Kulingana na Marko 12:1-44

  • Mufano wa walimaji wauaji (1-12)

  • Mungu na Kaisari (13-17)

  • Ulizo juu ya ufufuo (18-27)

  • Amri mbili kubwa zaidi (28-34)

  • Je, Kristo ni mwana wa Daudi? (35-37a)

  • Onyo juu ya waandishi (37b-40)

  • Feza mbili za kichele za mujane maskini (41-44)

12  Kisha akaanza kusema nao kwa kutumia mifano: “Mutu fulani alipanda shamba la mizabibu+ na kulizungushia ukuta, akachimba shimo kwa ajili ya kikamulio cha divai na akasimamisha munara;+ kisha akalikodisha kwa walimaji na akasafiri kuenda katika inchi ya kigeni.+  Wakati kipindi chake kilifika akatuma mutumwa kwa walimaji ili akusanye kutoka kwao sehemu fulani ya matunda ya shamba la mizabibu.  Lakini wakamukamata, wakamupiga, na wakamufukuza mikono wazi.  Tena akatuma mutumwa mwingine kwao, na huyo wakamupiga kwenye kichwa na kumukosea heshima.+  Na akatuma mwingine, na huyo wakamuua, na wengine wengi, wamoja wao wakawapiga na wengine wakawaua.  Mutu mumoja mwenye alibakia naye alikuwa mwana wake mupendwa.+ Akamutuma wa mwisho, akisema: ‘Watamuheshimia mwana wangu.’  Lakini wale walimaji wakaambiana, ‘Huyu ndiye muriti.+ Mukuje, tumuue, na uriti utakuwa wetu.’  Basi wakamukamata na kumuua, na wakamutupa inje ya shamba la mizabibu.+  Ule mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Atakuja na kuua wale walimaji na kupatia wengine shamba hilo la mizabibu.+ 10  Je, hamujasoma hata siku moja andiko hili: ‘Jiwe lenye wajenzi walikataa ndilo limekuwa jiwe kubwa la pembe.*+ 11  Hili limetoka kwa Yehova,* na ni la ajabu mbele ya macho yetu’?”+ 12  Halafu wakataka kumukamata, lakini waliogopa watu, kwa maana walijua kwamba alisema mufano huo juu yao. Kwa hiyo wakamuacha na kuenda.+ 13  Kisha wakamutumia Wafarisayo fulani na wafuasi fulani wa chama cha Herode ili wamunase katika maneno yake.+ 14  Wakati walifika, wakamuambia: “Mwalimu, tunajua kwamba wewe unasema kweli sikuzote na hautafute kukubaliwa na mutu yeyote, kwa maana hauangalie namna watu wanaonekana kwa inje, lakini unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli. Je, inaruhusiwa* kulipa Kaisari kodi ya kichwa ao hapana? 15  Je, tunapaswa kulipa, ao hatupaswe kulipa?” Akijua unafiki wao, akawaambia: “Sababu gani munanijaribu? Muniletee dinari* niiangalie.” 16  Wakaleta dinari moja, na Yesu akawaambia: “Sura hii na mwandiko huu ni vya nani?” Wakamuambia: “Ni vya Kaisari.” 17  Kisha Yesu akasema: “Mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari,+ lakini Mungu vitu vya Mungu.”+ Na wakashangazwa na maneno yake. 18  Sasa Wasadukayo, wenye wanasema hakuna ufufuo,+ wakakuja na kumuuliza:+ 19  “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama ndugu ya mutu anakufa na anamuacha bibi lakini haache mutoto, ndugu yake anapaswa kumuchukua bibi huyo na kumuinulia ndugu yake uzao.+ 20  Kulikuwa ndugu saba (7). Wa kwanza akaoa mwanamuke, lakini wakati alikufa hakuacha uzao wowote. 21  Na wa pili akamuoa, lakini akakufa bila kuacha uzao, na wa tatu (3) vilevile. 22  Na wote saba (7) hawakuacha uzao. Mwishowe, ule mwanamuke naye akakufa. 23  Wakati wa ufufuo, ule mwanamuke atakuwa bibi ya nani? Kwa maana alikuwa bibi ya wote saba (7).” 24  Yesu akawaambia: “Munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu.