Kulingana na Yohana 6:1-71

  • Yesu anakulisha watu elfu tano (1-15)

  • Yesu anatembea juu ya maji (16-21)

  • Yesu ni “mukate wa uzima” (22-59)

  • Wengi wanakwazwa na maneno ya Yesu (60-71)

6  Kisha mambo hayo Yesu akatoka na kuvuka Bahari ya Galilaya, ao Tiberia.+  Na watu wengi sana waliendelea kumufuata,+ kwa sababu walikuwa wanaona miujiza yenye alikuwa anafanya kwa kuponyesha wagonjwa.+  Basi Yesu akapanda kwenye mulima na kukaa kule pamoja na wanafunzi wake.  Sasa Pasaka,+ ile sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu.  Wakati Yesu aliinua macho yake na kuona kwamba watu wengi sana walikuwa wanakuja kwenye alikuwa, akamuuliza Filipo: “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wakule?”+  Lakini, alikuwa anasema vile ili kumujaribu, kwa maana alijua jambo lenye alikuwa karibu kufanya.  Filipo akamujibu: “Mikate ya dinari* mia mbili (200) haitaenea ili kila mumoja wao apate hata sehemu kidogo.”  Mumoja wa wanafunzi wake mwenye kuitwa Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamuambia:  “Hapa kuko kijana mwanaume mwenye iko* na mikate tano (5) ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini vitu hivi ni nini kwa watu hawa wengi?”+ 10  Yesu akasema: “Muambie watu wakae.” Kwa kuwa mahali pale kulikuwa majani mengi, wanaume wakakaa, walikuwa karibu elfu tano (5000).+ 11  Yesu akakamata ile mikate, na kisha kutoa shukrani, akaigawia wale wenye walikuwa wamekaa pale; akafanya vilevile kuhusu wale samaki wadogo, na wakapata kadiri walitaka. 12  Lakini wakati walikuwa wamekula na kushiba, akaambia wanafunzi wake: “Mukusanye pamoja vipande vyenye vilibakia, ili kitu chochote kisipotee.” 13  Basi wakavikusanya pamoja na kujaza vitunga kumi na mbili (12) vya vipande vyenye wale wenye walikula ile mikate tano (5) ya shairi waliacha. 14  Wakati watu waliona alama yenye alifanya, wakaanza kusema: “Kwa kweli huyu ndiye Nabii mwenye alipaswa kuja katika ulimwengu.”+ 15  Kisha Yesu, kwa sababu alijua kama walikuwa karibu kuja kumukamata ili wamufanye kuwa mufalme, akaondoka+ tena na kuenda kwenye mulima peke yake.+ 16  Wakati ilikuwa mangaribi, wanafunzi wake wakashuka kuenda kwenye bahari,+ 17  na wakapanda katika mashua,* wakaondoka na kuvuka bahari ili kuenda Kapernaumu. Sasa giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajafika kwenye walikuwa.+ 18  Pia, bahari ilikuwa inachafuka kwa sababu upepo mukali ulikuwa unavuma.+ 19  Lakini, wakati walikuwa wamepiga makasia* karibu kilometre tano (5) ao sita (6),* wakamuona Yesu akitembea juu ya bahari na alikuwa anakaribia mashua,* na wakaogopa. 20  Lakini akawaambia: “Ni mimi; musiogope!”+ 21  Basi walitaka kumubeba Yesu katika mashua,* na mara moja mashua ikafika kwenye inchi kavu mahali walikuwa wanaenda.+ 22  Siku yenye ilifuata watu wengi wenye walikuwa wamebakia ngambo ingine ya bahari waliona kwamba pale hapakukuwa mashua* ingine isipokuwa mashua moja tu ya kidogo, na kwamba Yesu hakukuwa ameingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, lakini wanafunzi wake walikuwa wameondoka peke yao. 23  Lakini, mashua* kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali kwenye walikulia mikate kisha Bwana kutoa shukrani. 