Kulingana na Matayo 5:1-48

  • MAHUBIRI KWENYE MULIMA (1-48)

    • Yesu anaanza kufundisha kwenye mulima (1, 2)

    • Mambo kenda yenye kuleta furaha (3-12)

    • Chumvi na mwangaza (13-16)

    • Yesu alikuja kutimiza Sheria (17-20)

    • Mashauri juu ya kasirani (21-26), uzinifu (27-30), kuvunja ndoa (31, 32), viapo(33-37), kulipiza kisasi (38-42), kupenda maadui (43-48)

5  Wakati aliona watu wengi wanapanda kwenye mulima; na kisha yeye kukaa, wanafunzi wake wakamukaribia.  Halafu akafungua kinywa chake na kuanza kuwafundisha, na kusema:  “Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho,*+ kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wao.  “Wenye furaha ni wale wenye kuomboleza, kwa sababu watafarijiwa.+  “Wenye furaha ni wale wenye tabia ya upole,+ kwa sababu watariti dunia.+  “Wenye furaha ni wale wenye njaa na kiu+ ya haki, kwa sababu watashibishwa.+  “Wenye furaha ni wale wenye rehema,+ kwa sababu wataonyeshwa rehema.  “Wenye furaha ni wale wenye moyo safi,+ kwa sababu watamuona Mungu.  “Wenye furaha ni wale wenye kufanya amani,+ kwa sababu wataitwa wana wa Mungu. 10  “Wenye furaha ni wale wenye wameteswa kwa sababu ya haki,+ kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wao. 11  “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawalaumu+ na kuwatesa+ na kuwasingizia kila namna ya uovu kwa sababu yangu.+ 12  Mushangilie na kufurahi sana,+ kwa sababu zawabu yenu+ ni kubwa mbinguni, kwa maana ni vile walitesa manabii wenye waliwatangulia.+ 13  “Ninyi ni chumvi+ ya dunia, lakini kama chumvi inapoteza nguvu yake, ni nini inaweza kufanywa ili nguvu yake ya kukoleza irudie tena? Haina tena faida yoyote, inapaswa kutupwa inje+ ili ikanyangwe na watu. 14  “Ninyi ni mwangaza wa ulimwengu.+ Muji wenye kuwa kwenye mulima hauwezi kufichwa. 15  Watu wanawasha taa na kuiweka, hapana chini ya kitunga,* lakini wanaiweka juu ya kinara cha taa ili iangazie watu wote wenye kuwa ndani ya nyumba.+ 16  Vilevile, muache mwangaza wenu uangaze mbele ya watu,+ ili waone matendo yenu ya muzuri+ na wamutukuze Baba yenu wa mbinguni.+ 17  “Musiwaze nilikuja kuharibu Sheria ao Manabii. Sikukuja kuharibu, lakini nilikuja kutimiza.+ 18  Kwa kweli ninawaambia kwamba mbingu na dunia zinaweza kupita, lakini hakuna hata herufi moja ya kidogo zaidi ao sehemu moja ya herufi yenye itapita katika Sheria mupaka mambo yote yatimie.+ 19  Kwa hiyo, kila mutu mwenye anavunja moja ya amri hizi za kidogo zaidi na anafundisha wengine kufanya vile, ataitwa mudogo zaidi kuhusiana na Ufalme wa mbinguni. Lakini kila mutu mwenye anazifanya na kuzifundisha ataitwa mukubwa kuhusiana na Ufalme wa mbinguni. 20  Kwa maana ninawaambia kwamba kama haki yenu haipite ile ya waandishi na Wafarisayo,+ hamutaingia hata kidogo katika Ufalme wa mbinguni.+ 21  “Mulisikia kama watu wa zamani waliambiwa: ‘Haupaswe kuua,+ lakini kila mutu mwenye anaua atasamba mbele ya tribinali.’+ 22  Lakini, ninawaambia kwamba kila mutu mwenye anaendelea kumukasirikia+ ndugu yake atasamba mbele ya tribinali; na kila mutu mwenye anamuambia ndugu yake neno la zarau lenye halipaswe kusemwa atasamba mbele ya Tribinali Kubwa; na kila mutu mwenye anasema, ‘Wewe mupumbavu bure!’ atastahili moto wa Gehena.*+ 23  “Basi, kama unaleta zawadi yako kwenye mazabahu+ na pale unakumbuka kama ndugu yako iko* na jambo fulani juu yako, 24  acha zawadi yako pale mbele ya mazabahu, na uende. Fanya kwanza amani na ndugu yako, na kisha urudie na utoe zawadi yako.+ 25  “Sikilizana haraka na mutu mwenye anakushitaki, wakati mungali katika njia ya kuenda kwenye tribinali, ili kwa njia fulani mwenye kukushitaki asikutie katika mikono ya muamuzi, na muamuzi akutie katika mikono ya mutumishi wa tribinali, na utupwe katika gereza.