Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kitabu cha Isaya

Sura

Habari Zenye Kuwa Ndani

  • 1

    • Baba na wana wake waasi (1-9)

    • Yehova anachukia ibada ya kidesturi (10-17)

    • “Tunyooshe mambo” (18-20)

    • Sayuni itarudishwa kuwa muji muaminifu (21-31)

  • 2

    • Mulima wa Yehova unainuliwa (1-5)

      • Mikuki inakuwa miundu (4)

    • Siku ya Yehova inashusha wenye majivuno (6-22)

  • 3

    • Viongozi wa Yuda wanapotosha watu (1-15)

    • Mabinti wa Sayuni wenye tabia ya kutongoza wanahukumiwa (16-26)

  • 4

    • Wanamuke saba kwa mwanaume mumoja (1)

    • Kile chenye Yehova anachipusha kitakuwa chenye utukufu (2-6)

  • 5

    • Wimbo kuhusu shamba la Yehova la mizabibu (1-7)

    • Ole kwa shamba la Yehova la mizabibu (8-24)

    • Kasirani ya Mungu juu ya watu wake (25-30)

  • 6

    • Katika maono, Isaya anamuona Yehova katika hekalu lake (1-4)

      • “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yehova” (3)

    • Midomo ya Isaya inasafishwa (5-7)

    • Isaya anatumwa (8-10)

      • “Mimi huyu! Unitume mimi!” (8)

    • “Mupaka wakati gani, Ee Yehova?” (11-13)

  • 7

    • Ujumbe kwa Mufalme Ahazi (1-9)

      • Shear-yashubu (3)

    • Alama ya Emanueli (10-17)

    • Matokeo ya kukosa uaminifu (18-25)

  • 8

    • Shambulizi lenye kuja la Ashuru (1-8)

      • Maher-shalal-hash-bazi (1-4)

    • Usiogope—“Mungu iko pamoja na sisi!” (9-17)

    • Isaya na watoto wake ni alama (18)

    • Mutafute habari katika sheria, hapana kwa pepo wachafu (19-22)

  • 9

    • Mwangaza mukubwa kwa ajili ya inchi ya Galilaya (1-7)

      • “Mukubwa wa Amani” anazaliwa (6-7)

    • Mukono wa Mungu unashambulia Israeli (8-21)

  • 10

    • Mukono wa Mungu unashambulia Israeli (1-4)

    • Ashuru—​Fimbo ya kasirani ya Mungu (5-11)

    • Ashuru anapewa azabu (12-19)

    • Mabaki wa Yakobo watarudia (20-27)

    • Mungu atahukumu Ashuru (28-34)

  • 11

    • Utawala wenye haki wa tawi la Yese (1-10)

      • Imbwa wa pori na mwana-kondoo wanakaa pamoja (6)

      • Dunia itajaa ujuzi juu ya Yehova (9)

    • Mabaki wanarudishwa (11-16)

  • 12

    • Wimbo wa shukrani (1-6)

      • “Yah Yehova ni nguvu zangu” (2)

  • 13

    • Tangazo juu ya Babiloni (1-22)

      • Siku ya Yehova iko karibu! (6)

      • Wamedi wataangusha Babiloni (17)

      • Babiloni haitaikaliwa na watu hata siku moja (20)

  • 14

    • Israeli watakaa kwenye inchi yao (1, 2)

    • Maneno ya kumuchokoza mufalme wa Babiloni (3-23)

      • Mwenye kungaa ataanguka kutoka mbinguni (12)

    • Mukono wa Yehova utamuponda Mwashuru (24-27)

    • Tangazo juu ya Ufilisti (28-32)

  • 15

    • Tangazo juu ya Moabu (1-9)

  • 16

    • Ujumbe juu ya Moabu unaendelea (1-14)

  • 17

    • Tangazo juu ya Damasko (1-11)

    • Mataifa yatakemewa na Yehova (12-14)

  • 18

    • Ujumbe juu ya Etiopia (1-7)

