Kulingana na Matayo 2:1-23

  • Kutembelewa na watu wenye elimu ya nyota (1-12)

  • Kukimbilia Misri (13-15)

  • Herode anaua watoto wanaume (16-18)

  • Kurudia Nazareti (19-23)

2  Kisha Yesu kuzaliwa katika Betlehemu+ ya Yudea katika siku za mufalme Herode,*+ angalia! watu wenye elimu ya nyota* kutoka Mashariki walikuja Yerusalemu,  na kusema: “Iko* wapi ule mufalme wa Wayahudi+ mwenye alizaliwa? Kwa maana tuliona nyota yake wakati tulikuwa Mashariki, na tumekuja kuinama mbele yake.”  Wakati Mufalme Herode alisikia jambo hilo, yeye na watu wote wa Yerusalemu wakakuwa katika musukosuko.  Akakusanya wakubwa wote wa makuhani na waandishi wa watu na akawauliza ni wapi Kristo* alipaswa kuzaliwa.  Wakamuambia: “Katika Betlehemu+ ya Yudea, kwa maana iliandikwa hivi kupitia nabii:  ‘Na wewe, Ee Betlehemu ya inchi ya Yuda, wewe ndiye muji mudogo sana kati ya magavana wa Yuda, kwa maana kiongozi, mwenye atachunga watu wangu Israeli atatokea kwako.’”+  Kisha Herode akaita kwa siri wale watu wenye elimu ya nyota na kuwaomba wamuambie ni wakati gani kabisa ile nyota ilionekana.  Wakati aliwatuma Betlehemu, aliwaambia: “Muende na mutafute kwa uangalifu ule mutoto mudogo, na wakati mutamupata, muniletee habari ili mimi pia niende na kuinama mbele yake.”  Kisha kumusikiliza mufalme, wakaenda, na angalia! nyota yenye waliona wakati walikuwa Mashariki+ ikaenda mbele yao mupaka ikasimama juu ya mahali kwenye ule mutoto mudogo alikuwa. 10  Wakati waliona ile nyota, wakafurahi sana. 11  Na wakati waliingia ndani ya nyumba, wakaona ule mutoto mudogo pamoja na Maria mama yake, wakapiga magoti na kuinama mbele ya ule mutoto. Pia, wakafungua hazina zao na kumutolea zawadi—zahabu na ubani na manemane. 12  Lakini, kwa sababu Mungu aliwaonya kupitia ndoto+ wasirudie kwa Herode, wakaondoka na kuenda katika inchi yao kupitia njia ingine. 13  Kisha wao kuenda, angalia! malaika wa Yehova* akamutokea Yosefu katika ndoto,+ na kusema: “Simama, chukua ule mutoto mudogo na mama yake na ukimbilie Misri, na ukae kule mupaka wakati nitakuambia urudie; kwa maana Herode iko* karibu kutafuta ule mutoto mudogo ili amuue.” 14  Basi Yosefu akasimama na akamuchukua mutoto na mama ya ule mutoto wakati wa usiku na akaenda Misri. 15  Akakaa kule mupaka wakati Herode alikufa. Hilo lilitimiza neno lenye lilisemwa na Yehova* kupitia nabii wake, wakati alisema: “Kutoka Misri nilimuita mwana wangu.”+ 16  Kisha, wakati Herode aliona kuwa wale watu wenye elimu ya nyota wamemudanganya, akakasirika sana, na akatuma watu waue watoto wote wanaume katika Betlehemu na katika wilaya zake zote, kuanzia miaka mbili na kushuka chini, kulingana na wakati wale watu wenye elimu ya nyota walikuwa wamemuhakikishia kabisa.+ 17  Halafu likatimia lile neno lenye lilisemwa kupitia nabii Yeremia, mwenye alisema: 18  “Sauti ilisikika katika Rama, kilio na maombolezo makubwa. Raheli+ ndiye alikuwa analilia watoto wake, na hakutaka kufarijiwa, kwa sababu hawako tena.”+ 19  Kisha kifo cha Herode, angalia! Malaika wa Yehova* akamutokea Yosefu katika ndoto+ kule Misri 20  na kusema: “Simama, chukua ule mutoto na mama yake na uende katika inchi ya Israeli, kwa sababu wale wenye walikuwa wanatafuta uzima wa* ule mutoto wamekufa.” 21  Basi akasimama na kuchukua ule mutoto na mama yake na akaingia katika inchi ya Israeli. 22  Lakini wakati alisikia kama Arkelao alikuwa anatawala Yudea pa nafasi ya Herode baba yake, akaogopa kuenda kule. Zaidi ya hayo, kwa kuwa Mungu alimuonya katika ndoto,+ akaenda katika eneo la Galilaya.+ 23  Na akaenda na kukaa katika muji wenye kuitwa Nazareti,+ ili neno lenye lilisemwa kupitia manabii litimie: “Ataitwa Munazareti.”*+

Maelezo ya Chini

Ao “wanajimu.”
Ao “Eko.”
Ao “Masiya; Mutiwa-Mafuta.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi ya.”
Pengine ni kutokana na neno la Kiebrania “chipukizi.”