24  Basi wakati wale watu wengi waliona kwamba Yesu hakukuwa pale wala wanafunzi wake, wakapanda katika mashua* zao na wakakuja Kapernaumu ili kumutafuta Yesu. 25  Wakati walimupata ngambo ingine ya bahari wakamuuliza: “Rabi,+ ulifika hapa wakati gani?” 26  Yesu akawajibu: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, hamunitafute kwa sababu muliona alama, lakini kwa sababu mulikula mikate na mukashiba.+ 27  Musifanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinaharibikaka, lakini mufanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele,+ chenye Mwana wa binadamu atawapatia; kwa maana Baba, Mungu mwenyewe, amemutia muhuri wake wa kumukubali.”+ 28  Basi wakamuuliza: “Tufanye nini ili tutimize kazi za Mungu?” 29  Yesu akawajibu: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba ninyi muamini ule mwenye huyo alimutuma.”+ 30  Basi wakamuambia: “Unafanya alama gani,+ ili tuione na tukuamini? Ni kazi gani yenye unafanya? 31  Mababu zetu walikula mana katika jangwa,+ kama vile imeandikwa: ‘Aliwapatia mukate kutoka mbinguni ili wakule.’”+ 32  Kisha Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Musa hakuwapatia ninyi mukate kutoka mbinguni, lakini Baba yangu anawapatia ninyi mukate wa kweli kutoka mbinguni. 33  Kwa maana mukate wa Mungu ni ule mwenye anashuka kutoka mbinguni na anapatia ulimwengu uzima.” 34  Basi wakamuambia: “Bwana, tupatie mukate huo sikuzote.” 35  Yesu akawaambia: “Mimi ndio mukate wa uzima. Kila mutu mwenye ananifuata hatasikia njaa hata kidogo, na kila mutu mwenye ananiamini hatasikia kiu hata kidogo.+ 36  Lakini kama vile niliwaambia ninyi, hata kama mumeniona lakini bado hamuamini.+ 37  Wale wote wenye Baba ananipatia watakuja kwangu, na mimi sitamufukuza hata siku moja ule mwenye anakuja kwangu;+ 38  kwa maana sikushuka kutoka mbinguni+ ili kufanya mapenzi yangu, lakini ili kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma.+ 39  Haya ndiyo mapenzi ya ule mwenye alinituma, kwamba nisipoteze hata mumoja kati ya wote wenye amenipatia, lakini niwafufue+ katika siku ya mwisho. 40  Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mutu mwenye anakubali Mwana na kumuamini akuwe na uzima wa milele,+ na mimi nitamufufua+ katika siku ya mwisho.” 41  Kisha Wayahudi wakaanza kumunungunikia kwa sababu alisema: “Mimi ndio mukate wenye ulishuka kutoka mbinguni.”+ 42  Na wakaanza kusema: “Je, huyu haiko Yesu mwana wa Yosefu, mwenye tunajua baba yake na mama yake?+ Sasa namna gani anasema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?” 43  Yesu akawajibu: “Muache kunungunika kati yenu wenyewe. 44  Hakuna mutu mwenye anaweza kuja kwangu isipokuwa Baba mwenye alinituma amuvute,+ na mimi nitamufufua katika siku ya mwisho.+ 45  Imeandikwa katika Manabii: ‘Wote watafundishwa na Yehova.’*+ Kila mutu mwenye amesikiliza Baba na amejifunza, anakuja kwangu. 46  Haiko kwamba kuko mwanadamu yeyote mwenye amekwisha kumuona Baba,+ isipokuwa ule mwenye alitoka kwa Mungu; huyo amemuona Baba.+ 47  Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye anaamini iko* na uzima wa milele.