  • 19

    • Tangazo juu ya Misri (1-15)

    • Misri itafikia kumujua Yehova (16-25)

      • Mazabahu kwa ajili ya Yehova kule Misri (19)

  • 20

    • Alama juu ya Misri na Etiopia (1-6)

  • 21

    • Tangazo juu ya jangwa la bahari (1-10)

      • Kuendelea kulinda kwenye munara wa mulinzi (8)

      • “Babiloni ameanguka!” (9)

    • Tangazo juu ya Duma na jangwa tambarare (11-17)

      • “Mulinzi, habari gani za usiku?” (11)

  • 22

    • Tangazo kuhusu Bonde la Maono (1-14)

    • Eliakimu anakuwa musimamizi-nyumba pa nafasi ya Shebna (15-25)

      • Kipande kidogo cha muti cha mufano (23-25)

  • 23

    • Tangazo juu ya Tiro (1-18)

  • 24

    • Yehova atafanya inchi ibakie bila kitu (1-23)

      • Yehova ni Mufalme katika Sayuni (23)

  • 25

    • Baraka nyingi juu ya watu wa Mungu (1-12)

      • Karamu ya Yehova ya divai ya muzuri (6)

      • Kifo hakitakuwa tena (8)

  • 26

    • Wimbo kuhusu tumaini na wokovu (1-21)

      • Yah Yehova, Mwamba wa milele (4)

      • Watu wa dunia watajifunza haki (9)

      • “Wafu wako wataishi” (19)

      • Muingie katika vyumba vya ndani na mujifiche (20)

  • 27

    • Yehova anaua Leviatani (1)

    • Wimbo kuhusu Israeli akiwa shamba la mizabibu (2-13)

  • 28

    • Ole wao walevi wa Efraimu! (1-6)

    • Makuhani na manabii wa Yuda wanayumba-yumba (7-13)

    • “Agano pamoja na Kifo” (14-22)

      • Jiwe la pembe lenye samani katika Sayuni (16)

      • Kazi ya Yehova yenye haiko ya kawaida (21)

    • Nizamu yenye hekima ya Yehova inaelezwa kupitia mifano (23-29)

  • 29

    • Ole wake Arieli! (1-16)

      • Heshima ya midomo tu inalaumiwa (13)

    • Viziwi watasikia; na vipofu wataona (17-24)

  • 30

    • Musaada wa Misri hauna mafaa yoyote kabisa (1-7)

    • Watu wanakataa ujumbe wa unabii (8-14)

    • Mutakuwa na nguvu kama munakuwa na tumaini (15-17)

    • Yehova anaonyesha watu wake wema (18-26)

      • Yehova, Mufundishaji Mukubwa (20)

      • “Hii ndiyo njia” (21)

    • Yehova ataleta hukumu juu ya Ashuru (27-33)

  • 31

    • Musaada wa kweli unatoka kwa Mungu, hapana kwa wanadamu (1-9)

      • Farasi wa Misri ni nyama tu (3)

  • 32

    • Mufalme na wakubwa watatawala kwa ajili ya haki ya kweli (1-8)

    • Wanamuke wenye hawahangaike wanaonywa (9-14)

    • Baraka wakati roho itamwangwa (15-20)

  • 33

    • Hukumu na tumaini kwa wenye haki (1-24)

      • Yehova ni Muamuzi, Mupaji-sheria, na Mufalme (22)

      • Hakuna mwenye atasema: “Niko mugonjwa” (24)

  • 34

    • Kisasi cha Yehova juu ya mataifa (1-8)

    • Edomu itafanywa kuwa ukiwa (9-17)

  • 35

    • Paradiso inarudishwa (1-7)

      • Vipofu wataona; viziwi watasikia (5)

    • Njia ya Utakatifu kwa ajili ya wenye walikombolewa (8-10)

  • 36

    • Senakeribu anashambulia Yuda (1-3)

    • Rabshake anamuzihaki Yehova (4-22)

