Matendo ya Mitume 7:1-60

  • Hotuba ya Stefano mbele ya Sanhedrini (1-53)

    • Nyakati za wazee wa ukoo (2-16)

    • Uongozi wa Musa; Waisraeli wanaabudu sanamu (17-43)

    • Mungu haishi katika mahekalu yenye yalifanywa na wanadamu (44-50)

  • Stefano anapigwa majiwe (54-60)

7  Lakini kuhani mukubwa akasema: “Je, mambo hayo ni kweli?”  Stefano akajibu: “Wanaume, ndugu na baba, musikilize. Mungu wa utukufu alitokea babu yetu Abrahamu wakati alikuwa Mesopotamia, mbele aanze kuishi Harani,+  na akamuambia: ‘Toka katika inchi yako na kwa watu wa jamaa yako na ukuje katika inchi yenye nitakuonyesha.’+  Kisha akatoka katika inchi ya Wakaldayo na akaanza kuishi Harani. Na kutoka pale, kisha baba yake kufa,+ Mungu akamuamuru ahamie katika inchi hii yenye ninyi munaishi ndani sasa.+  Hata hivyo, hakumupatia uriti wowote ndani yake, hapana, hata sehemu yenye kuenea ukubwa wa kukanyanga kwa muguu wake; lakini aliahidi kumupatia ikuwe mali yake na kisha yeye kuipatia wazao wake,*+ hata kama alikuwa hajapata mutoto.  Zaidi ya hayo, Mungu alimuambia kwamba wazao wake* watakuwa wageni katika inchi yenye haiko yao na kwamba watu wa inchi hiyo watawafanya kuwa watumwa na watawatesa* kwa miaka mia ine (400).+  Mungu akasema: ‘Na taifa hilo lenye watatumikia kama watumwa nitalihukumu,+ na kisha mambo hayo watatoka kule na watanitolea utumishi mutakatifu mahali hapa.’+  “Alimupatia pia agano la kutahiriwa,+ na akamuzaa Isaka+ na akamutahiri siku ya munane (8),+ na Isaka akamuzaa* Yakobo, na Yakobo akazaa wale vichwa vya familia* kumi na mbili (12).  Na wale vichwa vya familia wakamusikilia Yosefu+ wivu na wakamuuzisha apelekwe Misri.+ Lakini Mungu alikuwa pamoja naye,+ 10  na akamukomboa kutoka katika taabu zake zote na akamukubali na kumupatia hekima mbele ya Farao mufalme wa Misri. Na akamuweka aongoze Misri na nyumba yake yote.+ 11  Lakini njaa ikakuja juu ya Misri yote na Kanaani, ndiyo, taabu kubwa, na mababu zetu hawakukuwa na kitu chochote cha kula.+ 12  Lakini Yakobo akasikia kwamba Misri kulikuwa chakula,* na akatuma mababu zetu mara ya kwanza.+ 13  Mara ya pili, Yosefu akajitambulisha kwa ndugu zake, na familia ya Yosefu ikajulikana kwa Farao.+ 14  Basi Yosefu akatuma ujumbe na kumuita Yakobo baba yake na watu wote wa jamaa yake kutoka kule,+ wote walikuwa watu* makumi saba na tano (75).+ 15  Basi Yakobo akashuka kuenda Misri,+ na akakufia kule,+ na vilevile mababu zetu.+ 16  Wakabebwa mupaka Shekemu na kulalishwa katika kaburi lenye Abrahamu alikuwa amenunua kwa wana wa Hamori kwa kiasi fulani cha feza kule Shekemu.+ 17  “Kwa kuwa wakati wa kutimizwa kwa ahadi yenye Mungu alikuwa amemutangazia Abrahamu ulikuwa umekaribia, watu waliongezeka na wakakuwa wengi katika Misri, 18  mupaka mufalme mwingine akaanza kutawala juu ya Misri, mufalme mwenye hakumujua Yosefu.+ 19  Huyu akatendea jamii yetu kwa ujanja na akalazimisha kimakosa baba waache watoto wao wadogo ili wasiendelee kuishi.