Kulingana na Matayo 23:1-39

  • Musiige waandishi na Wafarisayo (1-12)

  • Ole wao waandishi na Wafarisayo (13-36)

  • Yesu anaomboleza juu ya Yerusalemu (37-39)

23  Kisha Yesu akaambia watu wengi na wanafunzi wake, na kusema:  “Waandishi na Wafarisayo wamejiikalisha katika kiti cha Musa.  Kwa hiyo, mambo yote yenye wanawaambia, muyafanye na kuyashika, lakini musitende kulingana na matendo yao, kwa maana wao wanasema lakini hawatende mambo yenye wanasema.+  Wanafunga mizigo mizito na kuiweka kwenye mabega ya watu,+ lakini wao wenyewe hawataki kuisogeza kwa kidole chao.+  Kazi zote zenye wanafanya, wanazifanya ili waonekane na watu,+ kwa maana wanapanua visanduku vyenye kuwa na maandiko ndani vyenye wanavaa kama ulinzi,*+ na wanarefusha sehemu za chini za nguo zao.+  Wanapenda nafasi za heshima zaidi kwenye chakula cha mangaribi na viti vya mbele* katika masinagogi+  na salamu katika masoko na kuitwa Rabi* na watu.  Lakini ninyi, musiitwe Rabi, kwa maana Mwalimu wenu ni mumoja,+ na ninyi wote ni ndugu.  Zaidi ya hayo, musimuite mutu yeyote baba yenu katika dunia, kwa maana Baba yenu ni mumoja,+ Ule wa mbinguni. 10  Wala musiitwe viongozi, kwa maana Kiongozi wenu ni mumoja, Kristo. 11  Lakini mwenye kuwa mukubwa zaidi kati yenu anapaswa kuwa mutumishi wenu.+ 12  Kila mutu mwenye kujiinua atanyenyekezwa,+ na kila mutu mwenye kujinyenyekeza atainuliwa.+ 13  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki! kwa sababu munafungia watu Ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi wenyewe hamuingie, na wale wenye wanataka kuingia munawazuia.+ 14 * —— 15  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu munasafiri katika bahari na kwenye inchi kavu ili kufanya mutu mumoja kuwa mugeuzwa-imani, na wakati amegeuzwa imani, munamufanya astahili Gehena* mara mbili zaidi kuliko ninyi. 16  “Ole wenu, viongozi vipofu+ wenye kusema, ‘Kama mutu yeyote anaapa kwa hekalu, hakuna ubaya; lakini kama mutu yeyote anaapa kwa zahabu ya hekalu, anapaswa kutimiza kiapo chake.’+ 17  Wapumbavu na vipofu! Kwa kweli, ni nini yenye kuwa kubwa zaidi, zahabu ao hekalu lenye limetakasa zahabu hiyo? 18  Tena munasema, ‘Kama mutu yeyote anaapa kwa mazabahu, hakuna ubaya; lakini kama mutu yeyote anaapa kwa zawadi yenye kuwa kwenye mazabahu, anapaswa kutimiza kiapo chake.’ 19  Ninyi vipofu! Kwa kweli, ni nini yenye kuwa kubwa zaidi, zawadi ao mazabahu yenye inatakasa zawadi hiyo? 20  Kwa hiyo, kila mutu mwenye anaapa kwa mazabahu anaapa kwa mazabahu na kwa vitu vyote vyenye kuwa juu yake; 21  na kila mutu mwenye anaapa kwa hekalu anaapa kwa hekalu na kwa Ule mwenye kukaa ndani yake;+ 22  na kila mutu mwenye anaapa kwa mbingu anaapa kwa kiti cha ufalme cha Mungu na kwa Ule mwenye kukaa juu yake. 23  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki! kwa sababu munatoa sehemu moja ya kumi (1/10) ya munanaa na dili na bizari,+ lakini mumepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, ni kusema, haki,+ rehema,+ na uaminifu. Mambo hayo, ilikuwa lazima kuyafanya, bila kupuuza yale mengine.+ 24  Viongozi vipofu,+ wenye kuchuya imbu+ lakini munameza ngamia!+ 25  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki! kwa sababu munasafisha upande wa inje wa kikombe na wa sahani,+ lakini ndani vimejaa pupa*+ na kukosa kujizuia.+ 26  Mufarisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe na sahani, ili upande wake wa inje ukuwe safi pia. 27  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu munafanana na makaburi yenye kupakaliwa rangi nyeupe,*+ yenye kwa inje, yanaonekana kabisa kuwa yenye kupendeza lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila namna ya uchafu. 28  Vilevile, kwa inje munaonekana mbele ya watu kuwa wenye haki, lakini ndani mumejaa unafiki na uvunjaji wa sheria.+ 29  “Ole wenu, waandishi na Wafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu munajenga makaburi ya manabii na kupamba makaburi* ya wenye haki,+ 30  na munasema, ‘Kama tungeishi katika siku za mababu zetu, hatungejiunga nao ili kumwanga damu ya manabii.’ 31  Kwa hiyo, munashuhudia juu yenu wenyewe kuwa ninyi ni wana wa wale wenye waliua manabii.+ 32  Basi, mujaze kipimo cha mababu zenu. 33  “Ninyi nyoka, uzao wa nyoka-vipiri,+ mutakimbia namna gani hukumu ya Gehena?*+ 34  Kwa sababu hiyo, ninatuma kwenu manabii+ na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.+ Wamoja kati yao mutawaua+ na kuwapigilia misumari kwenye miti, na wamoja kati yao mutawapiga mijeledi+ katika masinagogi yenu na kuwatesa+ katika muji baada ya muji, 35  ili damu yote yenye haki yenye ilimwangwa katika dunia ikuje juu yenu, kuanzia damu ya Abeli+ mwenye haki mupaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mwenye muliua kati ya patakatifu na mazabahu.+ 36  Kwa kweli ninawaambia ninyi, mambo yote haya yatafikia kizazi hiki. 37  “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na mwenye kupiga majiwe wale wenye walitumwa kwake+​—ni mara ngapi nilitaka kukusanya watoto wako, kama vile kuku anakusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka.+ 38  Angalia! Mungu ameacha nyumba yenu.*+ 39  Kwa maana ninawaambia ninyi, tangu sasa hamutaniona tena mupaka wakati mutasema, ‘Amebarikiwa ule mwenye anakuja katika jina la Yehova!’”*+

Maelezo ya Chini

Ao “wanapanua tepe zao.”
Ao “vya muzuri zaidi.”
Ao “Mwalimu.”
Gehena ilikuwa mahali pa kuunguzia uchafu inje ya Yerusalemu. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “unyanganyi.”
Ao “yenye yamepakaliwa chokaa.”
Ao “makaburi ya ukumbusho.”
Gehena ilikuwa mahali pa kuunguzia uchafu inje ya Yerusalemu. Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “imeachwa kwenu ukiwa.”