Zaburi 37:1-40

  • Wenye kumutegemea Yehova watasitawi

    • Usikasirishwe na waovu (1)

    • “Pata furaha nyingi sana katika Yehova” (4)

    • “Tia njia yako katika mukono wa Yehova” (5)

    • “Wapole watariti dunia” (11)

    • Wenye haki hawatakosa mukate (25)

    • Wenye haki wataishi milele juu ya dunia (29)

Ya Daudi. א [Aleph] 37  Usikasirike* kwa sababu ya waovu Wala usisikilie wivu wakosaji.+   Watakauka haraka kama majani+ Na kufifia kama majani ya mupya ya mubichi. ב [Beth]   Umutegemee Yehova na utende mambo mema;+ Kaa katika dunia,* na utende kwa uaminifu.+   Pata furaha nyingi sana* katika Yehova, Naye atakutimizia tamaa za moyo wako. ג [Gimel]   Tia njia yako katika mukono wa* Yehova;+ Umutegemee yeye, naye atatenda kwa ajili yako.+   Atafanya haki yako ingae kama mwangaza wa asubui sana, Na haki yako kama jua la katikati ya muchana. ד [Daleth]   Nyamaza mbele ya Yehova+ Na umungojee kwa matumaini.* Usikasirishwe na mutu Mwenye anafanikiwa katika kutimiza mipango yake ya mubaya.+ ה [He]   Acha hasira na uache kasirani kali;+ Usikasirike na kuanza kutenda uovu.*   Kwa maana waovu wataharibiwa,+ Lakini wale wenye kumutumainia Yehova watariti dunia.+ ו [Waw] 10  Kunabakia wakati kidogo tu, waovu hawatakuwa tena;+ Utaangalia mahali walikuwa, Nao hawatakuwa pale.+ 11  Lakini wapole watariti dunia,+ Na watapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.+ ז [Zayin] 12  Mutu muovu anapanga mupango mubaya juu ya mwenye haki;+ Anamusagia meno yake. 13  Lakini Yehova atamucheka, Kwa maana Anajua kwamba siku yake itakuja.+ ח [Heth] 14  Waovu wanachomoa panga zao na kukunja* pinde zao Ili kumuangusha chini mwenye kukandamizwa na maskini, Ili kuchinja wale wenye njia yao imenyooka. 15  Lakini upanga wao utatoboa moyo wao wenyewe;+ Pinde zao zitavunjwa. ט [Teth] 16  Kidogo yenye mwenye haki iko* nayo ni muzuri Kuliko wingi wa vitu vyenye waovu wengi wako navyo.+ 17  Kwa maana mikono ya waovu itavunjwa, Lakini Yehova atategemeza wenye haki. י [Yod] 18  Yehova anajua mambo yenye watu wenye hawana lawama wanapambana nayo,* Na uriti wao utadumu milele.+ 19  Hawatapatishwa haya wakati wa musiba; Wakati wa njaa watakuwa na chakula kingi. כ [Kaph] 20  Lakini waovu wataangamia;+ Maadui wa Yehova wataisha kama vile malisho yenye utukufu; Wataisha kama moshi. ל [Lamed] 21  Muovu anakopa lakini halipe, Lakini mwenye haki ni mukarimu* na mwenye kutoa.+ 22  Wale wenye kubarikiwa Naye watariti dunia, Lakini wale wenye kulaaniwa Naye wataharibiwa.+ מ [Mem] 23  Yehova anaongoza* hatua za mutu+ Wakati Yeye anafurahia njia ya mutu huyo.+ 24  Hata kama anaanguka, hatatupwa chini,+ Kwa maana Yehova anamutegemeza kwa kumushika mukono.*+ נ [Nun] 25  Nilikuwa kijana na sasa nimezeeka, Lakini sijamuona mutu yeyote mwenye haki akiwa ameachwa,+ Wala watoto wake wakitafuta mukate.*+ 26  Sikuzote anakopesha bila kuomba faida,+ Na watoto wake watapata baraka. ס [Samekh] 27  Geuka na uache mambo ya mubaya na utende mambo ya muzuri,+ Na utaishi milele. 28  Kwa maana Yehova anapenda haki, Na hataacha washikamanifu wake.+ ע [Ayin] Watalindwa sikuzote;+ Lakini wazao wa waovu wataharibiwa.+ 29  Wenye haki watariti dunia,+ Na wataishi milele juu yake.+ פ [Pe] 30  Kinywa cha mwenye haki kinajulisha hekima,* Na ulimi wake unaongea kuhusu haki.+ 31  Sheria ya Mungu wake iko katika moyo wake;+ Hatua zake hazitayumba-yumba.+ צ [Tsade] 32  Muovu anamuangalia mwenye haki, Akitafuta kumuua. 33  Lakini Yehova hatamuacha katika mukono wa mutu huyo+ Wala hatamupata na hatia wakati atahukumiwa.+ ק [Qoph] 34  Tumainia Yehova na ufuate njia yake, Naye atakuinua ili uriti dunia. Wakati waovu wataharibiwa,+ utaona jambo hilo.+ ר [Resh] 35  Nimemuona mutu mwenye hana huruma, muovu Akienea kama muti wenye majani mengi katika udongo wake wa asili.+ 36  Lakini alikufa kwa kushitukia na hakukuwa tena;+ Niliendelea kumutafuta, na hangeweza kupatikana.+ ש [Shin] 37  Angalia mutu mwenye hana lawama,* Na uendelee kumuangalia munyoofu,+ Kwa maana wakati wenye kuja wa mutu huyo utakuwa wenye amani.+ 38  Lakini wakosaji wote wataharibiwa; Wakati wenye kuja wa watu waovu utakomeshwa.+ ת [Taw] 39  Wokovu wa wenye haki unatoka kwa Yehova;+ Yeye ndiye ngome yao wakati wa taabu.+ 40  Yehova atawasaidia na kuwaokoa.+ Atawaokoa kutoka kwa waovu na kuwakomboa, Kwa sababu wanamukimbilia yeye.+

Maelezo ya Chini

Ao “Usiwake kasirani.”
Ao “inchi.”
Ao “Pata shangwe kubwa sana.”
Tnn., “Viringisha njia yako juu ya.”
Ao “kwa uvumilivu.”
Ao pengine, “Usikasirike, kwa maana kasirani itakuongoza tu kwenye mambo yenye kuumiza.”
Ao “kutia kamba kwenye.”
Ao “eko.”
Tnn., “siku za watu wenye hawana lawama.”
Ao “ni mwenye kuonyesha wema.”
Ao “anafanya imara.”
Ao “kwa mukono Wake.”
Ao “chakula.”
Ao “kinazungumuza hekima kwa sauti ya chini.”
Ao “mutu mwenye kushika uaminifu-mushikamanifu.”