+ 20  Wakati huo Musa akazaliwa, na alikuwa mwenye sura na umbo ya muzuri hata mbele ya macho ya Mungu. Na akanyonyeshwa* kwa miezi tatu (3) katika nyumba ya baba yake.+ 21  Lakini wakati alitupwa,+ binti ya Farao akamuchukua na kumulea kama mwana wake mwenyewe.+ 22  Basi Musa akafundishwa katika hekima yote ya Wamisri. Kwa kweli, alikuwa na nguvu katika maneno yake na matendo yake.+ 23  “Sasa wakati alifikia miaka makumi ine (40), wazo likaingia katika moyo wake la* kutembelea* ndugu zake, wana wa Israeli.+ 24  Wakati aliona mumoja wao akitendewa bila haki, akamutetea na akamupiga na kumuua ule Mumisri ili kulipiza kisasi kwa ajili ya ule mwenye alikuwa anatendewa mubaya. 25  Aliwaza ndugu zake wataelewa kwamba Mungu alikuwa anawapatia wokovu kupitia mukono wake, lakini hawakuelewa vile. 26  Siku yenye ilifuata aliwakuta wako wanapigana, na akajaribu kuwapatanisha kwa amani; akasema: ‘Wanaume, ninyi ni ndugu. Sababu gani munatendeana mubaya?’ 27  Lakini ule mwenye alikuwa anamutendea jirani yake mubaya akamusukuma mbali na kumuambia: ‘Ni nani alikuweka kuwa mutawala na muamuzi juu yetu? 28  Je, unataka kuniua kama vile ulimuua ule Mumisri jana?’ 29  Wakati Musa alisikia maneno hayo, akakimbia na kuenda kuishi akiwa mugeni katika inchi ya Midiani, na kule akazaa wana wawili.+ 30  “Kisha miaka makumi ine (40) kupita, malaika akamutokea katika jangwa la Mulima Sinai katika mwali wa moto wa muti mudogo wa miiba wenye kuwaka.+ 31  Wakati Musa aliona jambo hilo akashangaa sana. Lakini wakati alikuwa anakaribia ili kuchunguza, sauti ya Yehova* ikasikika: 32  ‘Mimi ni Mungu wa mababu zako, Mungu wa Abrahamu na wa Isaka na wa Yakobo.’+ Musa akaanza kutetemeka na hakupima tena kuchunguza zaidi. 33  Yehova* akamuambia, ‘Vua viatu kwenye miguu yako, kwa maana mahali unasimama ni udongo mutakatifu. 34  Kwa kweli nimeona namna watu wangu wenye kuwa Misri wanakandamizwa, na nimesikia kilio chao cha maumivu,+ na nimeshuka ili kuwakomboa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’ 35  Uleule Musa mwenye walikana, kwa kusema: ‘Ni nani alikuweka kuwa mutawala na muamuzi?’+ yeye ndiye Mungu alituma+ akiwa mutawala na mukombozi kupitia malaika mwenye alimutokea katika muti mudogo wa miiba. 36  Mutu huyu aliwatosha Misri,+ kwa kufanya maajabu na alama katika Misri+ na kwenye Bahari Nyekundu+ na katika jangwa kwa miaka makumi ine (40).+ 37  “Huyo ndiye ule Musa mwenye aliambia wana wa Israeli: ‘Mungu atawainulia ninyi kutoka kati ya ndugu zenu nabii kama mimi.’+ 38  Huyo ndiye alikuja kuwa katikati ya kutaniko katika jangwa pamoja na malaika+ mwenye alisema naye+ kwenye Mulima Sinai na pamoja na mababu zetu, na akapokea maneno matakatifu yenye uzima ili atupatie.+ 39  Mababu zetu walikataa kumutii, lakini walimusukuma pembeni+ na katika mioyo yao wakarudia Misri,+ 40  wakamuambia Haruni: ‘Ututengenezee miungu iende mbele yetu. Kwa maana hatujue kile kimemufikia huyu Musa, mwenye alitutosha katika inchi ya Misri.’