Mika 5:1-15

  • Mutawala mwenye atakuwa mukubwa katika dunia yote (1-6)

    • Mutawala atatokea Betlehemu (2)

  • Mabaki watakuwa kama umande na kama simba (7-9)

  • Inchi itasafishwa (10-15)

5  “Sasa unajikata-kata, Ee binti mwenye kushambuliwa; Wametuzunguka kwa ajili ya vita.+ Wanamupiga muamuzi wa Israeli kwenye shavu kwa fimbo.+   Na wewe, Ee Betlehemu Efrata,+ Mwenye kuwa mudogo sana kati ya maelfu ya* Yuda, Mwenye atatawala katika Israeli kwa ajili yangu atatokea kwako,+ Asili yake ni ya kuanzia nyakati za zamani, kuanzia siku za zamani sana.   Kwa hiyo atatia watu wake katika mikono ya adui Mupaka wakati ule mama mwenye kuzaa atakuwa amezaa. Na ndugu zake wenye walibakia watarudia kwa watu wa Israeli.   Atasimama na kuchunga watu wake kwa nguvu ya Yehova,+ Katika ukubwa wa jina la Yehova Mungu wake. Na watakaa kwa usalama,+ Kwa maana sasa ukubwa wake utafika mupaka kwenye miisho ya dunia.+   Na ataleta amani.+ Kama Mwashuru atashambulia inchi yetu na kukanyanga minara yetu yenye ngome,+ Tutainua wachungaji saba (7) ili wapambane naye, ndiyo, wakubwa* munane (8) kutoka kati ya wanadamu.   Watachunga inchi ya Ashuru kwa upanga,+ Na inchi ya Nimrodi+ kwenye milango yake. Na atatuokoa kutoka kwa Mwashuru,+ Wakati atashambulia inchi yetu na kuingia katika eneo letu.   Na wenye walibakia wa Yakobo watakuwa katikati ya vikundi vingi vya watu Kama umande kutoka kwa Yehova, Kama matone ya mvua juu ya mimea Yenye hayamutumainie mutu Wala kungojea wana wa binadamu.   Na wenye walibakia wa Yakobo watakuwa kati ya mataifa, Katikati ya vikundi vingi vya watu, Kama simba kati ya wanyama wa pori, Kama mwana-simba* kati ya makundi ya kondoo, Mwenye anapita na kurukia na kupasua vipande-vipande; Na hakuna mwenye anaweza kuwaokoa.   Mukono wako utainuka juu ya wapinzani wako, Na maadui wako wote wataharibiwa.” 10  “Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema, “Nitaondoa farasi wenu katikati yenu na kuharibu magari yenu. 11  Nitaharibu miji ya inchi yenu Na kubomoa ngome zenu zote. 12  Nitakomesha ulozi wenye munafanya,* Na hakuna muchawi mwenye atabakia kati yenu.+ 13  Nitaharibu kutoka katikati yenu sanamu zenu za kuchongwa na nguzo zenu, Na hamutainamia tena kazi ya mikono yenu.+ 14  Nitangoa miti yenu mitakatifu*+ kutoka katikati yenu Na kuharibu miji yenu. 15  Kwa hasira na kasirani kali nitalipiza kisasi Juu ya mataifa yenye hayakutii.”

Maelezo ya Chini

Ao “ukoo mbalimbali wa.”
Ao “viongozi.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Tnn., “kutoka katika mukono wenu.”