+ 48  “Mimi ndio mukate wa uzima.+ 49  Mababu zenu walikula mana katika jangwa lakini walikufa.+ 50  Huu ndio mukate wenye unashuka kutoka mbinguni, ili mutu yeyote apate kuukula na asikufe. 51  Mimi ni mukate wa uzima wenye ulishuka kutoka mbinguni. Kama mutu yeyote anakula mukate huu ataishi milele; na kwa kweli, mukate wenye nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”+ 52  Kisha Wayahudi wakaanza kubishana kati yao, na kusema: “Namna gani mutu huyu anaweza kutupatia mwili wake tuukule?” 53  Basi Yesu akawaambia: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kama hamukule mwili wa Mwana wa binadamu na kunywa damu yake, hamuna uzima ndani yenu wenyewe.+ 54  Kila mutu mwenye anakula mwili wangu na kunywa damu yangu iko* na uzima wa milele, na mimi nitamufufua+ katika siku ya mwisho; 55  kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 56  Kila mutu mwenye anakula mwili wangu na kunywa damu yangu anabakia katika umoja na mimi, na mimi katika umoja naye.+ 57  Kama vile Baba mwenye kuishi alinituma na mimi ninaishi kwa sababu ya Baba, vilevile ule mwenye ananikula mimi ataishi kwa sababu yangu.+ 58  Huu ndio mukate wenye ulishuka kutoka mbinguni. Haiko kama vile wakati mababu zenu walikula lakini wakakufa. Kila mutu mwenye anakula mukate huu ataishi milele.”+ 59  Alisema mambo haya wakati alikuwa anafundisha katika sinagogi moja* kule Kapernaumu. 60  Wakati walisikia mambo hayo, wengi kati ya wanafunzi wake wakasema: “Maneno hayo ni yenye kuchukiza; ni nani mwenye anaweza kuyasikiliza?” 61  Lakini Yesu, kwa kuwa alitambua ndani yake mwenyewe kwamba wanafunzi wake walikuwa wananungunika juu ya jambo hilo, akawaambia: “Je, jambo hili limewakwaza? 62  Basi, itakuwa namna gani, kama munamuona Mwana wa binadamu anapanda ili kurudia kwenye alikuwa hapo mbele?+ 63  Roho ndiyo inatoa uzima;+ mwili hauna faida hata kidogo. Maneno yenye nimewaambia ni roho na ni uzima.+ 64  Lakini kuko wamoja kati yenu wenye hawaamini.” Kwa maana tangu mwanzo Yesu alijua wale wenye hawakuamini na ule mwenye angemusaliti.+ 65  Akaendelea kusema: “Ndiyo sababu nimewaambia ninyi, hakuna mutu mwenye anaweza kuja kwangu isipokuwa Baba amuruhusu.”+ 66  Kwa sababu ya jambo hili, wengi kati ya wanafunzi wake wakaenda kwenye mambo yenye yalikuwa nyuma+ na hawakutembea tena pamoja naye. 67  Basi Yesu akauliza wale Kumi na Mbili (12): “Ninyi pia munataka kuenda?” 68  Simoni Petro akamujibu: “Bwana, tutaenda kwa nani?+ Wewe uko na maneno ya uzima wa milele.+ 69  Tumeamini na tumejua kwamba wewe ndiye Mutakatifu wa Mungu.”+ 70  Yesu akawajibu: “Niliwachagua ninyi kumi na mbili (12), haiko vile?+ Lakini mumoja wenu ni muchongezi.”*+ 71  Kwa kweli, alikuwa anasema juu ya Yuda mwana wa Simoni Iskariote, kwa maana huyo ndiye angemusaliti, hata kama alikuwa mumoja wa wale Kumi na Mbili (12).+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Kasia ni chombo chenye kufanana na mwiko chenye kinatumiwa kuendesha mashua.
Karibu maili 3 ao 4. Tnn., “stadia karibu 25 ao 30.” Angalia Nyongeza B14.
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “mukusanyiko mumoja wa watu wote.”
Ao “ibilisi.”