+ 41  Basi wakatengeneza kitoto-dume cha ngombe katika siku hizo na wakaletea sanamu hiyo zabihu, na wakaanza kujifurahisha katika kazi za mikono yao.+ 42  Basi Mungu akawaacha na kuwatoa ili watolee jeshi la mbinguni utumishi mutakatifu,+ kama vile imeandikwa katika kitabu cha Manabii: ‘Je, mimi ndiye mulitolea matoleo na zabihu kwa miaka makumi ine (40) katika jangwa, Ee nyumba ya Israeli? 43  Lakini mulikamata hema ya Moloki+ na nyota ya mungu Refani, sanamu zenye mulitengeneza ili kuziabudu. Kwa hiyo, nitawahamishia mbali kuliko hata Babiloni.’+ 44  “Mababu zetu walikuwa na hema ya ushahidi katika jangwa, kama vile Yeye alitoa maagizo wakati alikuwa anasema na Musa ili kulifanya kulingana na mufano wenye alikuwa ameona.+ 45  Na mababu zetu walilipokea kuwa uriti na wakalileta pamoja na Yoshua katika inchi yenye ilikuwa mali ya mataifa,+ yenye Mungu alifukuza kutoka mbele ya mababu zetu.+ Lilibakia hapa mupaka siku za Daudi. 46  Alikubaliwa mbele ya macho ya Mungu na akaomba pendeleo la kujenga makao kwa ajili ya Mungu wa Yakobo.+ 47  Lakini Sulemani ndiye alimujengea nyumba.+ 48  Hata hivyo, Mwenye Kuwa Juu Zaidi hakae katika nyumba zenye zilifanywa kwa mikono,+ kama vile nabii anasema: 49  ‘Mbingu ni kiti changu cha ufalme,+ na dunia ni kiti cha miguu yangu.+ Mutanijengea nyumba ya namna gani? Yehova* anasema. Ao mahali pangu pa kupumuzikia pako wapi? 50  Mukono wangu ulifanya vitu hivi vyote, haiko vile?’+ 51  “Ninyi watu wenye kuwa kichwa-nguvu na wenye hawatahiriwe katika mioyo na masikio, sikuzote munapinga roho takatifu; kama vile mababu zenu walifanya, ni vile munafanya.+ 52  Ni nani kati ya manabii mwenye mababu zenu hawakutesa?+ Ndiyo, waliua wale wenye walitangaza mbele ya wakati kuja kwa ule mwenye haki,+ mwenye ninyi mulisaliti na kuua,+ 53  ninyi wenye mulipokea Sheria kupitia malaika+ lakini hamukuishika.” 54  Basi, wakati walisikia mambo hayo wakakasirika sana* katika mioyo yao na wakaanza kumusagia meno. 55  Lakini yeye, akiwa amejaa roho takatifu, akaangalia mbinguni na akaona utukufu wa Mungu na Yesu akiwa amesimama kwenye mukono wa kuume wa Mungu,+ 56  na akasema: “Angalia! ninaona mbingu zimefunguka na Mwana wa binadamu+ amesimama kwenye mukono wa kuume wa Mungu.”+ 57  Halafu wakafanya makelele kwa sauti yao yote na kutia mikono yao kwenye masikio yao na wote pamoja wakamurukia. 58  Kisha kumutupa inje ya muji, wakaanza kumupiga majiwe.+ Mashahidi+ wakatia nguo zao za inje kwenye miguu ya kijana mwenye kuitwa Sauli.+ 59  Wakati walikuwa wanamupiga Stefano majiwe, akaomba hivi: “Bwana Yesu, pokea roho yangu.” 60  Kisha akapiga magoti, akasema kwa sauti kubwa: “Yehova,* usiwahesabie zambi hii.”+ Na kisha kusema maneno hayo, akalala usingizi katika kifo.

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbegu yake.”
Tnn., “mbegu yake.”
Ao “watawatendea mubaya.”
Ao “wazee wa ukoo.”
Ao pengine, “akafanya vilevile kwa.”
Ao “nafaka.”
Ao “nafsi.”
Ao “akalelewa.”
Ao “akaamua.”
Ao “kuchunguza.”
Ao “wakasikia wameumizwa.”