Barua kwa Wakolosai 1:1-29

  • 1 Salamu (1, 2)

  • Shukrani kwa sababu ya imani ya Wakolosai (3-8)

  • Sala kwa ajili ya kukomaa kiroho (9-12)

  • Daraka la maana la Kristo (13-23)

  • Kazi ya bidii ya Paulo kwa ajili ya kutaniko (24-29)

1  Paulo, mutume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, na Timoteo+ ndugu yetu,  kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika umoja na Kristo wenye kuwa Kolosai: Mukuwe na fazili zenye hazistahiliwe na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.  Sikuzote tunamushukuru Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunasali kwa ajili yenu,  kwa kuwa tulisikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na upendo wenye muko nao kwa watakatifu wote  kwa sababu ya tumaini lenye linawekwa kwa ajili yenu mbinguni.+ Pale mwanzo, mulisikia juu ya tumaini hili kupitia ujumbe wa kweli ya habari njema  wenye umekuja kwenu. Kama vile habari njema inazaa matunda na kuongezeka katika ulimwengu wote,+ ni vile pia inafanya katikati yenu tangu siku mulisikia na kujua kwa njia yenye haina makosa* fazili zenye hazistahiliwe za Mungu katika kweli.  Ni vile mumejifunza kutoka kwa mutumwa mwenzetu mupendwa Epafra,+ mutumishi muaminifu wa Kristo kwa ajili yetu.  Alitujulisha pia upendo wenu katika njia ya kiroho.*  Hiyo ndiyo sababu pia tangu siku tulisikia juu ya jambo hilo, hatujaacha hata kidogo kusali kwa ajili yenu+ na kuomba mujazwe ujuzi wenye hauna makosa*+ wa mapenzi yake katika hekima yote na uelewaji wa kiroho,+ 10  na hivyo mutembee kwa namna yenye kumustahili Yehova* ili kumupendeza kwa ukamili wakati uleule mukiendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema na kuongezeka katika ujuzi wenye hauna makosa* wa Mungu;+ 11  na mufanywe kuwa imara kwa nguvu zote kulingana na uwezo wake wenye utukufu+ ili muvumilie kwa ukamili kwa subira na furaha, 12  wakati uleule mukimushukuru Baba, mwenye alifanya mustahili kushiriki uriti wa watakatifu+ katika mwangaza. 13  Alituokoa kutoka katika mamlaka ya giza+ na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa, 14  mwenye kupitia yeye tunaachiliwa huru kupitia bei ya ukombozi, kusamehewa zambi zetu.+ 15  Yeye ni mufano wa Mungu mwenye haonekane,+ muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote;+ 16  kwa sababu kupitia yeye vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vyenye kuonekana na vitu vyenye havionekane,+ ikuwe ni viti vya ufalme ao utawala ao serikali ao mamlaka. Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia yeye+ na kwa ajili yake. 17  Pia, yeye ni wa mbele ya vitu vingine vyote,+ na kupitia yeye vitu vingine vyote vilifanywa vikuwe, 18  na yeye ni kichwa cha mwili, kutaniko.+ Yeye ni mwanzo, muzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,+ ili akuwe ndiye wa kwanza katika mambo yote; 19  kwa sababu Mungu alipenda ujazo wote ukae ndani yake,+ 20  na kupitia yeye apatanishe vitu vingine vyote pamoja naye mwenyewe+ kwa kufanya amani kupitia damu+ yenye alimwanga kwenye muti wa mateso,* ikuwe ni vitu vyenye kuwa duniani ao vitu vyenye kuwa mbinguni. 21  Kwa kweli, ninyi wenye zamani mulikuwa mumetengwa na mulikuwa maadui kwa sababu akili zenu zilikuwa zinafikiria matendo maovu, 22  sasa amewapatanisha kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake, ili awatoe ninyi mukiwa watakatifu na bila kasoro na bila shitaka lolote mbele yake+ 23  kama tu, kwa kweli, munaendelea katika imani,+ mukiwa mumewekwa imara juu ya musingi+ na kubakia bila kutikisika,+ bila kuondolewa kwenye tumaini la ile habari njema yenye mulisikia na yenye ilihubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.+ Mimi Paulo, nimekuwa mutumishi wa hii habari njema.+ 24  Sasa ninafurahi katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ na ninapata taabu za Kristo zenye zingali zinakosa katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake,+ ambao ni kutaniko.+ 25  Nilikuja kuwa mutumishi wa kutaniko hili kupatana na usimamizi-nyumba+ kutoka kwa Mungu wenye nilipewa kwa ajili yenu ili kuhubiri neno la Mungu kwa ukamili, 26  siri takatifu+ yenye ilikuwa imefichwa tangu mipangilio ya mambo*+ yenye ilipita na tangu vizazi vyenye vilipita. Lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake,+ 27  wenye Mungu amependezwa kuwajulisha katikati ya mataifa utajiri wenye utukufu wa siri hii takatifu,+ ambayo ni Kristo katika umoja na ninyi, tumaini la utukufu wake.+ 28  Yeye ndiye tunatangaza, kwa kuonya kila mutu na kufundisha kila mutu katika hekima yote, ili tutoe kila mutu akiwa kamili katika umoja na Kristo.+ 29  Kwa kusudi hili kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikaza kwa uwezo wake wenye unatenda kwa nguvu ndani yangu.+

Maelezo ya Chini

Ao “kwa usahihi.”
Tnn., “katika roho.”
Ao “sahihi.”
Ao “sahihi.”
Ao “mifumo ya mambo.” Angalia Maana ya Maneno.