Isaya 43:1-28
43 Sasa Yehova,Muumbaji wako, Ee Yakobo, Ule mwenye alikuumba, Ee Israeli, anasema hivi:+
“Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+
Nimekuita kwa jina lako.
Wewe ni wangu.
2 Wakati unapita katika maji, nitakuwa pamoja na wewe;+Na wakati unapita katika mito, haitakuzamisha.+
Wakati unatembea katika moto, hautaungua,Wala mwali wa moto hautakuchoma.
3 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako,Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wako.
Nimetoa Misri kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yako,Etiopia na Seba pa nafasi yako.
4 Kwa sababu ulikuwa mwenye samani mbele ya macho yangu,+Uliheshimiwa, na nimekupenda.+
Basi nitatoa watu pa nafasi yakoNa mataifa pa nafasi ya uzima wako.*
5 Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe.+
Nitaleta uzao wako* kutoka masharikiNa kukukusanya pamoja kutoka mangaribi.+
6 Nitaambia kaskazini, ‘Uwatoe!’+
Na kusini, ‘Usiwazuie.
Leta watoto wangu wanaume kutoka mbali, na watoto wangu wanamuke kutoka miisho ya dunia,+
7 Kila mutu mwenye kuitwa kwa jina langu+Na mwenye niliumba kwa ajili ya utukufu wangu,Mwenye nimefanya na kumutengeneza.’+
8 Mulete watu wenye kuwa vipofu, hata kama wako na macho,Na wenye kuwa viziwi, hata kama wako na masikio.+
9 Mataifa yote yakusanyike mahali pamoja,Na vikundi vya watu vikusanyike pamoja.+
Ni nani kati yao anaweza kutangaza jambo hili?
Ao, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?*+
Walete mashahidi wao ili kuonyesha kwamba wanasema kweli,Ao wasikie na kusema, ‘Ni kweli!’”+
10 “Muko mashahidi wangu,”+ ni vile Yehova anasema,“Ndiyo, mutumishi wangu mwenye nimechagua,+Ili mujue na kuniamini,*Na muelewe kwamba mimi ni uleule.+
Mbele yangu hapakukuwa Mungu mwenye alifanyizwa,Na kisha mimi hakujakuwa mwingine.+
11 Mimi—mimi ni Yehova,+ na hakuna mwokozi isipokuwa mimi.”+
12 “Mimi Ndiye nilitangaza na kuokoa na kujulisha,Wakati hapakukuwa mungu yeyote wa kigeni kati yenu.+
Basi muko mashahidi wangu,” ni vile Yehova anasema, “na mimi ni Mungu.+
13 Pia, mimi ni uleule sikuzote;+Na hakuna mwenye anaweza kunyanganya kitu chochote katika mukono wangu.+
Wakati ninatenda, ni nani anaweza kunizuia?”+
14 Yehova, Mukombozi wenu,+ Mutakatifu wa Israeli,+ anasema hivi:
“Nitatuma ujumbe kule Babiloni kwa ajili yenu na kushusha mapingo* yote ya milango mikubwa,+Na Wakaldayo, katika mashua* zao, watalia kwa taabu.+
15 Mimi ni Yehova Mutakatifu wenu,+ Muumbaji wa Israeli,+ Mufalme wenu.”+
16 Yehova anasema hivi,Yeye mwenye kufanya njia katika bahariNa njia hata katika maji yenye musukosuko,+
17 Yeye mwenye kutoa gari la vita na farasi,+
Jeshi pamoja na wapiganaji-vita wenye nguvu:
“Watalala chini na hawataamuka.+
Watazimwa, watazimishwa kama utambi wenye kuwaka.”
18 “Musikumbuke mambo ya kwanza,Na musiendelee kufikiria mambo ya zamani.
19 Angalia! Ninafanya jambo la mupya;+Hata sasa linatokea.
Je, hamulitambue?
Nitafanya njia katika jangwa,+Na mito katika jangwa.+
20 Munyama wa pori ataniheshimia,Mbweha na mbuni,Kwa maana nitatokeza maji katika jangwa,Mito katika jangwa,+Ili watu wangu, muchaguliwa wangu,+ wakunywe,
21 Watu wenye nimejifanyiaIli watangaze sifa yangu.+
22 Lakini haujaniitia, Ee Yakobo,+Kwa sababu umenichoka, Ee Israeli.+
23 Haukuniletea kondoo kwa ajili ya matoleo yako mazima ya kuteketezwa,Wala haukunitukuza kwa zabihu zako.
Sikukulazimisha uniletee zawadi,
Wala sikukuchokesha kwa kukuomba ubani.+
24 Haukuninunulia kane tamu* kwa feza zako,Na haukunitosheleza kwa mafuta ya zabihu zako.+
Lakini, umenilemea kupitia zambi zako;Na kunichokesha kupitia makosa yako.+
25 Mimi, mimi Ndiye ninafuta makosa yako*+ kwa ajili yangu mwenyewe,+Na sitakumbuka zambi zako.+
26 Unikumbushe; kila mumoja wetu alete shitaka lake juu ya mwenzake;Ujieleze ili kuonyesha kwamba uko na haki.
27 Babu yako wa kwanza alitenda zambi,Na wasemaji* wako mwenyewe wameniasi.+
28 Kwa hiyo nitachafua wakubwa wa mahali patakatifu,Na nitamutoa Yakobo ili aharibiweNa kumufanya Israeli atukanwe.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “nafsi yako.”
^ Tnn., “mbegu yako.”
^ Pengine ni mambo ya kwanza yenye yatatokea wakati wenye kuja.
^ Ao “kunitumainia.”
^ Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
^ Ao “mashua za maji; bateaux.”
^ Kane ni utete wenye harufu ya muzuri.
^ Ao “matendo yako ya uasi.”
^ Pengine ni walimu wa Sheria.