+ 25  Kwa maana wakati wanafufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoe na wanamuke hawaolewe, lakini wao ni kama malaika wa mbinguni.+ 26  Hata hivyo, kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamukusoma katika kitabu cha Musa, katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, kwamba Mungu alimuambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?+ 27  Yeye haiko Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wazima. Mumekosea sana.”+ 28  Mumoja kati ya waandishi mwenye alikuwa amekuja na kusikia wanabishana, akijua kwamba alikuwa amewajibu muzuri, akamuuliza: “Ni amri gani ndiyo ya kwanza* kati ya zote?”+ 29  Yesu akajibu: “Ya kwanza ni hii, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova* Mungu wetu ni Yehova* mumoja, 30  na unapaswa kumupenda Yehova* Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’+ 31  Ya pili ni hii, ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’+ Hakuna amri ingine yenye kuwa kubwa zaidi kuliko hizi.” 32  Ule mwandishi akamuambia: “Mwalimu, umesema muzuri kupatana na kweli, ‘Yeye ni Mumoja, na hakuna mwingine isipokuwa yeye’;+ 33  na mutu kumupenda kwa moyo wake wote, na kwa uelewaji wake wote, na kwa nguvu zake zote, na pia kumupenda jirani yake kama yeye mwenyewe ni muzuri sana kuliko matoleo yote mazima ya kuteketezwa na zabihu.”+ 34  Halafu Yesu, wakati alitambua kwamba amejibu kwa hekima, akamuambia: “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.” Lakini hakuna mutu mwenye aliweza tena kumuuliza ulizo.+ 35  Hata hivyo, wakati Yesu aliendelea kufundisha katika hekalu, alisema: “Sababu gani waandishi wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?+ 36  Kupitia roho takatifu,+ Daudi mwenyewe alisema, ‘Yehova* alimuambia Bwana wangu: “Kaa kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niweke maadui wako chini ya miguu yako.”’+ 37  Daudi mwenyewe anamuita Bwana, basi namna gani anaweza kuwa mwana wake?”+ Na watu wengi sana walikuwa wanamusikiliza kwa furaha. 38  Na katika mafundisho yake akaendelea kusema: “Mufanye angalisho na waandishi wenye wanapenda kutembea-tembea wakiwa wamevaa kanzu na wanapenda salamu katika masoko+ 39  na kukaa kwenye viti vya mbele* katika masinagogi, na wanapenda nafasi za heshima zaidi kwenye chakula cha mangaribi.+ 40  Wanameza nyumba za* wajane, na ili kujionyesha,* wanatoa sala za murefu. Hao watapokea hukumu kali* zaidi.” 41  Kisha akakaa akiangalia masanduku ya hazina,+ na akaanza kuangalia namna wale watu wengi walikuwa wanatumbukiza feza ndani ya masanduku ya hazina, na matajiri wengi walikuwa wanatumbukiza ndani feza nyingi za vichele.+ 42  Sasa, mujane fulani maskini akakuja na kutumbukiza ndani feza mbili za vichele zenye samani kidogo sana.*+ 43  Basi akaita wanafunzi wake na kuwaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, mujane huyu maskini ametoa zaidi ya wote wenye walitia feza ndani ya masanduku ya hazina.+ 44  Kwa sababu wote walitumbukiza ndani kutokana na wingi wa feza zao, lakini yeye, hata kama ni maskini,* alitumbukiza ndani kila kitu chenye alikuwa nacho, yote yenye alikuwa nayo ili kuishi.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kichwa cha pembe.”
Ao “ni sawa.”
Ao “ya maana zaidi.”
Ao “vya muzuri zaidi.”
Ao “vitu vya.”
Ao “kwa kisingizio.”
Ao “nzito.”
Tnn., “leptoni mbili, zenye ni kwadrani moja.” Angalia Nyongeza B14.
Ao “mwenye uhitaji.”