Kwa Waebrania 10:1-39

  • Zabihu za wanyama hazina uwezo (1-4)

    • Sheria ni kivuli (1)

  • Zabihu ya Kristo mara moja kwa wakati wote (5-18)

  • Njia mupya na yenye uzima ya kupitia (19-25)

    • Tusiache kukutana pamoja (24, 25)

  • Onyo juu ya zambi ya kimakusudi (26-31)

  • Uhakika na imani ili kuvumilia (32-39)

10  Kwa maana kwa kuwa Sheria iko na kivuli+ cha mambo ya muzuri yenye yatakuja,+ lakini hapana umbo ya kweli ya mambo hayo, haiwezi* hata kidogo, kwa zabihu zilezile zenye zinaendelea kutolewa mwaka kwa mwaka, kufanya wale wenye wanakaribia wakuwe wakamilifu.+  Tofauti na hilo, je, zabihu hazingeacha kutolewa, kwa sababu wale wenye wanatoa utumishi mutakatifu wangekuwa wametakaswa mara moja na hawangejisikia tena kuwa wako na zambi?  Kinyume cha hilo, zabihu hizo ni kikumbusho cha zambi mwaka kwa mwaka,+  kwa maana haiwezekane damu ya ngombe-dume na ya mbuzi kutosha zambi.  Basi wakati anakuja katika ulimwengu, anasema: “‘Haukutaka zabihu na toleo, lakini ulinitayarishia mwili.  Haukukubali matoleo mazima ya kuteketezwa na matoleo ya zambi.’+  Kisha nikasema: ‘Angalia! Nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu) ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.’”+  Kisha kusema kwanza: “Haukutaka na haukukubali zabihu na matoleo na matoleo mazima ya kuteketezwa na matoleo ya zambi”​—zabihu zenye zinatolewa kulingana na Sheria—  halafu anasema: “Angalia! Nimekuja ili kufanya mapenzi yako.”+ Anatosha ule mupango wa kwanza ili asimamishe ule wa pili. 10  Kwa “mapenzi” hayo+ sisi tumetakaswa kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.+ 11  Pia, kila kuhani anasimama mahali pake kila siku ili kutoa utumishi mutakatifu*+ na kutoa mara nyingi zabihu zilezile,+ zenye haziwezi kutosha kabisa zambi hata kidogo.+ 12  Lakini mutu huyu alitoa zabihu moja kwa ajili ya zambi mara moja kwa wakati wote na kukaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu,+ 13  tangu wakati huo na kuendelea akingojea mupaka maadui wake wawekwe kuwa kiti cha miguu yake.+ 14  Kwa maana ni kupitia toleo moja la zabihu ndiyo amefanya wale wenye wanatakaswa wakuwe wakamilifu+ kwa wakati wote. 15  Zaidi ya hayo, roho takatifu pia inatutolea ushahidi, kwa maana kisha kusema: 16  “‘Hili ndilo agano lenye nitafanya pamoja nao kisha siku hizo,’ ni vile Yehova* anasema. ‘Nitatia sheria zangu katika mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao.’”+ 17  Kisha inasema: “Na sitakumbuka tena zambi zao na matendo yao ya kuvunja sheria.”+ 18  Sasa mahali kwenye kuko musamaha wa mambo hayo, hakuna tena toleo kwa ajili ya zambi. 19  Kwa hiyo, ndugu, kwa kuwa hatuna woga* wa njia ya kuingia katika mahali patakatifu+ kupitia damu ya Yesu, 20  yenye alitufungulia* kuwa njia mupya na yenye uzima kupitia lile pazia,+ ni kusema, mwili wake, 21  na kwa kuwa tuko na kuhani mukubwa mwenye kuwa juu ya nyumba ya Mungu,+ 22  tukaribie tukiwa na mioyo myeupe na imani kamili, mioyo yetu ikiwa imenyunyiziwa* damu na kuwa safi kutokana na zamiri ya mubaya+ na miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.+ 23  Tushike imara tangazo la mbele ya watu wote la tumaini letu bila kuyumba-yumba,+ kwa maana ule mwenye aliahidi ni muaminifu. 24  Na tufikiriane* ili kuchocheana* katika upendo na matendo ya muzuri,+ 25  bila kuacha kukutana pamoja,+ kama vile wengine wako na desturi, lakini tutiane moyo,+ na kufanya vile zaidi sana kwa kadiri munaona siku ile kuwa inakaribia.+ 26  Kwa maana kama tunazoea kutenda zambi kimakusudi kisha kupokea ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli,*+ hakuna tena zabihu yoyote yenye inabakia kwa ajili ya zambi,+ 27  lakini kuko tazamio hakika la hukumu lenye linaogopesha na kasirani yenye kuwaka yenye itateketeza wale wenye wanapinga.+ 28  Mutu yeyote mwenye amezarau Sheria ya Musa anakufa bila huruma kwa ushuhuda wa watu wawili ao watatu (3).+ 29  Munawaza mutu mwenye amemukanyangia chini Mwana wa Mungu na kuona damu ya agano+ kuwa yenye samani ya kawaida tu, damu yenye alitakaswa kupitia hiyo, na mwenye ametukana kwa zarau roho ya fazili zenye hazistahiliwe, atapata azabu kubwa kadiri gani?+ 30  Kwa maana tunajua Ule mwenye alisema: “Kisasi ni changu; mimi nitalipa.” Na tena: “Yehova* atahukumu watu wake.”+ 31  Ni jambo lenye kuogopesha kuanguka katika mikono ya Mungu mwenye kuishi. 32  Hata hivyo, muendelee kukumbuka siku za zamani zenye, kisha kupata mwangaza,+ mulivumilia pigano kubwa pamoja na mateso. 33  Nyakati fulani mulifunuliwa mbele ya watu wote* kwa lawama na pia taabu, na nyakati fulani mulishiriki* pamoja na wale wenye walikuwa wanapatwa na jambo kama hilo. 34  Kwa maana muliwasikilia huruma wale wenye walikuwa katika gereza na mukakubali kwa furaha kunyanganywa vitu vyenu,+ mukijua kwamba ninyi wenyewe muko na malipo ya muzuri zaidi na yenye kudumu.+ 35  Kwa hiyo, musitupe hali yenu ya kutokuwa na woga,* yenye itapewa zawabu kwa wingi.+ 36  Kwa maana muko na lazima ya uvumilivu,+ ili kisha kufanya mapenzi ya Mungu, mupokee utimizo wa ile ahadi. 37  Kwa maana kunabakia “wakati kidogo sana,”+ na “ule mwenye anakuja atafika na hatakawia.”+ 38  “Lakini mutu wangu mwenye haki ataishi kwa sababu ya imani,”+ na “kama anarudia nyuma kwa kutetemeka, mimi sipendezwe* naye.”+ 39  Sasa sisi hatuko namna ya watu wenye wanarudia nyuma kwenye uharibifu,+ lakini sisi ni namna ya watu wenye wako na imani ili kulinda uzima wetu.*

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “watu hawawezi.”
Ao “kufanya utumishi wa watu wote.”
Ao “tuko na uhakika.”
Tnn., “alituzindulia.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “kutiana moyo.”
Ao “tuhangaikiane; tukaziane uangalifu.”
Ao “ujuzi sahihi wa ile kweli.”
Tnn., “mulifunuliwa kama katika jumba la maonyesho.”
Ao “mulisimama mumoja pembeni ya mwingine.”
Tnn., “uhuru wenu wa kusema.”
Ao “nafsi yangu haipendezwe.”
Ao “nafsi zetu.”