Muhubiri 3:1-22

  • Kila jambo liko na wakati wake wenye umewekwa (1-8)

  • Kufurahia maisha ni zawadi kutoka kwa Mungu (9-15)

    • Umilele uko katika moyo wa mwanadamu (11)

  • Mungu anahukumu watu wote kwa haki (16, 17)

  • Wanadamu na wanyama wote wanafikia kufa (18-22)

    • Wote watarudia katika mavumbi (20)

3  Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa,Kila kazi chini ya mbingu iko na wakati wake:   Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;Wakati wa kupanda na wakati wa kungoa kitu chenye kilipandwa;   Wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha;Wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;   Wakati wa kulia na wakati wa kucheka;Wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza;*   Wakati wa kutupa majiwe na wakati wa kukusanya majiwe;Wakati wa kukumbatia na wakati wa kujizuia kukumbatia;   Wakati wa kutafuta na wakati wa kuacha kutafuta chenye kimepotea;Wakati wa kulinda na wakati wa kutupa;   Wakati wa kupasua+ na wakati wa kushona,Wakati wa kunyamaza+ na wakati wa kusema;+   Wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;+Wakati wa vita na wakati wa amani.  Mufanyakazi anapata faida gani kwa bidii yake yote?+ 10  Nimeona kazi yenye Mungu amepatia wana wa binadamu wafanye. 11  Amefanya kila kitu kuwa kizuri* kwa wakati wake.+ Hata ametia umilele katika moyo wao; lakini wanadamu hawatavumbua hata siku moja kazi yenye Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mupaka mwisho. 12  Nimeona kwamba hakuna jambo la muzuri zaidi kwao kuliko kufurahi na kufanya mema wakati wa maisha yao,+ 13  na kwamba kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.+ 14  Nimefikia kujua kwamba kila kitu chenye Mungu wa kweli anafanya kitadumu milele. Hakuna chenye kinaweza kuongezwa wala kupunguzwa juu ya hicho. Mungu wa kweli amefanya mambo yakuwe vile, ili watu wamuogope.+ 15  Kila kitu chenye kinatokea kimekwisha kutokea, na kile kitakuja kimekwisha kuwa;+ lakini Mungu wa kweli anatafuta kile kimekuwa kikifuatiliwa.* 16  Tena nimeona hili chini ya jua: Mahali pa haki palikuwa uovu, na mahali pa uadilifu* palikuwa uovu.+ 17  Basi nikasema katika moyo wangu: “Mungu wa kweli atahukumu wenye haki na waovu,+ kwa maana kila kazi na kila jambo liko na wakati wake.” 18  Pia nikasema katika moyo wangu kuhusu wana wa binadamu kwamba Mungu wa kweli atawajaribu na kuwaonyesha kwamba wako kama wanyama, 19  kwa maana kuko jambo moja lenye linapata* wanadamu na jambo moja lenye linapata wanyama; wote wanapatwa na jambo lilelile.+ Namna mumoja anakufa, ni vile mwingine anakufa; na wote wako na roho ileile.+ Kwa hiyo mwanadamu hashindie wanyama, kwa sababu kila kitu ni bure.* 20  Wote wanaenda mahali palepale.+ Wote wanatoka katika mavumbi,+ na wote wanarudia katika mavumbi.+ 21  Ni nani kabisa anajua kama roho ya wanadamu inapanda juu, na kama roho ya wanyama inashuka kwenye udongo?+ 22  Na niliona kwamba hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kuliko kufurahia kazi yake,+ kwa sababu hiyo ndiyo zawabu yake,* kwa maana ni nani anaweza kumuonyesha mambo yenye yatatokea kisha yeye kufa?+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kuruka-ruka.”
Ao “chenye kupangwa muzuri; chenye kufaa.”
Ao pengine, “chenye kimepita.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mwisho mumoja wenye unapata.”
Ao “ubatili.”
Ao “fungu lake.”