Kwa Wagalatia 3:1-29

  • Tofauti kati ya matendo ya Sheria na imani (1-14)

    • Mwenye haki ataishi kwa imani (11)

  • Ahadi kwa Abrahamu haikukuwa kupitia Sheria (15-18)

    • Kristo, uzao wa Abrahamu (16)

  • Chanzo na kusudi la Sheria (19-25)

  • Wana wa Mungu kupitia imani (26-29)

    • Wazao wa Abrahamu, wale wenye kuwa wa Kristo (29)

3  Ninyi Wagalatia wenye kukosa akili! Ni nani mwenye aliwaleta chini ya uvutano huu muovu,+ ninyi wenye Yesu Kristo alionyeshwa mbele yenu waziwazi akiwa amepigiliwa misumari kwenye muti?+  Ninataka kuwauliza* jambo hili moja: Mulipokea roho kupitia matendo ya sheria ao kwa sababu ya kuamini mambo yenye mulisikia?+  Je, ninyi hamuna akili kabisa? Mulianza katika mwendo wa kiroho,* na je, munamalizia katika mwendo wa kimwili?*+  Je, mulipatwa na mateso mengi sana bila sababu? Kama kwa kweli ilikuwa bila sababu.  Kwa hiyo, je, ule mwenye anawapatia ninyi roho na kufanya matendo yenye nguvu+ katikati yenu, anafanya vile kwa sababu ya matendo yenu ya sheria ao kwa sababu munaamini mambo yenye mulisikia?  Kama vile Abrahamu “alikuwa na imani katika Yehova,* na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”+  Kwa kweli munajua kwamba ni wale wenye kushikamana na imani ndio wana wa Abrahamu.+  Sasa kwa kuwa andiko liliona mbele ya wakati kwamba Mungu angetangaza watu wa mataifa kuwa wenye haki kupitia imani, lilitangaza habari njema mbele ya wakati kwa Abrahamu, ni kusema: “Kupitia wewe mataifa yote yatabarikiwa.”+  Basi wale wenye kushikamana na imani wanabarikiwa pamoja na Abrahamu, mwenye alikuwa na imani.+ 10  Wale wote wenye wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana, kwa maana imeandikwa: “Amelaaniwa kila mutu mwenye habakie katika mambo yote yenye yaliandikwa katika kitabu cha kukunjwa cha Sheria kwa kuyatenda.”+ 11  Zaidi ya hayo, ni wazi kwamba kupitia sheria hakuna mutu mwenye anatangazwa kuwa mwenye haki mbele ya macho ya Mungu,+ kwa maana “mwenye haki ataishi kwa sababu ya imani.”+ 12  Sasa Sheria haitegemee imani. Lakini, “mutu yeyote mwenye anafanya mambo hayo ataishi kupitia hayo.”+ 13  Kristo alitununua,+ akatuweka huru+ kutoka katika laana ya Sheria kwa kuwa laana pa nafasi yetu, kwa sababu imeandikwa: “Amelaaniwa kila mutu mwenye ametundikwa kwenye muti.”+ 14  Ilikuwa vile ili baraka ya Abrahamu ikuje kwa mataifa kupitia Kristo Yesu,+ ili tupokee roho yenye iliahidiwa+ kupitia imani yetu. 15  Ndugu, ninasema kwa kutumia mufano wa mwanadamu: Wakati tu agano linakubaliwa, hata kama linakubaliwa na mwanadamu, hakuna mutu mwenye analifuta ao kuliongezea mambo mengine. 16  Sasa ahadi zilitolewa kwa Abrahamu na kwa uzao wake.*+ Andiko haliseme, “na kwa wazao wako,”* kama vile ni kwa wengi. Lakini, linasema, “na kwa uzao wako,”* kama vile ni kwa mumoja, ambaye ni Kristo.+ 17  Zaidi ya hayo, ninasema hivi: Sheria yenye ilitokea miaka mia ine makumi tatu (430) kisha pale,+ haivunje agano lenye lilifanywa na Mungu pale mwanzo, na kwa hiyo haifute ahadi. 18  Kwa maana kama uriti unategemea sheria, hautegemee tena ahadi; lakini Mungu amemupatia Abrahamu uriti kwa fazili kupitia ahadi.+ 19  Basi, sababu gani Sheria? Iliongezwa ili kufanya makosa yakuwe wazi,+ mupaka uzao ufike+ wenye ulikuwa umepewa* ahadi; na ilipitishwa kupitia malaika+ kwa mukono wa mupatanishi.+ 20  Sasa hakuna mupatanishi wakati mutu mumoja tu ndiye anahusika, lakini Mungu ni mumoja tu. 21  Kwa hiyo, je, Sheria inapinga ahadi za Mungu? Hapana kabisa! Kwa maana kama sheria yenye inaweza kuleta uzima ingetolewa, kwa kweli haki ingekuwa kupitia sheria. 22  Lakini Andiko liliweka mambo yote katika kifungo cha zambi, ili ahadi yenye inatokana na imani katika Yesu Kristo ipewe wale wenye kuamini. 23  Hata hivyo, mbele ya imani kufika, tulikuwa tunalindwa chini ya sheria, tukiwekwa katika kifungo, tukitazamia imani yenye ilikuwa karibu kufunuliwa.+ 24  Basi Sheria imekuwa mulinzi* wetu mwenye kutuongoza kwa Kristo,+ ili tutangazwe kuwa wenye haki kupitia imani.+ 25  Lakini sasa kwa kuwa imani imefika,+ hatuko tena chini ya mulinzi* huyo.+ 26  Kwa kweli, ninyi wote ni wana wa Mungu+ kupitia imani yenu katika Kristo Yesu.+ 27  Kwa maana ninyi wote wenye mulibatizwa katika Kristo mumevaa Kristo.+ 28  Hakuna Muyahudi ao Mugiriki,+ hakuna mutumwa ao mutu huru,+ hakuna mwanaume ao mwanamuke,+ kwa maana ninyi wote ni kitu kimoja katika umoja na Kristo Yesu.+ 29  Zaidi ya hayo, kama ninyi ni wa Kristo, ninyi kwa kweli ni uzao wa* Abrahamu,+ wariti+ kuhusiana na ahadi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kujifunza kutoka kwenu.”
Tnn., “mulianza katika roho.”
Tnn., “munakamilishwa katika mwili?”
Tnn., “mbegu yako.”
Tnn., “mbegu zako.”
Tnn., “mbegu yake.”
Ao “mbegu ifike yenye ilikuwa imepewa.”
Ao “mulezi.”
Ao “mulezi.”
Tnn., “mbegu ya.”