Kutoka 23:1-33

  • Maamuzi ya hukumu kwa ajili ya Israeli (1-19)

    • Kuhusu unyoofu na mwenendo muzuri (1-9)

    • Kuhusu sabato na sikukuu mbalimbali (10-19)

  • Malaika anaongoza Israeli (20-26)

  • Kukamata inchi na mipaka ya inchi hiyo (27-33)

23  “Haupaswe kueneza habari za uongo.+ Usishirikiane na mutu muovu kwa kutoa ushahidi wenye utaumiza wengine.+  Haupaswe kufuata watu wengi ili kutenda maovu, na haupaswe kupotosha haki kwa kutoa ushahidi ili kuunga mukono watu wengi.*  Haupaswe kuonyesha upendeleo katika mabishano ya mutu maskini.+  “Kama unakutana na ngombe-dume ao punda wa adui yako mwenye amepotea, unapaswa kumurudisha kwake.+  Kama punda wa mutu mwenye anakuchukia ameanguka chini ya muzigo wake, haupaswe kujifanya kama haumuone punda huyo na kuenda. Unapaswa kumusaidia kufungua munyama huyo.+  “Haupaswe kupotosha hukumu ya maskini kati yenu katika kesi yake ya kuhukumu.+  “Ujiepushe na mashitaka ya* uongo, na usimuue mutu mwenye hana kosa na mwenye haki, kwa maana sitamutangaza mutu muovu kuwa mwenye haki.*+  “Haupaswe kukubali rushwa,* kwa maana rushwa* inapofusha wenye hekima na inaweza kupotosha maneno ya wenye haki.+  “Haupaswe kumukandamiza mukaaji mugeni. Munajua namna mutu anajisikia wakati iko* mukaaji mugeni,* kwa sababu mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+ 10  “Kwa miaka sita (6) utapanda mbegu katika shamba lako na kuvuna mazao yake.+ 11  Lakini mwaka wa saba (7) utaliacha bila kulilima na utaliacha lipumuzike, na maskini wenye kuwa kati ya watu wako watakula chakula cha shamba hilo, na kile wataacha, kitakuliwa na wanyama wa pori. Ni vile utafanyia shamba lako la mizabibu na shamba lako la mizeituni. 12  “Utafanya kazi zako kwa siku sita (6); lakini siku ya saba (7), utaacha kufanya kazi zako, ili ngombe-dume wako na punda wako wapumuzike na mwana wa mutumwa wako mwanamuke na mukaaji mugeni wapate nguvu mupya.+ 13  “Munapaswa kuwa waangalifu ili kufanya mambo yote yenye nimewaambia,+ na hamupaswe kutaja majina ya miungu mingine; hayapaswe kusikika kwenye midomo yenu.*+ 14  “Mara tatu (3) kwa mwaka utanifanyia sikukuu.+ 15  Utafanya Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu.+ Utakula mikate yenye haina chachu kwa siku saba (7), kama vile nimekuamuru, kwa wakati wenye uliwekwa katika mwezi wa Abibu,*+ kwa maana kwa wakati huo ulitoka Misri. Mutu yeyote asionekane mbele yangu mikono wazi.+ 16  Pia, utafanya Sikukuu ya Mavuno* ya matunda ya kwanza yenye kukomaa ya kazi zako, na ya vitu vyenye unapanda katika mashamba;+ na Sikukuu ya Kukusanya* kwenye mwisho wa mwaka, wakati unakusanya katika shamba mazao ya kazi zako.+ 17  Mara tatu (3) kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele ya Bwana wa kweli, Yehova.+ 18  “Haupaswe kutoa damu ya zabihu yangu pamoja na kila kitu chenye kuwa na chachu. Na zabihu za mafuta zenye zinatolewa kwenye sikukuu zangu hazipaswe kuachwa usiku wote mupaka asubui. 19  “Utaleta katika nyumba ya Yehova Mungu wako matunda ya kwanza ya muzuri zaidi yenye kukomaa ya udongo wako.+ “Haupaswe kutokotesha mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+ 20  “Ninamutuma malaika mbele yenu+ ili akulinde katika safari na kukuingiza mahali kwenye nimetayarisha.+ 21  Umusikilize, na utii sauti yake. Usimuasi, kwa maana hatasamehe makosa yako,+ kwa sababu jina langu liko ndani yake. 22  Lakini, kama unatii kabisa sauti yake na kufanya mambo yote yenye ninasema, nitaonyesha maadui wako uadui na nitapinga wale wenye kukupinga. 23  Kwa maana malaika wangu ataenda mbele yako na atakupeleka kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi, na Wayebusi, na mimi nitawaharibu.+ 24  Haupaswe kuinamia miungu yao wala kushawishiwa kuitumikia, na haupaswe kuiga matendo yao.+ Lakini, unapaswa kuharibu sanamu zao na kuvunja-vunja nguzo zao takatifu.+ 25  Munapaswa kumutumikia Yehova Mungu wenu,+ naye atabariki mukate wako na maji yako.+ Nitaondoa magonjwa kati yako.+ 26  Mimba ya wanamuke katika inchi yako haitaharibika wala hawatakuwa tasa,+ na nitakupatia maisha ya murefu.* 27  “Nitatuma woga wangu mbele yako,+ na nitavuruga watu wote wenye utakutana nao, na nitafanya maadui wako wote washindwe na kukimbia.+ 28  Nitatuma hisia ya kuvunjika moyo* mbele yako,+ na itawakimbiza Wahivi, Wakanaani, na Wahiti mbele yako.+ 29  Sitawafukuza watoke mbele yako katika mwaka mumoja, ili inchi isikuwe ukiwa na ili wanyama wa pori wasiongezeke na kukushambulia.+ 30  Nitawafukuza hatua kwa hatua watoke mbele yako, mupaka uzae na kuongezeka na kuriti ile inchi.+ 31  “Nitaweka mupaka wako kuanzia Bahari Nyekundu kufikia bahari ya Wafilisti na kuanzia jangwa kufikia ule Muto;*+ kwa maana nitatia wakaaji wa inchi hiyo katika mukono wako, na utawafukuza watoke mbele yako.+ 32  Haupaswe kufanya agano pamoja nao wala pamoja na miungu yao.+ 33  Hawapaswe kuishi katika inchi yako, ili wasikufanye unitendee zambi. Kama unatumikia miungu yao, hakika jambo hilo litakuwa mutego kwako.”+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, ushahidi wenye kupendwa na watu wengi.
Tnn., “neno la.”
Ao “sitamutangaza kuwa hana kosa.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “eko.”
Ao “munajua maisha (nafsi) ya mukaaji mugeni.”
Tnn., “kinywa chenu.”
Inaitwa pia Sikukuu ya Vibanda (Tabenakulo).
Inaitwa pia Sikukuu ya Majuma, ao Pentekoste.
Ao “nitafanya siku zako zikuwe nyingi.”
Ao pengine, “wasiwasi; woga mukubwa.”
Ni kusema, Efrati.