  • 37

    • Hezekia anatafuta musaada wa Mungu kupitia Isaya (1-7)

    • Senakeribu anaogopesha Yerusalemu (8-13)

    • Sala ya Hezekia (14-20)

    • Isaya anajulisha jibu la Mungu (21-35)

    • Malaika anaua Waashuru elfu mia moja makumi munane na tano (36-38)

  • 38

    • Hezekia anakuwa mugonjwa kisha anapona (1-22)

      • Wimbo wa shukrani (10-20)

  • 39

    • Wajumbe kutoka Babiloni (1-8)

  • 40

    • Faraja kwa watu wa Mungu (1-11)

      • Sauti katika jangwa (3-5)

    • Ukubwa wa Mungu (12-31)

      • Mataifa ni kama tone kutoka katika mbeketi (15)

      • Mungu anakaa juu “ya muviringo wa dunia” (22)

      • Nyota zote zinaitwa kwa majina (26)

      • Mungu hachokake (28)

      • Kumutumainia Yehova kunaleta nguvu mupya (29-31)

  • 41

    • Mushindi kutoka mahali jua linatokea (1-7)

    • Israeli anachaguliwa kuwa mutumishi wa Mungu (8-20)

      • “Abrahamu rafiki yangu” (8)

    • Miungu mingine inajaribiwa (21-29)

  • 42

    • Mutumishi wa Mungu na kazi yenye alitumwa kufanya (1-9 (1-9)

      • ‘Jina langu ni Yehova’ (8)

    • Wimbo mupya wa kumusifu Yehova (10-17)

    • Israeli ni kipofu na kiziwi (18-25)

  • 43

    • Yehova anakusanya tena watu wake (1-7)

    • Miungu inajaribiwa (8-13)

      • “Muko mashahidi wangu” (10, 12)

    • Kukombolewa kutoka Babiloni (14-21)

    • “Tuende pamoja kwenye tribinali” (22-28)

  • 44

    • Baraka juu ya watu wa Mungu wenye kuchaguliwa (1-5)

    • Hakuna Mungu isipokuwa Yehova (6-8)

    • Upumbavu wa sanamu zenye kutengenezwa na wanadamu (9-20)

    • Yehova, Mukombozi wa Israeli (21-23)

    • Kurudishwa upya kupitia Koreshi (24-28)

  • 45

    • Koreshi anachaguliwa ili kukamata Babiloni (1-8)

    • Udongo haupaswe kushindana na Mufinyanzi (9-13)

    • Mataifa mengine yanatambua Israeli (14-17)

    • Mungu ni mwenye kutegemeka katika uumbaji na katika kufunua mambo (18-25)

      • Dunia iliumbwa ili ikaliwe na watu (18)

  • 46

    • Tofauti kati ya sanamu za Babiloni na Mungu wa Israeli (1-13)

      • Yehova anatabiri mambo ya wakati wenye kuja (10)

      • Ndege mwenye kuwinda kutoka mahali jua linatokea (11)

  • 47

    • Kuanguka kwa Babiloni (1-15)

      • Watu wenye elimu ya nyota wanafunuliwa (13-15)

  • 48

    • Israeli anakemewa na kusafishwa (1-11)

    • Yehova atakamata hatua juu ya Babiloni (12-16a)

    • Mafundisho ya Mungu ni yenye faida (16b-19)

    • “Mutoke katika Babiloni!” (20-22)

  • 49

    • Mugao wa mutumishi wa Yehova (1-12)

      • Mwangaza wa mataifa (6)

    • Faraja kwa Israeli (13-26)

  • 50

    • Zambi za Israeli zinaleta matatizo (1-3)

    • Mutumishi mutiifu wa Yehova (4-11)

      • Ulimi na sikio la wenye kufundishwa (4)

  • 51

    • Sayuni inarudishwa kama bustani ya Edeni (1-8)

    • Faraja kutoka kwa Mutengenezaji wa Sayuni mwenye nguvu (9-16)

    • Kikombe cha kasirani kali ya Yehova (17-23)

