Isaya 43:1-28

  • Yehova anakusanya tena watu wake (1-7)

  • Miungu inajaribiwa (8-13)

    • “Muko mashahidi wangu” (10, 12)

  • Kukombolewa kutoka Babiloni (14-21)

  • “Tuende pamoja kwenye tribinali” (22-28)

43  Sasa Yehova,Muumbaji wako, Ee Yakobo, Ule mwenye alikuumba, Ee Israeli, anasema hivi:+ “Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+ Nimekuita kwa jina lako. Wewe ni wangu.   Wakati unapita katika maji, nitakuwa pamoja na wewe;+Na wakati unapita katika mito, haitakuzamisha.+ Wakati unatembea katika moto, hautaungua,Wala mwali wa moto hautakuchoma.   Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako,Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Nimetoa Misri kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yako,Etiopia na Seba pa nafasi yako.   Kwa sababu ulikuwa mwenye samani mbele ya macho yangu,+Uliheshimiwa, na nimekupenda.+ Basi nitatoa watu pa nafasi yakoNa mataifa pa nafasi ya uzima wako.*   Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.+ Nitaleta uzao wako* kutoka masharikiNa kukukusanya pamoja kutoka mangaribi.+   Nitaambia kaskazini, ‘Uwatoe!’+ Na kusini, ‘Usiwazuie. Leta watoto wangu wanaume kutoka mbali, na watoto wangu wanamuke kutoka miisho ya dunia,+   Kila mutu mwenye kuitwa kwa jina langu+Na mwenye niliumba kwa ajili ya utukufu wangu,Mwenye nimefanya na kumutengeneza.’+   Mulete watu wenye kuwa vipofu, hata kama wako na macho,Na wenye kuwa viziwi, hata kama wako na masikio.+   Mataifa yote yakusanyike mahali pamoja,Na vikundi vya watu vikusanyike pamoja.+ Ni nani kati yao anaweza kutangaza jambo hili? Ao, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?*+ Walete mashahidi wao ili kuonyesha kwamba wanasema kweli,Ao wasikie na kusema, ‘Ni kweli!’”+ 10  “Muko mashahidi wangu,”+ ni vile Yehova anasema,“Ndiyo, mutumishi wangu mwenye nimechagua,+Ili mujue na kuniamini,*Na muelewe kwamba mimi ni uleule.+ Mbele yangu hapakukuwa Mungu mwenye alifanyizwa,Na kisha mimi hakujakuwa mwingine.+ 11  Mimi—mimi ni Yehova,+ na hakuna mwokozi isipokuwa mimi.”+ 12  “Mimi Ndiye nilitangaza na kuokoa na kujulisha,Wakati hapakukuwa mungu yeyote wa kigeni kati yenu.+ Basi muko mashahidi wangu,” ni vile Yehova anasema, “na mimi ni Mungu.+ 13  Pia, mimi ni uleule sikuzote;+Na hakuna mwenye anaweza kunyanganya kitu chochote katika mukono wangu.+ Wakati ninatenda, ni nani anaweza kunizuia?”+ 14  Yehova, Mukombozi wenu,+ Mutakatifu wa Israeli,+ anasema hivi: “Nitatuma ujumbe kule Babiloni kwa ajili yenu na kushusha mapingo* yote ya milango mikubwa,+Na Wakaldayo, katika mashua* zao, watalia kwa taabu.+ 15  Mimi ni Yehova Mutakatifu wenu,+ Muumbaji wa Israeli,+ Mufalme wenu.”+ 16  Yehova anasema hivi,Yeye mwenye kufanya njia katika bahariNa njia hata katika maji yenye musukosuko,+ 17  Yeye mwenye kutoa gari la vita na farasi,+ Jeshi pamoja na wapiganaji-vita wenye nguvu: “Watalala chini na hawataamuka.+ Watazimwa, watazimishwa kama utambi wenye kuwaka.” 18  “Musikumbuke mambo ya kwanza,Na musiendelee kufikiria mambo ya zamani. 19  Angalia! Ninafanya jambo la mupya;+Hata sasa linatokea. Je, hamulitambue? Nitafanya njia katika jangwa,+Na mito katika jangwa.+ 20  Munyama wa pori ataniheshimia,Mbweha na mbuni,Kwa maana nitatokeza maji katika jangwa,Mito katika jangwa,+Ili watu wangu, muchaguliwa wangu,+ wakunywe, 21  Watu wenye nimejifanyiaIli watangaze sifa yangu.+ 22  Lakini haujaniitia, Ee Yakobo,+Kwa sababu umenichoka, Ee Israeli.+ 23  Haukuniletea kondoo kwa ajili ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa,Wala haukunitukuza kwa zabihu zako. Sikukulazimisha uniletee zawadi, Wala sikukuchokesha kwa kukuomba ubani.+ 24  Haukuninunulia kane tamu* kwa feza zako,Na haukunitosheleza kwa mafuta ya zabihu zako.+ Lakini, umenilemea kupitia zambi zako;Na kunichokesha kupitia makosa yako.+ 25  Mimi, mimi Ndiye ninafuta makosa yako*+ kwa ajili yangu mwenyewe,+Na sitakumbuka zambi zako.+ 26  Unikumbushe; kila mumoja wetu alete shitaka lake juu ya mwenzake;Ujieleze ili kuonyesha kwamba uko na haki. 27  Babu yako wa kwanza alitenda zambi,Na wasemaji* wako mwenyewe wameniasi.+ 28  Kwa hiyo nitachafua wakubwa wa mahali patakatifu,Na nitamutoa Yakobo ili aharibiweNa kumufanya Israeli atukanwe.+

Maelezo ya Chini

Ao “nafsi yako.”
Tnn., “mbegu yako.”
Pengine ni mambo ya kwanza yenye yatatokea wakati wenye kuja.
Ao “kunitumainia.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Kane ni utete wenye harufu ya muzuri.
Ao “matendo yako ya uasi.”
Pengine ni walimu wa Sheria.