Ufunuo kwa Yohana 4:1-11

  • Maono ya kuwapo kwa Yehova mbinguni (1-11)

    • Yehova akiwa amekaa kwenye kiti chake cha ufalme (2)

    • Wazee makumi mbili na ine kwenye viti vya ufalme (4)

    • Viumbe ine vyenye uzima (6)

4  Kisha mambo hayo nikaona, na angalia! mulango wenye kufunguliwa mbinguni, na sauti ya kwanza yenye nilisikia ikisema na mimi ilikuwa kama tarumbeta, yenye kusema: “Panda ukuje huku, na nitakuonyesha mambo yenye yanapaswa kutendeka.”  Kisha mambo hayo mara moja nikakuwa katika nguvu za roho, na angalia! kiti cha ufalme kilikuwa mahali pake mbinguni, na mutu fulani alikuwa amekaa kwenye kile kiti cha ufalme.+  Na Ule mwenye kukaa alionekana kama jiwe la yaspi+ na jiwe nyekundu lenye samani, na kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa upinde wa mvua wenye kuonekana kama zumaridi.+  Kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa viti vya ufalme makumi mbili na ine (24), na kwenye vile viti vya ufalme niliona wazee makumi mbili na ine+ wamekaa wakiwa wamevaa nguo nyeupe, na juu ya vichwa vyao kulikuwa mataji ya zahabu.  Katika kile kiti cha ufalme kulikuwa kunatokea umeme wa radi+ na sauti na ngurumo za radi;+ na kulikuwa taa saba (7) za moto zenye kuwaka mbele ya kile kiti cha ufalme, na taa hizo zinamaanisha zile roho saba za Mungu.+  Mbele ya kile kiti cha ufalme kulikuwa kitu fulani chenye kufanana bahari ya kioo,+ kama fuwele. Katikati ya kile kiti cha ufalme* na kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa viumbe ine (4) vyenye uzima+ vyenye kujaa macho mbele na nyuma.  Kiumbe cha kwanza chenye uzima kilikuwa kama simba,+ na kiumbe cha pili chenye uzima kilikuwa kama ngombe-dume mudogo,+ na kiumbe cha tatu (3) chenye uzima+ kilikuwa na uso kama wa mwanadamu, na kiumbe cha ine (4) chenye uzima+ kilikuwa kama tai mwenye kuruka.+  Na vile viumbe ine (4) vyenye uzima, kila kimoja cha viumbe hivyo kilikuwa na mabawa sita (6); vilikuwa vimejaa macho kuvizunguka na chini yavyo.+ Na bila kuacha, muchana na usiku, vinasema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova*+ Mungu, Mweza-Yote, mwenye alikuwa na mwenye iko* na mwenye ana­kuja.”+  Kila wakati wenye vile viumbe vyenye uzima vinatoa utukufu na heshima na shukrani kwa Ule mwenye kukaa juu ya kile kiti cha ufalme, Ule mwenye kuishi milele na milele,+ 10  wale wazee makumi mbili na ine (24)+ wanaanguka chini mbele ya Ule mwenye kukaa juu ya kile kiti cha ufalme na wanamuabudu Ule mwenye kuishi milele na milele, na wanatupa mataji yao mbele ya kile kiti cha ufalme, wakisema: 11  “Unastahili, Yehova* Mungu wetu, kupokea utukufu+ na heshima+ na nguvu,+ kwa sababu uliumba vitu vyote,+ na kwa sababu ya mapenzi yako vilifikia kuwa na vikaumbwa.”

Maelezo ya Chini

Ao “Katikati pamoja na kile kiti cha ufalme.”
Ao “eko.”