Kulingana na Luka 6:1-49

  • Yesu ni “Bwana wa Sabato” (1-5)

  • Mutu mwenye mukono wenye kukauka anaponyeshwa (6-11)

  • Mitume kumi na mbili (12-16)

  • Yesu anafundisha na kuponyesha (17-19)

  • Furaha na ole (20-26)

  • Kupenda maadui (27-36)

  • Muache kuhukumu (37-42)

  • Muti unajulikana kwa matunda yake (43-45)

  • Nyumba yenye ilijengwa muzuri; nyumba yenye haina musingi wenye nguvu (46-49)

6  Sasa, siku moja ya Sabato alikuwa anapita katikati ya mashamba ya nafaka, na wanafunzi wake walikuwa wanakata masuke ya nafaka na kuyakula,+ wakitosha maganda kwa mikono yao.+  Halafu Wafarisayo fulani wakasema: “Sababu gani munafanya jambo lenye haliruhusiwe siku ya Sabato?”+  Lakini Yesu akajibu na kuwaambia: “Je, hamujasoma hata siku moja jambo lenye Daudi alifanya wakati yeye na watu wenye walikuwa pamoja naye walikuwa na njaa?+  Namna aliingia ndani ya nyumba ya Mungu na akapewa mikate ya toleo,* akakula na akapatia watu wenye walikuwa pamoja naye, mikate yenye hakuna mutu mwenye alikuwa na ruhusa ya kula isipokuwa tu makuhani?”+  Kisha akawaambia: “Mwana wa binadamu ni Bwana wa Sabato.”+  Siku ingine ya Sabato+ aliingia katika sinagogi na akaanza kufundisha. Na pale kulikuwa mutu mumoja mwenye mukono wake wa kuume ulikuwa wenye kukauka.*+  Waandishi na Wafarisayo walikuwa sasa wanamuangalia Yesu sana waone kama ataponyesha siku ya Sabato, ili wapate njia fulani ya kumushitaki.  Lakini, alijua mawazo yao,+ basi akamuambia ule mutu mwenye mukono wenye kukauka:* “Simama na ukuje katikati.” Na akainuka na kusimama pale.  Kisha Yesu akawaambia: “Ninawauliza ninyi, je, inaruhusiwa siku ya Sabato kufanya mambo ya muzuri ao mambo ya mubaya, kuokoa uzima* ao kuuharibu?”+ 10  Kisha kuwaangalia wote huku na huku, akamuambia mutu huyo: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, na mukono wake ukapona. 11  Lakini wakakasirika sana, na wakaanza kuzungumuza kati yao ni jambo gani wangemutendea Yesu. 12  Siku moja, Yesu alienda kwenye mulima ili kusali,+ na akasali kwa Mungu usiku wote.+ 13  Wakati usiku ulikuwa umekucha, akaita wanafunzi wake na akachagua kumi na mbili (12) kati yao, wenye aliita pia mitume:+ 14  Simoni, mwenye alipatia pia jina Petro, Andrea ndugu yake, Yakobo, Yohana, Filipo,+ Bartolomayo, 15  Matayo, Tomasi,+ Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni mwenye anaitwa “mwenye bidii,” 16  Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Iskariote, mwenye aligeuka kuwa musaliti. 17  Na akashuka pamoja nao na akasimama mahali tambarare, na kulikuwa kundi kubwa la wanafunzi wake, na kundi kubwa la watu kutoka Yudea yote na Yerusalemu na eneo la Tiro na Sidoni lenye kuwa pembeni ya bahari; walikuja kumusikiliza na kuponyeshwa magonjwa yao. 18  Hata wale wenye walisumbuliwa na roho wachafu waliponyeshwa. 19  Na watu wote walitafuta kumugusa, kwa sababu nguvu zilikuwa zinamutoka+ na kuwaponyesha wote. 20  Akainua macho na kuangalia wanafunzi wake na akaanza kusema: “Wenye furaha ni ninyi maskini, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wenu.+ 21  “Wenye furaha ni ninyi wenye kuwa na njaa sasa, kwa maana mutashiba.+ “Wenye furaha ni ninyi wenye kulia sasa, kwa maana muta­cheka.+ 22  “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawachukia,+ na wakati wanawafukuza,+ na wanawalaumu, na kuharibu jina lenu kwa kusema ni kitu chenye uovu kwa sababu ya Mwana wa binadamu. 23  Mushangilie katika siku hiyo na kuruka kwa furaha, kwa maana muangalie! zawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana mambo yaleyale ndiyo mababu zao walikuwa wanatendea manabii.+ 24  “Lakini ole wenu ninyi matajiri,+ kwa maana munapata faraja yenu kikamili.+ 25  “Ole wenu ninyi wenye kushiba sasa, kwa maana mutakuwa na njaa. “Ole wenu ninyi wenye kucheka sasa, kwa maana mutaomboleza na kulia.+ 26  “Ole wenu wakati watu wote wanasema muzuri juu yenu,+ kwa maana ni vile mababu zao walitendea manabii wa uongo. 