Ufunuo kwa Yohana 3:1-22

  • Ujumbe kwa kutaniko la Sardi (1-6), la Filadelfia (7-13), la Laodikia (14-22)

3  “Kwa malaika wa kutaniko lenye kuwa katika Sardi andika: Haya ndiyo mambo yenye anasema ule mwenye kuwa na zile roho saba (7) za Mungu+ na zile nyota saba:+ ‘Ninajua matendo yako, kwamba uko na jina* kwamba uko muzima, lakini umekufa.+  Ukuwe macho,+ na utie nguvu vitu vyenye vinabakia vyenye vilikuwa karibu kufa, kwa maana mimi sikuona kama kazi zako ­zilikuwa zimefanywa kwa ukamili* mbele ya Mungu wangu.  Kwa hiyo, endelea kufikiria* namna ulipokea na namna ulisikia, na uendelee kuchunga jambo hilo, na utubu.+ Hakika kama hauamuke, nitakuja kama mwizi,+ na hautajua hata kidogo saa yenye nitakuja juu yako.+  “‘Hata hivyo, uko na watu kidogo* katika Sardi wenye hawakuchafua nguo zao,+ na watatembea pamoja na mimi wakiwa wamevaa nguo nyeupe,+ kwa sababu wanastahili.  Kwa hiyo, ule mwenye atashinda+ atavaa nguo nyeupe,+ na sitafuta hata kidogo jina lake katika kitabu cha uzima,+ lakini nitakubali jina lake mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.+  Ule mwenye kuwa na sikio asikie mambo yenye roho inaambia makutaniko.’  “Kwa malaika wa kutaniko lenye kuwa katika Filadelfia andika: Haya ndiyo mambo yenye anasema ule mwenye kuwa mutakatifu,+ mwenye kuwa wa kweli,+ mwenye kuwa na funguo ya Daudi,+ mwenye anafungua hivi kwamba hakuna mutu mwenye atafunga na anafunga hivi kwamba hakuna mutu mwenye anafungua:  ‘Ninajua matendo yako—angalia! Nimeweka mbele yako mulango wenye kufunguliwa,+ wenye hakuna mutu anaweza kuufunga. Na ninajua kama uko na nguvu kidogo, na ulishika neno langu na haukukana jina langu.  Angalia! Nitafanya wale wa sinagogi la Shetani wenye wanasema ni Wayahudi hata kama hawako Wayahudi,+ lakini wanasema uongo—angalia! Nitawafanya wakuje na wainame mbele ya miguu yako na nitawafanya wajue kwamba nimekupenda wewe. 10  Kwa sababu ulishika neno juu ya uvumilivu wangu,*+ mimi pia nitakulinda katika ile saa ya jaribu+ yenye itakuja juu ya dunia yote yenye kuikaliwa na watu, ili kujaribu wale wenye wanakaa katika dunia. 11  Ninakuja mbio.+ Endelea kushika sana kile chenye uko nacho, ili mutu yeyote asichukue taji lako.+ 12  “‘Ule mwenye atashinda—nitamufanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka ndani hata kidogo, na nitaandika juu yake jina la Mungu wangu+ na jina la muji wa Mungu wangu, Yerusalemu Mupya+ wenye unashuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe la mupya.+ 13  Ule mwenye kuwa na sikio asikie mambo yenye roho inaambia makutaniko.’ 14  “Kwa malaika wa kutaniko lenye kuwa katika Laodikia+ andika: Haya ndiyo mambo yenye Amina+ anasema, shahidi+ muaminifu na wa kweli,+ mwanzo wa uumbaji wa Mungu:+ 15  ‘Ninajua matendo yako, kwamba wewe hauko baridi wala moto. Ningependa ukuwe baridi ao moto. 16  Basi kwa sababu wewe ni vuguvugu na hauko moto+ wala hauko baridi,+ nitakutapika kutoka katika kinywa changu. 17  Kwa sababu unasema, “Mimi ni tajiri,+ nimejipatia utajiri na sina lazima ya kitu chochote hata kidogo,” lakini haujue kwamba wewe ni mwenye taabu na wa kusikiliwa huruma na uko maskini na kipofu na uchi, 18  ninakushauri ununue kutoka kwangu zahabu yenye kusafishwa kwa moto ili ukuwe tajiri, na nguo nyeupe ili uvae na haya ya uchi wako isifunuliwe,+ na dawa ya macho ya kupakaa katika macho yako+ ili uweze kuona.+ 19  “‘Wale wote wenye ninapenda, ninawakaripia na kuwatia nizamu.+ Basi ukuwe mwenye bidii na utubu.+ 20  Angalia! Nimesimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu yeyote anasikia sauti yangu na kufungua mulango, nitaingia ndani ya nyumba yake na kula chakula cha mangaribi pamoja naye, na yeye pamoja na mimi. 21  Ule mwenye atashinda+ nitamupatia ruhusa ya kukaa pamoja na mimi kwenye kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilipata ushindi na nikakaa+ pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha ufalme. 22  Ule mwenye kuwa na sikio asikie mambo yenye roho inaambia makutaniko.’”

Maelezo ya Chini

Ao “unajulikana.”
Ao “zimekamilika.”
Ao “kukumbuka.”
Tnn., “majina kidogo.”
Ao pengine, “ulifuata mufano wa uvumilivu wangu.”