  • 52

    • Amuka, Ee Sayuni! (1-12)

      • Miguu yenye kupendeza ya wale wenye kuleta habari njema (7)

      • Walinzi wa Sayuni wanapandisha sauti zao pamoja (8)

      • Wale wenye kubeba vyombo vya Yehova wanapaswa kuwa safi (11)

    • Mutumishi wa Yehova atainuliwa (13-15)

      • Sura yenye kuharibika (14)

  • 53

    • Kuteseka, kufa, na kuzikwa kwa mutumishi wa Yehova (1-12)

      • Anazarauliwa na kuepukwa (3)

      • Anabeba magonjwa na maumivu (4)

      • “Kama kondoo mwenye anaenda kuchinjwa” (7)

      • Anabeba zambi za wengi (12)

  • 54

    • Sayuni mwenye kuwa tasa atakuwa na wana wengi (1-17)

      • Yehova ni bwana ya Sayuni (5)

      • Wana wa Sayuni watafundishwa na Yehova (13)

      • Silaha zenye zitapigana na Sayuni zitashindwa (17)

  • 55

    • Mualiko wa kula na kunywa bure (1-5)

    • Mumutafute Yehova na neno lake lenye kutegemeka (6-13)

      • Njia za Mungu ziko juu kuliko njia za mwanadamu (8, 9)

      • Neno la Mungu litafanikiwa hakika (10, 11)

  • 56

    • Baraka juu ya wageni na matowashi (1-8)

      • Nyumba ya sala kwa ajili ya wote (7)

    • Walinzi vipofu, imbwa wenye kuwa bubu (9-12)

  • 57

    • Mwenye haki na pia watu washikamanifu wanaangamia (1, 2)

    • Ukahaba wa kiroho wa Israeli unafunuliwa (3-13)

    • Faraja kwa watu wa hali ya chini (14-21)

      • Waovu ni kama bahari yenye kuchafuka (20)

      • Hakuna amani kwa waovu (21)

  • 58

    • Kufunga kwa kweli na kwa uongo (1-12)

    • Kushika Sabato kwa furaha (13, 14)

  • 59

    • Zambi za Israeli zinawatenga na Mungu (1-8)

    • Kuungama zambi (9-15a)

    • Yehova anaingilia kati kwa ajili ya wenye kutubu (15b-21)

  • 60

    • Utukufu wa Mungu unaangazia Sayuni (1-22)

      • Kama njiwa kwenye nyumba zao (8)

      • Zahabu mahali pa shaba (17)

      • Mudogo atakuwa elfu (22)

  • 61

    • Alitiwa mafuta ili kutangaza habari njema (1-11)

      • “Mwaka wa nia njema ya Yehova” (2)

      • “Miti mikubwa ya haki” (3)

      • Watu wa inchi zingine watasaidia (5)

      • “Makuhani wa Yehova” (6)

  • 62

    • Jina mupya la Sayuni (1-12)

  • 63

    • Kisasi cha Yehova juu ya mataifa (1-6))

    • Upendo mushikamanifu wa Yehova nyakati za zamani (7-14)

    • Sala ya kutubu (15-19)

  • 64

    • Sala ya kutubu inaendelea (1-12)

      • Yehova “Mufinyanzi wetu” (8)

  • 65

    • Hukumu ya Yehova juu ya waabudu-sanamu (1-16)

      • Mungu wa Bahati Njema na mungu wa Mambo Yenye Kupangwa Mbele ya Wakati (11)

      • “Watumishi wangu watakula” (13)

    • Mbingu mupya na dunia mupya (17-25)

      • Kujenga nyumba; kupanda mashamba ya mizabibu (21)

      • Hakuna mwenye atafanya kazi ya jasho ya bure (23)

  • 66

    • Ibada ya kweli na ibada ya uongo (1-6)

    • Mama Sayuni na wana wake (7-17)

    • Watu wanakusanyika Yerusalemu ili kuabudu (18-24)