Ufunuo kwa Yohana 5:1-14

  • Kitabu cha kukunjwa chenye mihuri saba (1-5)

  • Mwana-Kondoo anakamata kitabu cha kukunjwa (6-8)

  • Mwana-Kondoo anastahili kufungua mihuri (9-14)

5  Na nikaona katika mukono wa kuume wa Ule mwenye kukaa kwenye kile kiti cha ufalme,+ kitabu cha kukunjwa chenye kuandikwa pande zote mbili,* ­chenye kufungwa kabisa kwa mihuri saba (7).  Na nikaona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Ni nani mwenye anastahili kufungua kile kitabu cha kukunjwa na kuvunja mihuri yake?”  Lakini hakuna mutu yeyote mbinguni ao duniani ao chini ya dunia mwenye aliweza kufungua kile kitabu cha kukunjwa ao kuangalia ndani yake.  Nikalia sana kwa sababu hakuna mutu yeyote mwenye alipatikana mwenye alistahili kufungua kile kitabu cha kukunjwa ao kuangalia ndani yake.  Lakini mumoja wa wale wazee akaniambia: “Acha kulia. Angalia! Simba wa kabila la Yuda,+ muzizi+ wa Daudi,+ ameshinda+ ili afungue kile kitabu cha kukunjwa na mihuri yake saba (7).”  Na nikaona mwana-kondoo+ mwenye kuonekana kama vile amechinjwa,+ akiwa amesimama katikati ya kile kiti cha ufalme na ya vile viumbe ine (4) vyenye uzima na katikati ya wale wazee,+ akiwa na pembe saba (7) na macho saba, na macho hayo yanamaanisha zile roho saba za Mungu+ zenye zimetumwa katika dunia yote.  Mara moja akakuja na kukikamata kutoka katika mukono wa kuume wa Ule mwenye kukaa kwenye kile kiti cha ufalme.+  Wakati alikamata kile kitabu cha kukunjwa, vile viumbe ine (4) vyenye uzima na wale wazee makumi mbili na ine (24)+ wakaanguka chini mbele ya Mwana-Kondoo, na kila mumoja alikuwa na kinubi na mabakuli ya zahabu yenye kujaa uvumba. (Uvumba huo unamaanisha sala za watakatifu.)+  Na wanaimba wimbo mupya,+ wakisema: “Unastahili kukamata kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake, kwa maana ulichinjwa na kwa damu yako ukanunulia Mungu watu+ kutoka katika kila kabila na luga na watu na taifa,+ 10  na ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani kwa ajili ya Mungu wetu,+ na watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.” 11  Na nikaona, na nikasikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na vile viumbe vyenye uzima na wale wazee, na hesabu yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu na maelfu ya maelfu,+ 12  na walikuwa wanasema kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo mwenye alichinjwa+ anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”+ 13  Na nikasikia kila kiumbe chenye kuwa mbinguni na duniani na chini ya dunia+ na katika bahari, na vitu vyote vyenye kuwa ndani ya hivyo, vikisema: “Kwa Ule mwenye kukaa juu ya kile kiti cha ufalme+ na kwa Mwana-Kondoo+ kukuwe baraka na heshima+ na utukufu na nguvu milele na milele.”+ 14  Vile viumbe ine (4) vyenye uzima vilikuwa vinasema: “Amina!” na wale wazee wakaanguka chini na kuabudu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “upande wa ndani na wa inje.”