu mutumwa hajue mambo yenye bwana wake anafanya. Lakini nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu nimewajulisha mambo yote yenye nilisikia kutoka kwa Baba yangu. 16  Ninyi hamukunichagua, lakini mimi niliwachagua, na niliwaweka ili muende na muendelee kuzaa matunda na kwamba matunda yenu yaendelee kubakia, ili jambo lolote lenye munamuomba Baba katika jina langu, awapatie ninyi jambo hilo.+ 17  “Mambo haya ninawaamuru ninyi, kwamba mupendane.+ 18  Kama ulimwengu unawachukia ninyi, munajua kwamba umenichukia mimi mbele ya kuwachukia ninyi.+ 19  Kama mungekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kitu chake. Sasa kwa sababu ninyi hamuko sehemu ya ulimwengu,+ lakini nimewachagua ninyi kutoka katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.+ 20  Muweke katika akili neno lenye niliwaambia ninyi: Mutumwa haiko mukubwa kuliko bwana wake. Kama wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia;+ kama wameshika neno langu, watashika lenu pia. 21  Lakini watawatendea ninyi mambo yote haya kwa sababu ya jina langu, kwa kuwa hawajue Ule mwenye alinituma.+ 22  Kama singekuja na kusema nao, hawangekuwa na zambi.+ Lakini sasa hawana sababu ya kujitetea kwa ajili ya zambi yao.+ 23  Kila mutu mwenye ananichukia mimi, anamuchukia Baba yangu pia.+ 24  Kama singefanya kati yao kazi zenye hakuna mutu mwingine mwenye alizifanya, hawangekuwa na zambi;+ lakini sasa wameniona mimi na wamenichukia na wamemutendea Baba yangu vilevile. 25  Lakini jambo hilo lilifanyika ili kutimiza neno lenye liliandikwa katika Sheria yao: ‘Walinichukia bila sababu.’+ 26  Wakati musaidizi atakuja mwenye nitawatumia ninyi kutoka kwa Baba, roho ya ile kweli+ yenye inakuja kutoka kwa Baba, huyo atatoa ushahidi juu yangu;+ 27  na ninyi, kwa upande wenu, mutatoa ushahidi,+ kwa sababu mumekuwa pamoja na mimi tangu mwanzo.

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “nafsi yake.”