Kwa Waebrania 2:1-18

  • Kukaza uangalifu zaidi kuliko kawaida (1-4)

  • Vitu vyote vimetiishwa chini ya Yesu (5-9)

  • Yesu na ndugu zake (10-18)

    • Kiongozi Mukubwa wa wokovu wao (10)

    • Kuhani mukubwa mwenye rehema (17)

2  Hiyo ndiyo sababu ni lazima tukaze uangalifu zaidi kuliko kawaida juu ya mambo yenye tulisikia,+ ili tusipeperushwe mbali hata kidogo.+  Kwa maana kama neno lenye lilisemwa kupitia malaika+ lilikuwa hakika, na kila kosa na tendo la kukosa kutii lilipata azabu kupatana na haki,+  namna gani sisi tutaponyoka ikiwa tumepuuza wokovu huo mukubwa wa namna hiyo?+ Kwa maana ulianza kusemwa kupitia Bwana wetu+ na ulihakikishwa kwetu na wale wenye walimusikia,  wakati Mungu alijiunga katika kutoa ushahidi kwa alama na maajabu na matendo mbalimbali yenye nguvu+ na kwa roho takatifu yenye ilitolewa kulingana na mapenzi yake.+  Kwa maana haiko kwa malaika ndio ametiisha dunia yenye kuikaliwa na watu yenye kuja,+ yenye tunasema juu yake.  Lakini mahali fulani shahidi mumoja alisema: “Mwanadamu ni nini ili umuweke katika akili, ao mwana wa binadamu ili umuhangaikie?+  Ulimufanya mudogo kidogo kuliko malaika; ulimuvalisha taji la utukufu na heshima, na kumuweka juu ya kazi za mikono yako.  Ulitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Kwa kutiisha vitu vyote chini yake,+ Mungu hakuacha kitu chochote bila kukitiisha chini yake.+ Hata hivyo, sasa hatuone bado vitu vyote kuwa vimetiishwa chini yake.+  Lakini tunamuona Yesu, mwenye alifanywa kuwa mudogo kidogo kuliko malaika,+ sasa amevalishwa taji la utukufu na heshima kwa sababu alipatwa na kifo,+ ili kwa fazili zenye hazistahiliwe za Mungu aonje kifo kwa ajili ya kila mutu.+ 10  Kwa maana ilifaa kwamba ule mwenye kwa ajili yake na kupitia yeye vitu vyote viko, katika kuleta wana wengi kwenye utukufu,+ afanye Kiongozi Mukubwa wa wokovu wao+ kuwa mukamilifu kupitia mateso.+ 11  Kwa maana ule mwenye anatakasa na pia wale wenye wanatakaswa+ wote wanatokana na mumoja,+ na kwa sababu hiyo yeye hasikie haya kuwaita ndugu,+ 12  wakati anasema: “Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kutaniko nitakusifu kwa wimbo.”+ 13  Na tena: “Nitamutegemea yeye.”+ Na tena: “Angalia! Mimi na watoto wadogo, wenye Yehova* alinipatia.”+ 14  Basi, kwa kuwa “watoto wadogo” ni washiriki wa damu na mwili, vilevile yeye pia alishiriki mambo yaleyale,+ ili kupitia kifo chake aharibu ule mwenye kuwa na uwezo wa kutokeza kifo, ni kusema, Ibilisi,+ 15  na ili aweke huru* wale wote wenye walikuwa chini ya utumwa katika maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa kifo.+ 16  Kwa maana kwa kweli haiko malaika ndio anasaidia, lakini anasaidia uzao wa* Abrahamu.+ 17  Kwa hiyo alipaswa kuwa kama “ndugu” zake katika mambo yote,+ ili akuwe kuhani mukubwa mwenye rehema na muaminifu ­katika mambo yenye yanahusiana na Mungu, ili atoe zabihu ya kufunika zambi+ kwa ajili ya zambi za watu.+ 18  Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteseka wakati alijaribiwa,+ anaweza kusaidia wale wenye wanajari­biwa.+

Maelezo ya Chini

Ao “akomboe.”
Tnn., “mbegu ya.”