Kulingana na Luka 3:1-38

  • Mwanzo wa kazi ya Yohana (1, 2)

  • Yohana anahubiri ubatizo (3-20)

  • Yesu anabatizwa (21, 22)

  • Ukoo wa Yesu Kristo (23-38) (23-38)

3  Katika mwaka wa kumi na tano (15) wa utawala wa Kaisari Tiberio, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Yudea, Herode*+ alikuwa mutawala wa wilaya ya Galilaya, Filipo ndugu yake alikuwa mutawala wa wilaya ya inchi ya Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mutawala wa wilaya ya Abilene,  katika siku za kuhani mukubwa Anasi na za Kayafa,+ neno la Mungu likakuja kwa Yohana+ mwana wa Zekaria katika jangwa.+  Basi akaenda katika inchi yote yenye kuzunguka Yordani, akihubiri ubatizo wenye kuonyesha kutubu kwa ajili ya musamaha wa zambi,+  kama vile imeandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mutu mwenye kusema kwa sauti kubwa katika jangwa, ‘Mutayarishe njia ya Yehova!* Munyooshe barabara zake.+  Kila bonde linapaswa kujazwa, na kila mulima na kilima vinapaswa kufanywa kuwa tambarare; njia zenye kujikunja zinapaswa kunyooshwa, na njia zenye mikwaruzo zinapaswa kufanywa laini;  na miili yote itaona* wokovu wa Mungu.’”*+  Kwa hiyo, akaanza kuambia watu wengi wenye walikuwa wanakuja ili awabatize: “Ninyi wazao wa nyoka-vipiri, ni nani aliwaonya mukimbie kasirani kali yenye inakuja?+  Basi, muzae matunda yenye kuonyesha kwamba mumetubu. Musianze kusema katika mioyo yenu, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu anaweza kumuinulia Abrahamu ­watoto ­kutoka ­katika majiwe haya.  Kwa kweli, tayari shoka limewekwa kwenye muzizi wa miti. Basi, kila muti wenye hauzae matunda ya muzuri utakatwa na kutupwa katika moto.”+ 10  Na watu wengi walikuwa wanamuuliza: “Basi, tufanye nini?” 11  Akawajibu: “Mutu mwenye kuwa na nguo mbili* amupatie moja ule mwenye hana, na mutu mwenye kuwa na chakula afanye vilevile.”+ 12  Hata wakusanya-kodi wakakuja ili wabatizwe,+ na wakamuuliza: “Mwalimu, tufanye nini?” 13  Akawaambia: “Musiombe* jambo lolote zaidi ya kodi yenye iliwekwa.”+ 14  Pia, maaskari walikuwa wanamuuliza: “Tufanye nini?” Akawaambia: “Musimusumbue* mutu yeyote ao kumushitaki mutu yeyote kwa uongo,+ lakini mutosheke na posho yenu.”* 15  Sasa watu wote walikuwa wanangojea na wote walikuwa wanawaza katika mioyo yao, “Je, inawezekana huyu ndiye Kristo?”+ 16  Yohana akajibu, akiwaambia wote: “Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji, lakini ule mwenye nguvu kuliko mimi anakuja, na sistahili kufungua kamba za viatu vyake.+ Yeye atawabatiza ninyi kwa roho ­takatifu na kwa moto.+ 17  Kipao* chake cha kupepua kiko katika mukono wake ili kusafisha kabisa kiwanja chake cha kupigia-pigia nafaka, na kukusanya ngano yake katika depo yake, lakini maganda ya mbegu atayachoma kwa moto wenye hauwezi kuzimishwa.” 18  Pia, aliwachochea kwa maneno mengine mengi na akaendelea kutangazia watu habari njema. 19  Lakini Yohana alikuwa amemukaripia Herode mutawala wa wilaya, kwa sababu alimuoa Herodia bibi ya ndugu yake na kwa sababu ya matendo yote maovu yenye Herode alikuwa amefanya. 20  Na Herode akaongeza jambo hili kwenye matendo hayo yote: Akamufunga Yohana katika gereza.+ 21  Sasa wakati watu wote walikuwa wamebatizwa, Yesu pia akabatizwa.+ Wakati alikuwa anasali, mbingu ikafunguka,+ 22  na roho takatifu ikashuka juu yake katika umbo ya njiwa, na sauti ikatoka mbinguni: “Wewe ni Mwana wangu, mupendwa; nimekukubali.”+ 23  Wakati Yesu+ alianza kazi yake, alikuwa na miaka karibu makumi tatu (30).+ Na watu walimuona kuwa mwana,wa Yosefu,+mwana wa Heli, 24  mwana wa Matati,mwana wa Lawi,mwana wa Melki,mwana wa Yanai,mwana wa Yosefu, 25  mwana wa Matatia,mwana wa Amosi,mwana wa Nahumu,mwana wa Esli,mwana wa Nagai, 26  mwana wa Maati,mwana wa Matatia,mwana wa Semei,mwana wa Yoseki,mwana wa Yoda, 27  mwana wa Yoanani,mwana wa Resa,mwana wa Zerubabeli,+mwana wa Shealtieli,+mwana wa Neri, 28  mwana wa Melki,mwana wa Adi,mwana wa Kosamu,mwana wa Elmadamu,mwana wa Eri, 29  mwana wa Yesu,mwana wa Eliezeri,mwana wa Yorimu,mwana wa Matati,mwana wa Lawi, 30  mwana wa Simioni,mwana wa Yuda,mwana wa Yosefu,mwana wa Yonamu,mwana wa Eliakimu, 31  mwana wa Melea,mwana wa Mena,mwana wa Matata,mwana wa Natani,+mwana wa Daudi,+ 32  mwana wa Yese,+mwana wa Obedi,+mwana wa Boazi,+mwana wa Salmoni,+mwana wa Nashoni,+ 33  mwana wa Aminadabu,mwana wa Arni,mwana wa Hezroni,mwana wa Perezi,+mwana wa Yuda,+ 34  mwana wa Yakobo,+mwana wa Isaka,+mwana wa Abrahamu,+mwana wa Tera,+mwana wa Nahori,+ 35  mwana wa Serugi,+mwana wa Reu,+mwana wa Pelegi,+mwana wa Eberi,+mwana wa Shela,+ 36  mwana wa Kainani,mwana wa Arpakshadi,+mwana wa Shemu,+mwana wa Noa,+mwana wa Lameki,+ 37  mwana wa Metusela,+mwana wa Enoko,mwana wa Yaredi,+mwana wa Mahalaleeli,+mwana wa Kainani,+ 38  mwana wa Enoshi,+mwana wa Seti,+mwana wa Adamu,+mwana wa Mungu.

Maelezo ya Chini

Ni kusema, Herode Antipa. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “wanadamu wote wataona.”
Ao “njia ya Mungu ya kuokoa.”
Ao “nguo ingine.”
Ao “Musikusanye.”
Ao “Musimunyanganye.”
Ao “mishahara yenu.”
Ao “sepetu; bêche.”