Kutoka 6:1-30

  • Ahadi ya kuwekwa huru inarudiliwa (1-13)

    • Jina Yehova halikujulikana kwa ukamili (2, 3)

  • Ukoo wa Musa na Haruni (14-27)

  • Musa anapaswa kufika tena mbele ya Farao (28-30)

6  Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Sasa utaona mambo yenye nitamutendea Farao.+ Mukono wenye nguvu utamulazimisha aruhusu watu wangu waende, na mukono wenye nguvu utamulazimisha awafukuze mutoke katika inchi yake.”+  Kisha Mungu akamuambia Musa: “Mimi ni Yehova.  Nilikuwa ninamutokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo kama Mungu Mweza-Yote,+ lakini kuhusu jina langu Yehova+ sikujitambulisha kwao.+  Pia, nilifanya agano pamoja nao ili kuwapatia inchi ya Kanaani, inchi yenye waliishi ndani yake kama wageni.+  Sasa mimi mwenyewe nimesikia kilio cha maumivu cha watu wa Israeli, wenye Wamisri wako wanafanya kuwa watumwa, na ninakumbuka agano langu.+  “Kwa hiyo uambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, na nitawatosha chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa katika utumwa wao,+ na nitawakomboa kwa mukono wenye kunyooshwa* na kwa hukumu kubwa.+  Na nitawachukua kuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu,+ na hakika mutajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu mwenye anawatosha chini ya mizigo ya Misri.  Na nitawaingiza katika inchi yenye niliapa kwa kiapo* kwamba nitamupatia Abrahamu, Isaka, na Yakobo; na nitawapatia inchi hiyo ikuwe uriti wenu.+ Mimi ni Yehova.’”+  Kisha wakati fulani Musa akapatia Waisraeli ujumbe huo, lakini hawakumusikiliza Musa kwa sababu walikuwa wamevunjika moyo na kwa sababu ya utumwa mugumu.+ 10  Kisha Yehova akasema na Musa, na kumuambia: 11  “Ingia na umuambie Farao, mufalme wa Misri, kwamba anapaswa kuruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.” 12  Lakini Musa akamujibu Yehova: “Angalia! Waisraeli hawakunisikiliza;+ namna gani Farao atanisikiliza, mimi mwenye kuwa muzito wa kusema?”*+ 13  Lakini Yehova akamuambia tena Musa na Haruni amri za kupatia Waisraeli na Farao, mufalme wa Misri, ili kutosha Waisraeli katika inchi ya Misri. 14  Hawa ndio vichwa vya nyumba za baba zao: Wana wa Rubeni, muzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ Ni hizo zilikuwa familia za Rubeni. 15  Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, mwana wa mwanamuke Mukanaani.+ Ni hizo zilikuwa familia za Simeoni. 16  Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi,+ kulingana na vizazi vya familia zao: Gershoni, Kohati, na Merari.+ Lawi aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137). 17  Wana wa Gershoni walikuwa Libni na Shimei, kulingana na familia zao.+ 18  Wana wa Kohati walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+ Kohati aliishi miaka mia moja makumi tatu na tatu (133). 19  Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi. Ni hizo zilikuwa familia za Walawi, kulingana na vizazi vya familia zao.+ 20  Sasa Amramu alimuchukua Yokebedi, dada ya baba yake, akuwe bibi yake.+ Yokebedi akamuzalia Haruni na Musa.+ Amramu aliishi miaka mia moja makumi tatu na saba (137). 21  Wana wa Ishari walikuwa Kora,+ Nefegi, na Zikri. 22  Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elsafani,+ na Sitri. 23  Sasa Haruni akamuchukua Elisheba, binti ya Aminadabu, dada ya Nashoni,+ akuwe bibi yake. Akamuzalia Nadabu, Abihu, Eleazari, na Itamari.+ 24  Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elkana, na Abiasafu.+ Ni hizo zilikuwa familia za Wakora.+ 25  Eleazari+ mwana wa Haruni, alichukua mumoja wa mabinti wa Putieli akuwe bibi yake. Akamuzalia Finehasi.+ Hao ndio vichwa vya jamaa za upande wa baba za Walawi, kulingana na familia zao.+ 26  Huyu ndiye Haruni na Musa wenye Yehova aliambia: “Mutoshe watu wa Israeli katika inchi ya Misri, vikundi-vikundi.”*+ 27  Ni wao walisema na Farao, mufalme wa Misri, atoshe watu wa Israeli katika Misri. Ilikuwa huyu Musa na huyu Haruni.+ 28  Katika siku hiyo wakati Yehova alisema na Musa katika inchi ya Misri, 29  Yehova akamuambia Musa: “Mimi ni Yehova. Umuambie Farao, mufalme wa Misri, kila jambo lenye ninakuambia.” 30  Kisha Musa akasema mbele ya Yehova: “Angalia! Niko muzito wa kusema,* kwa hiyo namna gani Farao atanisikiliza?”+

Maelezo ya Chini

Ao “wenye nguvu.”
Tnn., “niliinua mukono wangu.”
Tnn., “sijatahiriwa midomo?”
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “sijatahiriwa midomo.”