+ 26  Hakika ninakuambia, hautatoka mule mupaka ulipe feza yako ya kidogo ya kichele ya mwisho.* 27  “Mulisikia kama ilisemwa: ‘Haupaswe kufanya uzinifu.’+ 28  Lakini mimi ninawaambia kama kila mutu mwenye anaendelea kumuangalia mwanamuke+ kwa njia ya kumutamani amekwisha kufanya uzinifu pamoja naye katika moyo wake.+ 29  Basi, kama jicho lako la kuume linafanya ujikwae, ulingoe na ulitupe mbali na wewe.+ Kwa maana ni muzuri zaidi upoteze kimoja cha viungo vyako kuliko mwili wako wote utupwe katika Gehena.*+ 30  Tena, kama mukono wako wa kuume unafanya ujikwae, uukate na kuutupa mbali na wewe.+ Kwa maana ni muzuri zaidi upoteze kimoja cha viungo vyako kuliko mwili wako wote uende katika Ge­hena.*+ 31  “Zaidi ya hayo, ilisemwa: ‘Kila mutu mwenye anavunja ndoa na bibi yake, amupatie cheti cha kuvunja ndoa.’+ 32  Lakini, mimi ninawaambia kwamba kila mutu mwenye anavunja ndoa na bibi yake, kama haiko tu kwa sababu ya uasherati,* anamutia bibi yake katika hatari ya kufanya uzinifu, na kila mutu mwenye anamuoa mwanamuke mwenye ndoa yake ilivunjika anafanya uzinifu.+ 33  “Tena mulisikia kama watu wa zamani waliambiwa: ‘Haupaswe kuapa na kisha ukose kutimiza,+ lakini unapaswa kutimiza naziri zako kwa Yehova.’*+ 34  Lakini, mimi ninawaambia: Musiape hata kidogo+ kwa mbingu kwa sababu ni kiti cha Ufalme cha Mungu; 35  ao kwa dunia, kwa sababu ni kiti cha miguu yake;+ ao kwa Yerusalemu, kwa sababu ni muji wa Mufalme mukubwa.+ 36  Usiape kwa kichwa chako, kwa sababu hauwezi kugeuza unywele mumoja kuwa mweupe ao mweusi. 37  Muache tu neno lenu ‘Ndiyo’ limaanishe ndiyo, na ‘Hapana’ yenu imaanishe hapana,+ kwa maana lenye kupita hayo linatoka kwa ule muovu.+ 38  “Mulisikia kama ilisemwa: ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’+ 39  Lakini, mimi ninawaambia: Musipingane na mutu muovu, lakini kila mutu mwenye anakupiga kofi kwenye shavu la kuume, umugeuzie pia lile lingine.+ 40  Na kama mutu anataka kukupeleka kwenye tribinali ili akamate nguo yako ya ndani, umuache akamate pia nguo yako ya inje;+ 41  na kama mutu mwenye mamlaka anakulazimisha umutumikie kilometre* moja, uende naye kilometre mbili. 42  Upatie mwenye anakuomba, na usimugeuzie mugongo mutu mwenye anataka umukopeshe.*+ 43  “Mulisikia kama ilisemwa: ‘Unapaswa kumupenda jirani yako+ na kuchukia adui yako.’ 44  Lakini, mimi ninawaambia ninyi: Muendelee kupenda maadui wenu+ na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatesa ninyi,+ 45  ili muonyeshe kuwa ninyi ni wana wa Baba yenu mwenye kuwa mbinguni,+ kwa sababu yeye anaangazia jua lake watu waovu na watu wazuri, tena ananyesha mvua juu ya wenye haki na wenye hawako wenye haki.+ 46  Kwa maana kama munapenda wale wenye wanawapenda ninyi, muko na zawabu gani?+ Je, wakusanya-kodi hawafanye jambo hilo pia? 47  Na kama munasalimia ndugu zenu tu, munafanya jambo gani lenye kupita la kawaida? Je, watu wa mataifa pia hawafanye jambo hilo pia? 48  Basi lazima mukuwe wakamilifu,* kama vile Baba yenu wa mbinguni ni mukamilifu.+

Maelezo ya Chini

Ao “wenye kuomba-omba roho.”
Ao “kitunga cha kupimia.”
Gehena ilikuwa mahali pa kuunguzia uchafu inje ya Yerusalemu. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Tnn., “leptoni ya mwisho.” Angalia Nyongeza B14.
Gehena ilikuwa mahali pa kuunguzia uchafu inje ya Yerusalemu. Angalia Maana ya Maneno.
Gehena ilikuwa mahali pa kuunguzia uchafu inje ya Yerusalemu. Angalia Maana ya Maneno.
Neno la Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “maili.” Angalia Nyongeza B14.
Ni kusema, mwenye anataka umukopeshe bila faida.
Ao “wenye kuenea.”