Kulingana na Matayo 24:1-51

  • ALAMA YA KUWAPO KWA KRISTO (1-51)

    • Vita, upungufu wa chakula, matetemeko ya inchi (7)

    • Habari njema itahubiriwa (14)

    • Taabu kubwa (21, 22)

    • Alama ya Mwana wa binadamu (30)

    • Muti wa tini (32-34)

    • Kama siku za Noa (37-39)

    • Muendelee kukesha (42-44)

    • Mutumwa mwaminifu na mutumwa muovu (45-51)

24  Sasa, wakati Yesu alikuwa anatoka katika hekalu, wanafunzi wake wakamukaribia ili kumuonyesha majengo ya hekalu.  Akawajibu na kuwaambia: “Je, hamuone vitu hivi vyote? Kwa kweli ninawaambia ninyi, hakuna jiwe lenye litaachwa hapa juu ya jiwe bila kuangushwa chini.”+  Wakati alikuwa amekaa chini kwenye Mulima wa Mizeituni, wanafunzi wakamukaribia akiwa peke yake, na kusema: “Tuambie, mambo haya yatakuwa wakati gani, na ni nini itakuwa alama ya kuwapo*+ kwako na ya umalizio wa mupangilio wa mambo?”*+  Yesu akawajibu na kuwaambia: “Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwapotoshe,+  kwa maana wengi watakuja wakitumia jina langu, na kusema, ‘Mimi ndiye Kristo,’ na watapotosha watu wengi.+  Mutasikia juu ya vita na habari za vita. Mufanye angalisho kwamba musiogope, kwa maana mambo hayo lazima yatokee, lakini ule mwisho bado.+  “Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme,+ na kutakuwa upungufu wa chakula+ na matetemeko ya inchi mahali pamoja kisha pengine.+  Mambo hayo yote ni mwanzo wa maumivu ya taabu.  “Kisha watu watawatia ninyi katika taabu+ na watawaua ninyi,+ na mutachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.+ 10  Kisha tena, wengi watakwazika, watasalitiana, na kuchukiana. 11  Manabii wengi wa uongo watatokea na kupotosha watu wengi;+ 12  na kwa sababu ya kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria, upendo wa watu wengi utapoa. 13  Lakini ule mwenye atavumilia* mupaka mwisho ataokolewa.+ 14  Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote,+ na kisha ule mwisho utakuja. 15  “Kwa hiyo, wakati mutaona lile chukizo lenye linaleta uharibifu limesimama mahali patakatifu, kama vile nabii Danieli alisema+ (musomaji atumie utambuzi), 16  basi wale wenye kuwa katika Yudea waanze kukimbilia kwenye milima.+ 17  Mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba asishuke ili kukamata vitu katika nyumba yake, 18  na mutu mwenye kuwa katika shamba asirudie ili kukamata nguo yake ya inje. 19  Ole wao wanamuke wenye mimba na wale wenye kunyonyesha watoto katika siku hizo! 20  Muendelee kusali kwamba wakati mutakimbia isikuwe katika kipindi cha baridi ao siku ya Sabato; 21  kwa maana kutakuwa taabu kubwa+ yenye haijatokea tangu mwanzo wa ulimwengu mupaka sasa, hapana, na haitatokea tena.+ 22  Kwa kweli, kama siku hizo hazingefupishwa, hakuna mwili wowote wenye ungeokolewa; lakini kwa sababu ya wale wenye kuchaguliwa, siku hizo zitafupishwa.+ 23  “Basi, kama mutu yeyote anawaambia ninyi, ‘Muangalie! Kristo iko* hapa,’+ ao, ‘Iko pale!’ musiamini.+ 24  Kwa maana Makristo wa uongo na manabii wa uongo+ watatokea na watafanya alama kubwa na maajabu ili kupotosha,+ ikiwezekana, hata wale wenye kuchaguliwa. 25  Muangalie! Nimewaonya ninyi mbele ya wakati. 26  Basi, kama watu wanawaambia ninyi, ‘Muangalie! Iko* katika jangwa,’ musiende; ‘Muangalie! Iko katika vyumba vya ndani,’ musiamini.