Barua kwa Wakolosai 3:1-25

  • Utu wa zamani na utu mupya (1-17)

    • Muue viungo vya mwili (5)

    • Upendo, kifungo kikamilifu cha umoja (14)

  • Mashauri kwa familia za Kikristo (18-25)

3  Hata hivyo, kama mulifufuliwa pamoja na Kristo,+ muendelee kutafuta mambo yenye kuwa juu, kwenye Kristo amekaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu.+  Muendelee kukaza akili zenu juu ya mambo yenye kuwa juu,+ hapana juu ya mambo yenye kuwa katika dunia.+  Kwa maana mulikufa, na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika umoja na Mungu.  Wakati Kristo, ambaye ni uzima wetu,+ atafunuliwa, basi ninyi pia mutafunuliwa pamoja naye katika utukufu.+  Kwa hiyo, muue viungo vya mwili wenu+ vyenye kuwa katika dunia kuhusiana na uasherati,* uchafu, tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe,+ tamaa yenye kuumiza, na pupa, yenye kuwa ibada ya sanamu.  Kwa sababu ya mambo hayo kasirani kali ya Mungu inakuja.  Ni vile ninyi pia mulikuwa munajiendesha* katika maisha yenu ya zamani.*+  Lakini sasa, kwa kweli, munapaswa kuondoa mambo haya yote kutoka kwenu: kasirani kali, hasira, ubaya,+ matukano,+ na maneno machafu+ kutoka katika kinywa chenu.  Musiambiane uongo.+ Muvue utu* wa zamani+ pamoja na mazoea yake, 10  na muvae utu mupya,+ wenye kupitia ujuzi wenye hauna makosa* unafanywa kuwa mupya kulingana na mufano wa Ule mwenye aliuumba,+ 11  kwenye hakuna Mugiriki ao Muyahudi, kutahiriwa ao kutokutahiriwa, mugeni, Musikite,* mutumwa, ao mutu huru; lakini Kristo ni kila kitu na iko* katika vitu vyote.+ 12  Basi, kama wachaguliwa wa Mungu,+ watakatifu na wapendwa, muvae upendo wenye upole* wa huruma,+ fazili, unyenyekevu,*+ upole,+ na uvumilivu.+ 13  Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda+ hata kama mutu yeyote iko* na sababu ya kulalamika juu ya mwingine.+ Kama vile Yehova* aliwasamehe ninyi kwa kupenda, ninyi pia munapaswa kufanya vilevile.+ 14  Lakini zaidi ya mambo haya yote, muvae upendo,+ kwa maana upendo ni kifungo kikamilifu cha umoja.+ 15  Pia, amani ya Kristo itawale katika mioyo yenu,*+ kwa maana muliitwa kwenye amani hiyo katika mwili mumoja. Na mujionyeshe kuwa wenye shukrani. 16  Neno la Kristo likae ndani yenu kwa wingi katika hekima yote. Muendelee kufundishana na kutiana moyo* kwa zaburi,+ sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho zenye zinaimbwa kwa shukrani,* mukimuimbia Yehova* katika mioyo yenu.+ 17  Jambo lolote lenye munafanya kwa neno ao kwa tendo, mufanye mambo yote katika jina la Bwana Yesu, mukimushukuru Mungu Baba kupitia yeye.+ 18  Ninyi bibi, mujitiishe kwa bwana zenu,+ kwa kuwa inafaa katika Bwana. 19  Ninyi bwana, muendelee kupenda bibi zenu+ na musiwakasirikie kwa uchungu.*+ 20  Ninyi watoto, mutii wazazi wenu katika kila jambo,+ kwa maana hilo linamupendeza Bwana. 21  Ninyi baba, musikuwe munakasirisha* watoto wenu,+ ili wasivunjike moyo. 22  Ninyi watumwa, mutii katika kila jambo wale wenye kuwa mabwana wenu wanadamu,*+ haiko tu wakati wanaangalia, ili tu kupendeza wanadamu,* lakini kwa moyo muzuri, kwa kumuogopa Yehova.* 23  Jambo lolote lenye munafanya, mulifanye kwa nafsi* yote kama kwa ajili ya Yehova,*+ na hapana kwa ajili ya wanadamu, 24  kwa maana munajua kwamba mutapokea kutoka kwa Yehova* uriti kama zawabu.+ Mumutumikie Bwana, Kristo. 25  Hakika ule mwenye anafanya kosa atapokea malipo kwa lile kosa lenye amefanya,+ na hakuna ubaguzi wowote.+

Maelezo ya Chini

Neno la Kigiriki por·neiʹa. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mulikuwa munatembea.”
Ao “wakati muliishi vile.”
Tnn., “mutu.”
Ao “sahihi.”
Neno “Musikite” lilitumiwa ili kutaja mushenzi.
Ao “eko.”
Ao “unyenyekevu wa akili.”
Ao “upendo mwororo.”
Ao “eko.”
Ao “iongoze mioyo yenu.”
Ao “kuonyana.”
Ao “neema.”
Ao “musikuwe wakali kwao.”
Ao “musikuwe munachokoza; musikuwe munasumbua.”
Tnn., “kwa njia ya kimwili.”
Tnn., “hapana kwa matendo ya utumishi wa macho, kama watu wenye kupendeza wanadamu.”