Kwa Waroma 12:1-21

  • Mutoe miili yenu ikuwe zabihu yenye uzima (1, 2)

  • Zawadi mbalimbali lakini mwili mumoja (3-8)

  • Mashauri juu ya maisha ya Wakristo wa kweli (9-21)

12  Kwa sababu hiyo, ndugu, ninawaomba kwa huruma za Mungu, mutoe miili yenu+ ikuwe zabihu yenye uzima, takatifu,+ na yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mutakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.+  Na muache kufinyangwa na mupangilio huu wa mambo,* lakini mugeuzwe kwa kufanya upya akili yenu,+ ili mujihakikishie ninyi wenyewe+ mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.  Kwa maana kupitia fazili zenye hazistahiliwe zenye nilipewa, ninaambia kila mutu pale kati yenu asijifikirie yeye mwenyewe sana kuliko vile inaomba kufikiri,+ lakini afikiri ili akuwe na akili ya muzuri, kila mumoja kama vile Mungu alimupatia* kipimo cha imani.+  Kwa maana kama vile tuko na viungo vingi katika mwili mumoja,+ lakini viungo hivyo havifanye kazi ileile,  ni vile sisi pia, hata kama tuko wengi, tuko mwili mumoja katika umoja na Kristo, lakini kila mumoja wetu ni kiungo cha mwingine.+  Basi, kwa kuwa tuko na zawadi zenye kuwa tofauti kulingana na fazili zenye hazistahiliwe zenye tulipewa,+ kama ni zawadi ya unabii, tutoe unabii kulingana na kipimo cha imani yenye tuligawiwa;  ao kama ni utumishi, tukuwe katika utumishi huu; ao ule mwenye kufundisha, aendelee kufundisha;+  ao ule mwenye kutia moyo,* atie moyo;+ ule mwenye kugawa,* afanye vile kwa ukarimu;+ ule mwenye kusimamia,* afanye vile kwa bidii;+ ule mwenye kuonyesha rehema, afanye vile kwa uchangamufu.+  Upendo wenu ukuwe bila unafiki.+ Muchukie sana mambo maovu;+ mushikamane na mambo mema. 10  Katika upendo wa kindugu mukuwe na upendo wenye upole* kwa mutu na mwenzake. Katika kuonyeshana heshima, mukuwe wa kwanza.+ 11  Mukuwe wenye bidii, hapana wavivu.*+ Muwake roho.+ Mumutumikie Yehova.*+ 12  Mufurahi katika tumaini. Muvumilie chini ya taabu.+ Mudumu katika sala.+ 13  Mushiriki pamoja na watakatifu kulingana na mambo yenye wako nayo lazima.+ Mufuate njia ya ukaribishaji-wageni.+ 14  Muendelee kubariki wale wenye wanawatesa ninyi;+ mubariki lakini musilaani.+ 15  Mufurahi pamoja na wale wenye kufurahi; mulie pamoja na wale wenye kulia. 16  Mukuwe na mutazamo uleule kuelekea wengine kama ule wenye muko nao kuelekea ninyi wenyewe; musikaze akili yenu juu ya mambo ya hali ya juu, lakini muongozwe na mambo ya hali ya chini.+ Musikuwe wenye hekima mbele ya macho yenu wenyewe.+ 17  Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu.+ Mufanye mambo ya muzuri mbele ya macho ya* watu wote. 18  Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani na watu wote.+ 19  Wapendwa, musijilipizie kisasi, lakini muachie kasirani kali* nafasi;+ kwa maana imeandikwa: “‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa,’ ni vile Yehova* anasema.”+ 20  Lakini, “kama adui yako iko* na njaa, mupatie chakula; kama iko* na kiu, mupatie kitu akunywe; kwa maana kwa kufanya vile utakusanya makaa yenye moto juu ya kichwa chake.”*+ 21  Usiache ushindwe na uovu, lakini endelea kushinda uovu kwa wema.+

Maelezo ya Chini

Ao “mufumo huu wa mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “alimugawia.”
Ao “kuongoza.”
Ao “kuchangia.”
Ao “kuhimiza.”
Ao “upendo mwororo.”
Ao “musikuwe wavivu katika kazi zenu.”
Ao “kulingana na mawazo ya.”
Ni kusema, kasirani kali ya Mungu.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ni kusema, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.