+ 27  Kwa maana kama vile umeme wa radi unatokea mashariki na kuangaza mupaka mangaribi, ni vile kuwapo* kwa Mwana wa binadamu kutakuwa.+ 28  Kila mahali kwenye kuwa muzoga, ni pale tai watakusanyika pamoja.+ 29  “Kisha tu taabu ya siku hizo, jua litatiwa giza,+ na mwezi hautatoa mwangaza wake, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni, na nguvu za mbingu zitatikiswa.+ 30  Kisha alama ya Mwana wa binadamu itaonekana mbinguni, na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni,+ na wataona Mwana wa binadamu+ akikuja juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.+ 31  Na atatuma malaika wake pamoja na sauti kubwa ya tarumbeta, na watakusanya watu wake wenye kuchaguliwa kutoka pande ine (4) za dunia,* kutoka mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho mwingine.+ 32  “Sasa mujifunze mufano huu kuhusu muti wa tini: Wakati tu matawi yake machanga yanakuwa teketeke na kutoa majani, munajua kwamba kipindi cha joto kinakaribia.+ 33  Vilevile ninyi pia, wakati mutaona mambo yote hayo, mujue kama iko* karibu kwenye milango.+ 34  Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kizazi hiki hakitapita hata kidogo mupaka mambo haya yote yatokee. 35  Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita hata kidogo.+ 36  “Kuhusu siku ile na saa ile, hakuna mutu mwenye anajua,+ ikuwe malaika wa mbinguni ao Mwana, lakini Baba tu.+ 37  Kwa maana kama vile siku za Noa zilikuwa,+ ni vile kuwapo* kwa Mwana wa binadamu kutakuwa.+ 38  Kwa maana kama vile walikuwa katika siku hizo mbele ya Garika, walikuwa wanakula na kunywa, wanaume walikuwa wanaoa na wanamuke walikuwa wanaolewa, mupaka siku ile Noa aliingia ndani ya safina,+ 39  na hawakuhangaika mupaka Garika ikakuja na kuwaharibu wote,+ ni vile kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakuwa. 40  Wakati huo watu wawili watakuwa katika shamba; mumoja atachukuliwa na mwingine ataachwa. 41  Wanamuke wawili watakuwa wakisaga kwenye jiwe la kusagia la mukono; mumoja atachukuliwa na mwingine ataachwa.+ 42  Kwa hiyo, muendelee kukesha kwa sababu hamujue Bwana wenu atakuja siku gani.+ 43  “Lakini mujue jambo hili: Kama mwenye nyumba angejua ni wakati gani wa usiku* mwizi atakuja,+ angekaa macho na hangeruhusu nyumba yake ivunjwe.+ 44  Kwa hiyo ninyi pia mukuwe tayari,+ kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa yenye hamuwazie. 45  “Ni nani kwa kweli mutumwa muaminifu na mwenye busara* mwenye bwana wake ameweka juu ya watumishi wake wa nyumbani, ili kuwapatia chakula chao kwa wakati wenye kufaa?+ 46  Mwenye furaha ni mutumwa huyo kama bwana wake wakati atakuja atamukuta akifanya vile!+ 47  Kwa kweli ninawaambia ninyi, atamuweka juu ya mali zake zote. 48  “Lakini kama mutumwa huyo muovu anasema katika moyo wake, ‘Bwana wangu anakawia,’+ 49  na anaanza kupiga watumwa wenzake na kula na kunywa pamoja na walevi wakubwa, 50  bwana wa mutumwa huyo atakuja siku yenye hakutazamia na katika saa yenye hajue,+ 51  na atamupatia azabu kwa ukali mukubwa zaidi na kumuweka pamoja na wanafiki. Ni kule atalia na kusaga meno yake.+

Maelezo ya Chini

Ao “mufumo wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “anavumilia.”
Ao “eko.”
Ao “Eko.”
Tnn., “pepo ine za dunia.”
Ao “eko.”
Ao “katika kesha gani.”
Ao “mwenye hekima.”