Zaburi 36:1-12

  • Upendo mushikamanifu wa Mungu wenye samani

    • Muovu hamuogope Mungu (1)

    • Mungu ni chanzo cha uzima (9)

    • “Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza” (9)

Kwa kiongozi. Ya Daudi, mutumishi wa Yehova. 36  Kosa linazungumuza na muovu ndani kabisa ya moyo wake; Hakuna kumuogopa Mungu mbele ya macho yake.+   Kwa maana anajisifu-sifu sana mbele ya macho yake mwenyewe Ili asiweze kutambua kosa lake na kulichukia.+   Maneno ya kinywa chake yanaumiza na ni ya udanganyifu; Haonyeshe ufahamu wowote wa kutenda mambo ya muzuri.   Anafanya mipango yenye kuumiza hata katika kitanda chake. Anafuata njia yenye haiko ya muzuri; Hakatae mambo ya mubaya.   Ee Yehova, upendo wako mushikamanifu unafika mupaka mbinguni,+ Uaminifu wako mupaka kwenye mawingu.   Haki yako iko kama milima mikubwa;*+ Hukumu zako ni kama maji mengi yenye kuenda chini sana.+ Unalinda* mwanadamu na munyama, Ee Yehova.+   Upendo wako mushikamanifu ni wenye samani sana, Ee Mungu!+ Katika kivuli cha mabawa yako, Wana wa binadamu wanakimbilia.+   Wanakunywa na kushiba vitu vyenye kunona vya* nyumba yako,+ Na unawanywesha kwenye muto wa vitu vyako vyenye kufurahisha.+   Kwako kuko chemchemi ya uzima;+ Kupitia mwangaza wako tunaweza kuona mwangaza.+ 10  Endelea kuonyesha upendo wako mushikamanifu kwa wale wenye kukujua,+ Na haki yako, kwa wale wenye kuwa wanyoofu katika moyo.+ 11  Usiruhusu muguu wa mwenye majivuno unikanyange Wala mukono wa muovu unifukuze. 12  Wakosaji wameanguka kule; Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kama milima ya Mungu.”
Ao “Unaokoa.”
Tnn., “unono wa.”