27  “Lakini ninawaambia ninyi wenye kusikiliza: Muendelee kupenda maadui wenu, kutendea mema wale wenye kuwachukia ninyi,+ 28  kubariki wale wenye kuwalaani ninyi, na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatukana ninyi.+ 29  Mutu mwenye anakupiga kwenye shavu moja, umugeuzie pia lile lingine; na mwenye anakamata nguo yako ya inje, usimukatalie pia nguo yako ya ndani.+ 30  Upatie kila mutu mwenye anakuomba,+ na mwenye anakamata vitu vyako, usimuombe akurudishie. 31  “Pia, kama vile munataka watu wawatendee ninyi, muwatendee kwa njia ileile.+ 32  “Kama munapenda wale wenye wanawapenda ninyi, hilo linawapatia ninyi sifa gani? Kwa maana hata watenda-zambi wanapenda wale wenye wanawapenda wao.+ 33  Na kama munatendea mema wale tu wenye wanawatendea ninyi mema, hilo linawapatia ninyi sifa gani? Hata watenda-zambi wanafanya vilevile. 34  Pia, kama munakopesha* wale wenye munatumaini watawalipa, hilo linawapatia ninyi sifa gani?+ Hata watenda-zambi wanakopesha watenda-zambi wenzao ili wawarudishie kiasi kilekile. 35  Tofauti na hilo, muendelee kupenda maadui wenu, kutenda mema, na kukopesha bila kutumaini kurudishiwa kitu chochote;+ na zawabu yenu itakuwa kubwa, na mutakuwa wana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, kwa maana yeye ni mwenye fazili kuelekea watu wenye hawana shukrani na waovu.+ 36  Muendelee kuwa wenye rehema, kama vile Baba yenu ni mwenye re­hema.+ 37  “Zaidi ya hayo, muache kuhukumu, na ninyi hamutahukumiwa hata kidogo;+ na muache kulaumu, na ninyi hamutalaumiwa hata kidogo. Muendelee kusamehe,* na ninyi mutasamehewa.*+ 38  Muzoee kupatia watu, na watu watawapatia ninyi.+ Watawamwangia katika mufuko wa nguo zenu kipimo kizuri, chenye kushindiliwa, chenye kutikiswa, na kujaa sana. Kwa maana kwa kipimo chenye munapimia watu, wao pia watawapimia ninyi.” 39  Kisha akawaambia pia mufano: “Kipofu anaweza kuongoza kipofu mwingine? Wote wawili hawataangukia katika shimo?+ 40  Mwanafunzi hamupite mwalimu wake, lakini kila mutu mwenye alifundishwa muzuri kabisa atakuwa kama mwalimu wake. 41  Basi, sababu gani unaangalia unyasi wenye kuwa katika jicho la ndugu yako lakini hauone kipande cha muti chenye kuwa katika jicho lako mwenyewe?+ 42  Namna gani unaweza kumuambia ndugu yako, ‘Ndugu, uniruhusu nitoshe unyasi wenye kuwa katika jicho lako mwenyewe,’ wakati wewe mwenyewe hauone kipande cha muti chenye kuwa katika jicho lako mwenyewe? Munafiki! Kwanza tosha kipande cha muti katika jicho lako, kisha utaona muzuri namna ya kutosha unyasi wenye kuwa katika jicho la ndugu yako. 43  “Kwa maana hakuna muti muzuri wenye unazaa matunda yenye kuoza, na hakuna muti wenye kuoza wenye unazaa matunda ya muzuri.+ 44  Kwa maana kila muti unajulikana kwa matunda yake.+ Kwa mufano, watu hawachume tini kwenye miiba, ao hawakate zabibu kwenye muti mudogo wa miiba. 45  Mutu muzuri anatosha mambo ya muzuri katika hazina ya muzuri ya moyo wake, lakini mutu muovu anatosha mambo maovu katika hazina yake ya mubaya; kwa maana kinywa chake kinasema mambo yenye kujaa katika moyo.+ 46  “Basi sababu gani munaniita ‘Bwana! Bwana!’ lakini hamufanye mambo yenye ninasema?+ 47  Kila mutu mwenye anakuja kwangu na kusikia maneno yangu kisha anayatenda, nitawaambia yeye anafanana na nani:+ 48  Anafanana na mutu mwenye wakati alijenga nyumba, alichimba na kushuka chini kabisa na akaweka musingi juu ya mwamba. Kisha, wakati mafuriko yalitokea, muto ukapiga nyumba hiyo lakini haukukuwa na nguvu ya kuitikisa, kwa maana ilikuwa imejengwa muzuri.+ 49  Kwa upande mwingine, mutu yeyote mwenye anasikia na hatende,+ ni kama mutu mwenye alijenga nyumba kwenye udongo bila musingi. Muto ukaipiga, na mara moja ikaanguka, na uharibifu wa nyumba hiyo ukakuwa mukubwa.”

Maelezo ya Chini

Ao “mikate ya wonyesho.”
Ao “kupooza.”
Ao “kupooza.”
Ao “nafsi.”
Ni kusema, kukopesha bila faida.
Ao “mutaachiliwa.”
Ao “kuachilia.”